< Waefeso 3 >

1 Kwa sababu hii, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi watu wa Mataifa:
For this cause [[I bend my knees]], I Paul, the prisoner of Christ Jesus for you gentiles;
2 Kwa hakika mmekwisha kusikia kuhusu ile huduma ya neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu,
if, indeed, ye heard of the dispensation of the grace of God which was given me toward you,
3 yaani, ile siri iliodhihirishwa kwangu kwa njia ya ufunuo, kama nilivyotangulia kuandika kwa kifupi.
that by revelation the mystery was made known to me, as I wrote before in few words,
4 Kwa kusoma haya, basi mtaweza kuelewa ufahamu wangu katika siri ya Kristo.
whereby, when ye read, ye may perceive my insight into the mystery of Christ;
5 Siri hii haikudhihirishwa kwa wanadamu katika vizazi vingine kama vile sasa ilivyodhihirishwa na Roho kwa mitume na manabii watakatifu wa Mungu.
which in other generations was not made known to the sons of men, as it hath now been revealed to his holy apostles and prophets by the Spirit;
6 Siri hii ni kwamba, kwa njia ya Injili, watu wa Mataifa ni warithi pamoja na Israeli, viungo vya mwili mmoja na washiriki pamoja wa ahadi katika Kristo Yesu.
that the gentiles are fellow-heirs, and of the same body, and partakers with us of the promise in Christ Jesus through the gospel;
7 Nimekuwa mtumishi wa Injili hii kwa kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa nguvu yake itendayo kazi.
of which I became a minister according to the gift of the grace of God, given to me according to the effectual working of his power.
8 Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii: ili niwahubirie watu wa Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo,
To me, who am less than the least of all saints, was this grace given, to make known among the gentiles the glad tidings of the unsearchable riches of Christ,
9 na kuweka wazi kwa kila mtu siri hii iliyokuwa imefichwa tangu zamani katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. (aiōn g165)
to make all men see what is the dispensation of the mystery, which hath been hidden for ages in God, who created all things; (aiōn g165)
10 Ili sasa kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na wenye mamlaka katika ulimwengu wa roho,
to the intent that now to the principalities and powers in the heavenly regions might be known through the church the manifold wisdom of God,
11 sawasawa na kusudi lake la milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn g165)
according to his purpose for ages, which he accomplished in Christ Jesus our Lord; (aiōn g165)
12 Ndani yake na kwa njia ya imani katika yeye twaweza kumkaribia Mungu kwa uhuru na kwa ujasiri.
in whom we have our boldness and our access in confidence, through faith in him.
13 Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu.
Wherefore I entreat you not to be disheartened by the troubles I am suffering for you, since they are your glory.
14 Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,
For this cause I bend my knees to the Father,
15 ambaye ubaba wote wa kila jamaa za mbinguni na za duniani unatokana naye.
from whom every family in heaven and on earth receiveth its name,
16 Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
that he would grant you, according to the riches of his glory, to be strengthened with might by his Spirit in the inner man;
17 ili kwamba, Kristo apate kukaa mioyoni mwenu kwa njia ya imani. Nami ninaomba kwamba ninyi mkiwa wenye mizizi tena imara katika msingi wa upendo,
that Christ may dwell in your hearts by faith, ye having been rooted and grounded in love,
18 mwe na uwezo wa kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, urefu, kimo na kina upendo wa Kristo,
that ye may be able to comprehend, with all the saints, what is the breadth, and length, and depth, and height,
19 na kujua upendo huu unaopita fahamu, ili mpate kujazwa na kufikia kipimo cha ukamilifu wote wa Mungu.
and to know the love of Christ, which passeth knowledge, that ye may be filled unto all the fullness of God.
20 Basi kwa yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu yasiyopimika kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya uweza wake ule utendao kazi ndani yetu,
Now unto him that is able to do exceeding abundantly above all that we ask or think, according to the power that worketh in us,
21 yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen. (aiōn g165)
to him be the glory in the church in Christ Jesus throughout all generations, for ever and ever. Amen. (aiōn g165)

< Waefeso 3 >