< Waefeso 3 >
1 Kwa sababu hii, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi watu wa Mataifa:
For this reason I Paul, prisoner of the Christ Jesus for you nations,
2 Kwa hakika mmekwisha kusikia kuhusu ile huduma ya neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu,
(if indeed ye have heard of the administration of the grace of God which has been given to me towards you,
3 yaani, ile siri iliodhihirishwa kwangu kwa njia ya ufunuo, kama nilivyotangulia kuandika kwa kifupi.
that by revelation the mystery has been made known to me, (according as I have written before briefly,
4 Kwa kusoma haya, basi mtaweza kuelewa ufahamu wangu katika siri ya Kristo.
by which, in reading it, ye can understand my intelligence in the mystery of the Christ, )
5 Siri hii haikudhihirishwa kwa wanadamu katika vizazi vingine kama vile sasa ilivyodhihirishwa na Roho kwa mitume na manabii watakatifu wa Mungu.
which in other generations has not been made known to the sons of men, as it has now been revealed to his holy apostles and prophets in [the power of the] Spirit,
6 Siri hii ni kwamba, kwa njia ya Injili, watu wa Mataifa ni warithi pamoja na Israeli, viungo vya mwili mmoja na washiriki pamoja wa ahadi katika Kristo Yesu.
that [they who are of] the nations should be joint heirs, and a joint body, and joint partakers of [his] promise in Christ Jesus by the glad tidings;
7 Nimekuwa mtumishi wa Injili hii kwa kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa nguvu yake itendayo kazi.
of which I am become minister according to the gift of the grace of God given to me, according to the working of his power.
8 Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii: ili niwahubirie watu wa Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo,
To me, less than the least of all saints, has this grace been given, to announce among the nations the glad tidings of the unsearchable riches of the Christ,
9 na kuweka wazi kwa kila mtu siri hii iliyokuwa imefichwa tangu zamani katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. (aiōn )
and to enlighten all [with the knowledge of] what is the administration of the mystery hidden throughout the ages in God, who has created all things, (aiōn )
10 Ili sasa kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na wenye mamlaka katika ulimwengu wa roho,
in order that now to the principalities and authorities in the heavenlies might be made known through the assembly the all-various wisdom of God,
11 sawasawa na kusudi lake la milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn )
according to [the] purpose of the ages, which he purposed in Christ Jesus our Lord, (aiōn )
12 Ndani yake na kwa njia ya imani katika yeye twaweza kumkaribia Mungu kwa uhuru na kwa ujasiri.
in whom we have boldness and access in confidence by the faith of him.
13 Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu.
Wherefore I beseech [you] not to faint through my tribulations for you, which is your glory.
14 Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,
For this reason I bow my knees to the Father [of our Lord Jesus Christ],
15 ambaye ubaba wote wa kila jamaa za mbinguni na za duniani unatokana naye.
of whom every family in [the] heavens and on earth is named,
16 Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
in order that he may give you according to the riches of his glory, to be strengthened with power by his Spirit in the inner man;
17 ili kwamba, Kristo apate kukaa mioyoni mwenu kwa njia ya imani. Nami ninaomba kwamba ninyi mkiwa wenye mizizi tena imara katika msingi wa upendo,
that the Christ may dwell, through faith, in your hearts, being rooted and founded in love,
18 mwe na uwezo wa kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, urefu, kimo na kina upendo wa Kristo,
in order that ye may be fully able to apprehend with all the saints what [is] the breadth and length and depth and height;
19 na kujua upendo huu unaopita fahamu, ili mpate kujazwa na kufikia kipimo cha ukamilifu wote wa Mungu.
and to know the love of the Christ which surpasses knowledge; that ye may be filled [even] to all the fulness of God.
20 Basi kwa yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu yasiyopimika kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya uweza wake ule utendao kazi ndani yetu,
But to him that is able to do far exceedingly above all which we ask or think, according to the power which works in us,
21 yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen. (aiōn )
to him be glory in the assembly in Christ Jesus unto all generations of the age of ages. Amen). (aiōn )