< Mhubiri 7 >

1 Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi, nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa.
A good name is better than precious oil, and the day of death, better than the day of one's birth.
2 Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu, kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu, imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao.
It is better to go to the house of mourning than to go to the house of feasting; inasmuch as that is the end of all men: and let the living lay it to his heart.
3 Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.
Better is vexation than laughing; for through the sadness of the countenance the heart is made better.
4 Moyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa.
The heart of the wise is in the house of mourning; but the heart of fools is in the house of joy.
5 Afadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima, kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
It is better to hear the rebuke of the wise, than that a man should hear the song of fools.
6 Kama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Hili nalo pia ni ubatili.
For as the crackling of thorns under a pot, so is the laughter of the fool. Also this is vanity.
7 Dhuluma humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, nayo rushwa huuharibu moyo.
For [exercising] oppression maketh a wise man mad; and bribery corrupteth the heart.
8 Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake, uvumilivu ni bora kuliko kiburi.
Better is the end of a thing than the beginning thereof: better is the patient in spirit than the proud in spirit.
9 Usiwe mwepesi kukasirika rohoni mwako, kwa kuwa hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
Be not rash in thy spirit to be angry; for anger resteth in bosom of fools.
10 Usiseme, “Kwa nini siku za kale zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa maana si hekima kuuliza maswali kama hayo.
Thou must not say, How was it that the former days were better than these? for it is not out of wisdom that thou askest concerning this.
11 Hekima, kama ulivyo urithi, ni kitu chema na huwafaidia wale walionalo jua.
Wisdom is better than an inheritance, yea, preferable for those that see the sun;
12 Hekima ni ulinzi kama fedha ilivyo ulinzi, lakini faida ya maarifa ni hii: kwamba hekima huhifadhi maisha ya aliye nayo.
For under the shadow of wisdom [a man is equally well as] under the shadow of money; but the superior excellency of knowledge is, that wisdom giveth life to him that possesseth it.
13 Tafakari kile Mungu alichokitenda: Nani awezaye kunyoosha kile ambacho yeye amekipinda?
Consider [then] the work of God; for who can make straight what he hath made crooked?
14 Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi, lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari: Mungu amefanya hiyo moja, naam, sanjari na hiyo nyingine. Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.
On the day of prosperity be happy, but on the day of adversity look on: also this hath God made in equal measure with the other, to the end that man should not find the least to censure him.
15 Katika maisha haya yangu ya ubatili nimeshaona haya mawili: mtu mwadilifu akiangamia katika uadilifu wake, naye mtu mwovu akiishi maisha marefu katika uovu wake.
All things have I seen in the days of my vanity: there is many a righteous man that perisheth in his righteousness, and there is many a wicked man that liveth long in his wickedness.—
16 Usiwe mwenye haki kupita kiasi, wala usiwe na hekima kupita kiasi: kwa nini kujiangamiza mwenyewe?
Be not righteous over much; neither show thyself over wise: why wouldst thou destroy thyself?
17 Usiwe mwovu kupita kiasi, wala usiwe mpumbavu: kwa nini kufa kabla ya wakati wako?
Be not wicked over much, and be no fool: why wouldst thou die before thy time?
18 Ni vyema kushika hilo moja na wala usiache hilo jingine likupite. Mtu amchaye Mungu ataepuka huko kupita kiasi.
It is good that thou shouldst take hold of that, and that also from this thou withdraw not thy hand; for he that feareth God will come forth out of them all.
19 Hekima humfanya yeye aliye nayo kuwa na uwezo zaidi kuliko watawala kumi katika mji.
Wisdom giveth more strength to the wise than ten rulers which were in the city.
20 Hakuna mtu mwenye haki duniani ambaye hufanya mambo ya haki na kamwe asitende dhambi.
For no man is so righteous upon earth, that he should do always good, and never sin.—
21 Usitie maanani kila neno linalosemwa na watu, la sivyo, waweza kumsikia mtumishi wako akikulaani:
Also take no heed unto all the words that are spoken: lest thou hear thy servant cursing thee.
22 kwa kuwa unafahamu moyoni mwako kwamba wewe mwenyewe mara nyingi umewalaani wengine.
For oftentimes also doth thy own heart know that thou thyself likewise hast cursed others.—
23 Yote haya niliyajaribu kwa hekima, nikasema, “Nimeamua kuwa na hekima”: lakini hii ilikuwa nje ya uwezo wangu.
All this have I proved by wisdom: I said, I will be wise; but it was far from me.
24 Vyovyote hekima ilivyo, hekima iko mbali sana na imejificha, ni nani awezaye kuigundua?
Far is what formerly was so, and what was deep remaineth deep: who can find it out?
25 Nikageuza fikira zangu ili kuelewa, kuchunguza na kuitafuta hekima na kusudi la mambo, na ili kuelewa ujinga wa uovu, na wazimu wa upumbavu.
Then I turned myself about together with my heart to know, and to search, and to seek out wisdom, and experience, and to know the wickedness of folly, and the foolishness of madness.
26 Nimeona jambo lililo chungu kuliko mauti, mwanamke ambaye ni mtego, ambaye moyo wake ni wavu wa kutegea na mikono yake ni minyororo. Mtu ampendezaye Mungu atamkwepa, bali mwenye dhambi atanaswa naye.
And I find as more bitter than death the woman, whose heart is snares and nets, and whose hands are bonds: he that is deemed good before God will escape from her; but the sinner will be caught by her.
27 Mhubiri anasema, “Tazama, hili ndilo nililogundua: “Nimegundua kitu kimoja baada ya kingine nilipokuwa katika kusudi la mambo:
Behold, this have I found, saith Koheleth, [adding] one to the other, to find experience,
28 ningali natafiti lakini sipati: nilimpata mwanaume mmoja mnyofu miongoni mwa elfu, lakini hakuna mwanamke mmoja mnyofu miongoni mwao.
What my soul constantly sought, but I found it not; one man among a thousand did I find; but a woman among all these did I not find.
29 Hili ndilo peke yake nililolipata: Mungu amemuumba mwanadamu mnyofu, lakini mwanadamu amebuni mambo mengi.”
Lo, this only did I find, that God hath made man upright; but they have sought for many [sinful] devices.

< Mhubiri 7 >