< Waefeso 2 >

1 Kwa habari zenu, mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu,
and you also [[he raised up]], who were dead through your trespasses and sins,
2 ambazo mlizitenda mlipofuatisha namna ya ulimwengu huu na za yule mtawala wa ufalme wa anga, yule roho atendaye kazi sasa ndani ya wale wasiotii. (aiōn g165)
in which ye once walked according to the course of this world, according to the prince of the powers of the air, the spirit that is now working in the sons of disobedience; (aiōn g165)
3 Sisi sote pia tuliishi katikati yao hapo zamani, tukitimiza tamaa za asili yetu ya dhambi na kufuata tamaa zake na mawazo yake. Nasi kwa asili tulikuwa wana wa ghadhabu, kama mtu mwingine yeyote.
among whom even we all had our way of life in times past in the lusts of our flesh, fulfilling the desires of the flesh and of the thoughts, and were by nature children of wrath, even as others;
4 Lakini Mungu kwa upendo wake mwingi kwetu sisi, ambaye ni mwingi wa rehema,
but God, who is rich in mercy, on account of his great love wherewith he loved us, gave to us,
5 hata tulipokuwa wafu kwa ajili ya makosa yetu, alitufanya tuwe hai pamoja na Kristo Yesu, yaani, mmeokolewa kwa neema.
even when dead through our trespasses, life with Christ, —by grace have ye been saved, —
6 Mungu alitufufua pamoja na Kristo na kutuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu,
and raised us up with him, and caused us to sit with him in the heavenly regions in Christ Jesus,
7 ili katika ule ulimwengu ujao apate kuonyesha wingi wa neema yake isiyopimika, iliyodhihirishwa kwetu kwa wema wake ndani ya Kristo Yesu. (aiōn g165)
that he might show in the ages to come the exceeding riches of his grace in kindness toward us in Christ Jesus. (aiōn g165)
8 Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, wala si kwa matendo yenu mema. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu,
For by grace ye have been saved, through faith; and this is not of yourselves; it is the gift of God;
9 si kwa matendo, ili mtu yeyote asije akajisifu.
not of works, lest any one should boast.
10 Kwa maana sisi ni kazi ya mikono ya Mungu, tulioumbwa katika Kristo Yesu, ili tupate kutenda matendo mema, ambayo Mungu alitangulia kuyaandaa tupate kuishi katika hayo.
For we are his workmanship, created in Christ Jesus unto good works, which God before prepared that we should walk in them.
11 Kwa hiyo kumbukeni kwamba ninyi ambao hapo awali mlikuwa watu wa Mataifa kwa kuzaliwa na kuitwa “wasiotahiriwa” na wale wanaojiita “waliotahiriwa” (yaani tohara ifanyikayo katika mwili kwa mikono ya wanadamu),
Wherefore remember, that in time past ye, the gentiles in the flesh, who are called uncircumcised by those who are called circumcised, having the circumcision of the flesh, performed by hand, —
12 kumbukeni kwamba wakati ule mlikuwa mbali na Kristo, mkiwa mmetengwa kutoka jumuiya ya Israeli, na mkiwa wageni katika yale maagano ya ahadi, nanyi mkiwa hamna tumaini wala Mungu duniani.
that ye were at that time without Christ, being aliens from the commonwealth of Israel, and strangers to the covenants of the promise, having no hope, and without God, in the world;
13 Lakini sasa katika Kristo Yesu, ninyi ambao hapo kwanza mlikuwa mbali na Mungu, sasa mmeletwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo.
but now, in Christ Jesus, ye, who formerly were afar off, have been brought nigh by the blood of Christ.
14 Kwa maana yeye mwenyewe ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi tuliokuwa wawili, yaani, Wayahudi na watu wa Mataifa, tuwe wamoja kwa kuvunja kizuizi na kubomoa ule ukuta wa uadui uliokuwa kati yetu,
For it is he who is our peace, who made both one, and broke down the middle wall of partition between us, that is, the enmity;
15 kwa kuibatilisha ile sheria pamoja na amri zake na maagizo yake alipoutoa mwili wake, ili apate kufanya ndani yake mtu mmoja mpya badala ya hao wawili, hivyo akifanya amani,
having abolished in his flesh the law of commandments contained in ordinances; that he might create of the two one new man in himself, thus making peace,
16 naye katika mwili huu mmoja awapatanishe wote wawili na Mungu kupitia msalaba, ili kwa huo msalaba akaangamiza uadui wao.
and might reconcile both to God in one body by the cross, having slain on it the enmity.
17 Alikuja na kuhubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali na pia akahubiri amani kwao waliokuwa karibu.
And he came and brought the glad tidings of peace to you who were afar off, and of peace to those that were near;
18 Kwa maana kwa kupitia kwake, sisi sote tunaweza kumkaribia Baba katika Roho mmoja.
for through him we both have our access in one Spirit to the Father.
19 Hivyo basi, ninyi sasa si wageni tena wala wapitaji, bali mmekuwa wenyeji pamoja na watakatifu na pia jamaa wa nyumbani mwake Mungu.
So then ye are no longer strangers and foreigners, but are fellow-citizens with the saints, and members of the household of God,
20 Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ndiye jiwe kuu la pembeni.
and are built upon the foundation of the apostles and prophets, Christ Jesus himself being the chief corner-stone;
21 Ndani yake jengo lote limeshikamanishwa pamoja na kusimamishwa ili kuwa Hekalu takatifu katika Bwana.
in whom all the building, fitly framed together, is growing into a holy temple in the Lord;
22 Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja ili mpate kuwa makao ambayo Mungu anaishi ndani yake kwa njia ya Roho wake.
in whom ye also are built together into a dwelling-place of God in the Spirit.

< Waefeso 2 >