< Waefeso 3 >

1 Kwa sababu hii, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi watu wa Mataifa:
For this reason I, Paul, the prisoner of Christ Jesus on behalf of you Gentiles—
2 Kwa hakika mmekwisha kusikia kuhusu ile huduma ya neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu,
surely you have heard of the dispensation of the grace of God that was given to me for you,
3 yaani, ile siri iliodhihirishwa kwangu kwa njia ya ufunuo, kama nilivyotangulia kuandika kwa kifupi.
how that by revelation He made known to me the ‘secret’ (as I have written briefly already,
4 Kwa kusoma haya, basi mtaweza kuelewa ufahamu wangu katika siri ya Kristo.
with reference to which, when you read, you can understand my insight into Christ's secret),
5 Siri hii haikudhihirishwa kwa wanadamu katika vizazi vingine kama vile sasa ilivyodhihirishwa na Roho kwa mitume na manabii watakatifu wa Mungu.
which in different generations was not made known to the sons of men, as it has now been revealed by Spirit to His holy apostles and prophets:
6 Siri hii ni kwamba, kwa njia ya Injili, watu wa Mataifa ni warithi pamoja na Israeli, viungo vya mwili mmoja na washiriki pamoja wa ahadi katika Kristo Yesu.
that the Gentiles are joint-heirs, of the same body, and fellow partakers of His promise in the Christ through the Gospel,
7 Nimekuwa mtumishi wa Injili hii kwa kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa nguvu yake itendayo kazi.
of which I became a servant according to the gift of God's grace, the gift given to me according to the outworking of His power.
8 Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii: ili niwahubirie watu wa Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo,
To me, the very least of all saints, was this grace given, to preach among the Gentiles the unsearchable riches of Christ,
9 na kuweka wazi kwa kila mtu siri hii iliyokuwa imefichwa tangu zamani katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. (aiōn g165)
and to enlighten all as to the program of the secret that from the beginning of the ages has been hidden by the God who created all things through Jesus Christ; (aiōn g165)
10 Ili sasa kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na wenye mamlaka katika ulimwengu wa roho,
to the intent that now, through the Church, the manifold wisdom of God might be made known to the rulers and the authorities in the heavenly realms,
11 sawasawa na kusudi lake la milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn g165)
according to the eternal purpose that He accomplished by Christ Jesus our Lord, (aiōn g165)
12 Ndani yake na kwa njia ya imani katika yeye twaweza kumkaribia Mungu kwa uhuru na kwa ujasiri.
in whom we have the boldness and the access with confidence through faith in Him.
13 Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu.
Therefore I ask that you not lose heart at my afflictions on your behalf, which is your glory.
14 Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,
For this reason I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
15 ambaye ubaba wote wa kila jamaa za mbinguni na za duniani unatokana naye.
from whom every family in heaven and on earth receives its name,
16 Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
that He[F] may grant you, according to the riches of His glory: 1) to be strengthened with power by His Spirit in the inner man;
17 ili kwamba, Kristo apate kukaa mioyoni mwenu kwa njia ya imani. Nami ninaomba kwamba ninyi mkiwa wenye mizizi tena imara katika msingi wa upendo,
2) Christ to dwell in your hearts through the Faith, having been rooted and established in love
18 mwe na uwezo wa kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, urefu, kimo na kina upendo wa Kristo,
so that you may be fully able to grasp (with all saints) what is the breadth and length and depth and height;
19 na kujua upendo huu unaopita fahamu, ili mpate kujazwa na kufikia kipimo cha ukamilifu wote wa Mungu.
and 3) to know the love of Christ that surpasses knowledge—so that you may be fulfilled into all the fullness of God.
20 Basi kwa yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu yasiyopimika kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya uweza wake ule utendao kazi ndani yetu,
Now to Him who is able to do immeasurably more than all we ask or imagine, according to the power that is working in us,
21 yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen. (aiōn g165)
to Him be the glory in the Church in Christ Jesus, to all generations, forever and ever. Amen. (aiōn g165)

< Waefeso 3 >