< Waefeso 3 >
1 Kwa sababu hii, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi watu wa Mataifa:
For this cause I, Paul, am the prisoner of Christ Jesus on behalf of you Gentiles,
2 Kwa hakika mmekwisha kusikia kuhusu ile huduma ya neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu,
if it is so that you have heard of the administration of that grace of God which was given me toward you,
3 yaani, ile siri iliodhihirishwa kwangu kwa njia ya ufunuo, kama nilivyotangulia kuandika kwa kifupi.
how that by revelation the mystery was made known to me, as I wrote before in few words,
4 Kwa kusoma haya, basi mtaweza kuelewa ufahamu wangu katika siri ya Kristo.
by which, when you read, you can perceive my understanding in the mystery of Christ,
5 Siri hii haikudhihirishwa kwa wanadamu katika vizazi vingine kama vile sasa ilivyodhihirishwa na Roho kwa mitume na manabii watakatifu wa Mungu.
which in other generations was not made known to the children of men, as it has now been revealed to his holy apostles and prophets in the Spirit,
6 Siri hii ni kwamba, kwa njia ya Injili, watu wa Mataifa ni warithi pamoja na Israeli, viungo vya mwili mmoja na washiriki pamoja wa ahadi katika Kristo Yesu.
that the Gentiles are fellow heirs and fellow members of the body, and fellow partakers of his promise in Christ Jesus through the Good News,
7 Nimekuwa mtumishi wa Injili hii kwa kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa nguvu yake itendayo kazi.
of which I was made a servant according to the gift of that grace of God which was given me according to the working of his power.
8 Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii: ili niwahubirie watu wa Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo,
To me, the very least of all saints, was this grace given, to preach to the Gentiles the unsearchable riches of Christ,
9 na kuweka wazi kwa kila mtu siri hii iliyokuwa imefichwa tangu zamani katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. (aiōn )
and to make all men see what is the administration of the mystery which for ages (aiōn ) has been hidden in God, who created all things through Jesus Christ,
10 Ili sasa kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na wenye mamlaka katika ulimwengu wa roho,
to the intent that now through the assembly the manifold wisdom of God might be made known to the principalities and the powers in the heavenly places,
11 sawasawa na kusudi lake la milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn )
according to the purpose of the ages (aiōn ) which he accomplished in Christ Jesus our Lord.
12 Ndani yake na kwa njia ya imani katika yeye twaweza kumkaribia Mungu kwa uhuru na kwa ujasiri.
In him we have boldness and access in confidence through our faith in him.
13 Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu.
Therefore I ask that you may not lose heart at my troubles for you, which are your glory.
14 Kwa sababu hii nampigia Baba magoti,
For this cause, I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
15 ambaye ubaba wote wa kila jamaa za mbinguni na za duniani unatokana naye.
from whom every family in heaven and on earth is named,
16 Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kwa njia ya Roho wake kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
that he would grant you, according to the riches of his glory, that you may be strengthened with power through his Spirit in the inner person,
17 ili kwamba, Kristo apate kukaa mioyoni mwenu kwa njia ya imani. Nami ninaomba kwamba ninyi mkiwa wenye mizizi tena imara katika msingi wa upendo,
that Christ may dwell in your hearts through faith, to the end that you, being rooted and grounded in love,
18 mwe na uwezo wa kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, urefu, kimo na kina upendo wa Kristo,
may be strengthened to comprehend with all the saints what is the width and length and height and depth,
19 na kujua upendo huu unaopita fahamu, ili mpate kujazwa na kufikia kipimo cha ukamilifu wote wa Mungu.
and to know Christ’s love which surpasses knowledge, that you may be filled with all the fullness of God.
20 Basi kwa yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu yasiyopimika kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya uweza wake ule utendao kazi ndani yetu,
Now to him who is able to do exceedingly abundantly above all that we ask or think, according to the power that works in us,
21 yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen. (aiōn )
to him be the glory in the assembly and in Christ Jesus to all generations for the age (aiōn ) of the ages (aiōn ). Amen.