< Mhubiri 7 >
1 Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi, nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa.
Laba slava ir labāka nekā salda eļļa, un miršanas diena labāka nekā dzimšanas diena.
2 Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu, kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu, imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao.
Labāki ir vaidu namā iet nekā dzīru namā; jo tas ir visu cilvēku gals, un tas, kas dzīvo, to ņem pie sirds.
3 Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.
Noskumt ir labāki nekā smieties; jo kad vaigs noskumis, tas sirdij labi.
4 Moyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa.
Gudru ļaužu sirds ir vaidu namā, bet ģeķu sirds ir prieku namā.
5 Afadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima, kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
Labāk ir klausīties gudra vīra rāšanu, nekā klausīties ģeķa dziesmu.
6 Kama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Hili nalo pia ni ubatili.
Jo kā ērkšķi sprakst apakš poda, tāpat ir ģeķa smiešanās, - tā ir arī niecība.
7 Dhuluma humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, nayo rushwa huuharibu moyo.
Tiešām, netaisna peļņa arī gudru padara neprātīgu, un dāvanas samaitā sirdi.
8 Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake, uvumilivu ni bora kuliko kiburi.
Labāks ir kādas lietas gals nekā viņas iesākums. Lēnprātīgais ir labāks nekā lepnais.
9 Usiwe mwepesi kukasirika rohoni mwako, kwa kuwa hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
Neesi ātrs savā prātā dusmot, jo dusmība mājo ģeķu azotē.
10 Usiseme, “Kwa nini siku za kale zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa maana si hekima kuuliza maswali kama hayo.
Nesaki: kā tas nāk, ka senās dienas bijušas labākas nekā šīs! Jo ar gudrību tu to nevaicā.
11 Hekima, kama ulivyo urithi, ni kitu chema na huwafaidia wale walionalo jua.
Gudrība ir tik laba kā mantība un labums tiem, kas sauli redz.
12 Hekima ni ulinzi kama fedha ilivyo ulinzi, lakini faida ya maarifa ni hii: kwamba hekima huhifadhi maisha ya aliye nayo.
Jo gudrības pavēnī ir kā naudas pavēnī; un tas ir atzīšanas labums, ka gudrība dod dzīvību tiem, kam tā ir.
13 Tafakari kile Mungu alichokitenda: Nani awezaye kunyoosha kile ambacho yeye amekipinda?
Uzlūko Dieva darbu, jo kas to var darīt taisnu, ko viņš ir darījis līku?
14 Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi, lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari: Mungu amefanya hiyo moja, naam, sanjari na hiyo nyingine. Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.
Baudi labumu labā dienā, bet ļaunu dienu ņem arī par labu; jo Dievs dara gan šo gan to, tāpēc ka cilvēkam nebūs zināt, kas būs pēc viņa.
15 Katika maisha haya yangu ya ubatili nimeshaona haya mawili: mtu mwadilifu akiangamia katika uadilifu wake, naye mtu mwovu akiishi maisha marefu katika uovu wake.
Visu to esmu redzējis savas niecības dienās: Cits ir taisns, kas savā taisnībā iet bojā, un cits ir bezdievīgs, kas savā blēdībā ilgi pastāv.
16 Usiwe mwenye haki kupita kiasi, wala usiwe na hekima kupita kiasi: kwa nini kujiangamiza mwenyewe?
Neesi pārlieku taisns un neturies pats par visai gudru, - kāpēc tu gribi iet bojā?
17 Usiwe mwovu kupita kiasi, wala usiwe mpumbavu: kwa nini kufa kabla ya wakati wako?
Neesi pārlieku bezdievīgs, un neesi visai ģeķīgs; kāpēc tu gribi nomirt nelaikā?
18 Ni vyema kushika hilo moja na wala usiache hilo jingine likupite. Mtu amchaye Mungu ataepuka huko kupita kiasi.
Labi ir, ka tu šo satver un arī no tā otra savu roku neatrauj; jo kas Dievu bīstas, tas no visa tā izsprūk.
19 Hekima humfanya yeye aliye nayo kuwa na uwezo zaidi kuliko watawala kumi katika mji.
Gudrība stiprina gudro vairāk nekā desmit vareni, kas ir pilsētā.
20 Hakuna mtu mwenye haki duniani ambaye hufanya mambo ya haki na kamwe asitende dhambi.
Tiešām, nav neviena cilvēka, kas taisns būtu virs zemes, kas labi darītu un negrēkotu.
21 Usitie maanani kila neno linalosemwa na watu, la sivyo, waweza kumsikia mtumishi wako akikulaani:
Neliec arī vērā visus vārdus, kas top runāti, lai tev nav jādzird, ka tavs kalps tev lād.
22 kwa kuwa unafahamu moyoni mwako kwamba wewe mwenyewe mara nyingi umewalaani wengine.
Jo daudzkārt arī tava sirds zin, ka arī tu citus esi lādējis.
23 Yote haya niliyajaribu kwa hekima, nikasema, “Nimeamua kuwa na hekima”: lakini hii ilikuwa nje ya uwezo wangu.
Visu šo es ar gudrību esmu izmeklējis. Es sacīju: es dabūšu gudrību, bet viņa bija vēl tālu no manis.
24 Vyovyote hekima ilivyo, hekima iko mbali sana na imejificha, ni nani awezaye kuigundua?
Tālu ir, kas ir, un ļoti dziļš; kas to var atrast?
25 Nikageuza fikira zangu ili kuelewa, kuchunguza na kuitafuta hekima na kusudi la mambo, na ili kuelewa ujinga wa uovu, na wazimu wa upumbavu.
Es griezos ar savu sirdi, ka es zinātu un izvaicātu un meklētu gudrību un skaidrību, un ka es atzītu bezdievību par ģeķību un neprātību par nelietību.
26 Nimeona jambo lililo chungu kuliko mauti, mwanamke ambaye ni mtego, ambaye moyo wake ni wavu wa kutegea na mikono yake ni minyororo. Mtu ampendezaye Mungu atamkwepa, bali mwenye dhambi atanaswa naye.
Un es atradu vienu lietu rūgtāku nekā nāvi: sievu, kā sirds ir tīkli un valgi un kā rokas ir saites. Kas labs ir Dieva priekšā, tas no viņas izglābsies, bet grēcinieks caur viņu taps sagūstīts.
27 Mhubiri anasema, “Tazama, hili ndilo nililogundua: “Nimegundua kitu kimoja baada ya kingine nilipokuwa katika kusudi la mambo:
Redzi, šo esmu atradis, saka tas mācītājs, citu pēc cita, ka es to galavārdu atrastu.
28 ningali natafiti lakini sipati: nilimpata mwanaume mmoja mnyofu miongoni mwa elfu, lakini hakuna mwanamke mmoja mnyofu miongoni mwao.
To mana dvēsele vēl meklē, un to es vēl neesmu atradis: Starp tūkstošiem es vienu vīru esmu atradis, bet sievu starp šiem visiem es neesmu atradis.
29 Hili ndilo peke yake nililolipata: Mungu amemuumba mwanadamu mnyofu, lakini mwanadamu amebuni mambo mengi.”
Bet redzi, to tikai es esmu atradis, ka Dievs cilvēku ir radījis taisnu, bet tie dodas uz daudz gudrošanām.