< Mhubiri 9 >

1 Kwa hiyo niliyatafakari yote haya nikafikia uamuzi kwamba waadilifu na wenye hekima na yale wanayoyafanya yako mikononi mwa Mungu, lakini hakuna mtu ajuaye kama anangojewa na upendo au chuki.
Kajti vse to sem preudaril v svojem srcu, celo da vse to oznanim, da so pravični in modri in njihova dela v roki Boga. Noben človek ne spozna bodisi ljubezni ali sovraštva po vsem, kar je pred njimi.
2 Wote wanayo hatima inayofanana, mwadilifu na mwovu, mwema na mbaya, aliye safi na aliye najisi, wale wanaotoa dhabihu na wale wasiotoa. Kama ilivyo kwa mtu mwema, ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye dhambi; kama ilivyo kwa wale wanaoapa, ndivyo ilivyo kwa wale wasioapa.
Vse stvari pridejo podobno k vsem: je en dogodek pravičnemu in zlobnemu; dobremu, čistemu in nečistemu; tistemu, ki daruje in tistemu, ki ne daruje; kakor je dobri, tako je grešnik; in kdor prisega, kakor tisti, ki se prisege boji.
3 Huu ni ubaya ulio katika kila kitu kinachotendeka chini ya jua: Mwisho unaofanana huwapata wote. Zaidi ya hayo, mioyo ya watu, imejaa ubaya na kuna wazimu mioyoni mwao wangali hai, hatimaye huungana na waliokufa.
To je zlo med vsemi stvarmi, ki so storjene pod soncem, da je en dogodek za vse. Da, tudi srce človeških sinov je polno zla in dokler živijo je v njihovih srcih norost, potem pa gredo k smrti.
4 Yeyote aliye miongoni mwa walio hai analo tumaini, hata mbwa hai ni bora kuliko simba aliyekufa!
Kajti za tistega, ki je pridružen k vsem živim, je upanje, kajti živ pes je boljši kakor mrtev lev.
5 Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui chochote, hawana tuzo zaidi, hata kumbukumbu yao imesahaulika.
Kajti živi vedo, da bodo umrli, toda mrtvi ne vedo ničesar niti nimajo več nobene nagrade, kajti spomin nanje je pozabljen.
6 Upendo wao, chuki yao na wivu wao vimetoweka tangu kitambo, kamwe hawatakuwa tena na sehemu katika lolote linalotendeka chini ya jua.
Prav tako je njihova ljubezen, njihovo sovraštvo in njihova zavist sedaj izginila niti nimajo več deleža na veke v katerikoli stvari, ki je storjena pod soncem.
7 Nenda, kula chakula chako kwa furaha, unywe divai yako kwa moyo wa shangwe, kwa maana sasa Mungu anakubali unachofanya.
Pojdi svojo pot, svoj kruh jej z radostjo in svoje vino pij z veselim srcem, kajti Bog sedaj sprejema tvoja dela.
8 Daima uvae nguo nyeupe na daima upake kichwa chako mafuta.
Naj bodo tvoje obleke vedno bele in tvoji glavi naj ne manjka mazila.
9 Furahia maisha na mke wako, umpendaye, siku zote za maisha ya ubatili uliyopewa na Mungu chini ya jua, siku zote za ubatili. Kwa maana hili ndilo fungu lako katika maisha na katika kazi yako ya taabu chini ya jua.
Živi radostno, z ženo, ki jo ljubiš, vse dni življenja svoje ničevosti, ki ti je dana pod soncem vse dni tvoje ničevosti, kajti to je tvoj delež v tem življenju in v tvojem trudu, ki se ga lotevaš pod soncem.
10 Lolote mkono wako upatalo kufanya, fanya kwa nguvu zako zote, kwa kuwa huko kuzimu, unakokwenda, hakuna kufanya kazi wala mipango wala maarifa wala hekima. (Sheol h7585)
Karkoli tvoja roka najde, da stori, to stôri z vso svojo močjo, kajti v grobu, kamor greš, ni dela, niti naklepa, niti spoznanja, niti modrosti. (Sheol h7585)
11 Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.
Vrnil sem se in videl pod soncem, da tek ni za nagle, niti bitka za močne, niti kruh za modre, niti bogastva za ljudi spoznanja, niti celo naklonjenost veščim ljudem, temveč se čas in priložnost dogajata njim vsem.
12 Zaidi ya hayo, hakuna mwanadamu ajuaye wakati saa yake itakapokuja: Kama vile samaki wavuliwavyo katika wavu mkatili, au ndege wanaswavyo kwenye mtego, vivyo hivyo wanadamu hunaswa na nyakati mbaya zinazowaangukia bila kutazamia.
Kajti tudi človek ne pozna svojega časa. Kakor ribe, ki so ujete v zlo mrežo in kakor ptice, ki so ujete v zanko, tako so človeški sinovi ujeti v zlobnem času, ko le-ta nenadoma pade nanje.
13 Pia niliona chini ya jua mfano huu wa hekima ambao ulinivutia sana:
Tudi to modrost sem videl pod soncem in ta se mi je zdela velika:
14 Palikuwa na mji mdogo uliokuwa na watu wachache ndani yake. Mfalme mwenye nguvu akainuka dhidi yake, akauzunguka akaweka jeshi kubwa dhidi yake.
bilo je majhno mesto in znotraj njega malo ljudi in zoper njega je prišel velik kralj, ga oblegal in zoper njega zgradil velike branike.
15 Katika mji huo kulikuwepo mtu mmoja maskini lakini mwenye hekima, naye akauokoa ule mji kwa hekima yake. Lakini hakuna aliyemkumbuka yule maskini.
Torej v njem je bil najden reven, moder človek in on je s svojo modrostjo osvobodil mesto, vendar se noben človek ni spominjal tega ubogega moža.
16 Kwa hiyo, nikasema, “Hekima ni bora kuliko nguvu.” Lakini hekima ya maskini imedharauliwa, wala hakuna anayesikiliza maneno yake.
Potem sem rekel: »Modrost je boljša kakor moč; kljub temu je modrost revnega moža prezirana in njegove besede niso slišane.«
17 Maneno ya utulivu ya mwenye hekima husikiwa kuliko makelele ya mtawala wa wapumbavu.
Besede modrih ljudi se bolj slišijo v tišini kakor vpitje tistega, ki vlada med bedaki.
18 Hekima ni bora kuliko silaha za vita, lakini mwenye dhambi mmoja huharibu mema mengi.
Modrost je boljša kakor bojna orožja, toda en grešnik uničuje mnogo dobrega.

< Mhubiri 9 >