< Mhubiri 6 >

1 Nimeona ubaya mwingine chini ya jua, nao unalemea sana wanadamu:
Je zlo, ki sem ga videl pod soncem in to je pogosto med ljudmi.
2 Mungu humpa mwanadamu utajiri, mali na heshima, hivyo hakukosa chochote moyo wake unachokitamani. Lakini Mungu hamwezeshi kuvifurahia, badala yake mgeni ndiye anayevifurahia. Hili ni ubatili, ni ubaya unaosikitisha.
Človek, ki mu je Bog dal bogastva, premoženje in čast, tako da za svojo dušo ne potrebuje ničesar od vsega, kar si želi, pa mu vendar Bog ne daje moči, da od tega jé, temveč to jé tujec. To je ničevost in to je zla bolezen.
3 Mtu anaweza kuwa na watoto mia moja naye akaishi miaka mingi, lakini haidhuru kuwa ataishi muda mrefu kiasi gani, kama hawezi kufurahia mafanikio yake na kwamba hapati mazishi ya heshima, ninasema afadhali mtoto aliyezaliwa akiwa amekufa kuliko yeye.
Če človek zaplodi sto otrok in živi mnogo let, tako da je dni njegovih let mnogo in njegova duša ne bo nasičena z dobrinami in tudi da nima pogreba, pravim, da je prezgodaj rojeni boljši kakor on.
4 Kuzaliwa kwake hakuna maana, huondokea gizani na gizani jina lake hufunikwa.
Kajti vstopa z ničevostjo in odhaja v temi in njegovo ime bo prekrito s temo.
5 Ingawa hakuwahi kuliona jua wala kujua kitu chochote, yeye ana pumziko zaidi kuliko mtu huyo,
Poleg tega ni videl sonca niti ni poznal nobene stvari; ta ima več počitka kakor drugi.
6 Hata kama huyo mtu ataishi miaka elfu mara mbili na zaidi, lakini akashindwa kufurahia mafanikio yake, je, wote hawaendi sehemu moja?
Da, čeprav je bilo rečeno, da živi dvakrat tisoč let, vendar ni videl dobrega; mar ne gredo vsi na en kraj?
7 Juhudi zote za binadamu ni kwa ajili ya kinywa chake, hata hivyo hamu yake kamwe haitoshelezwi.
Vse človekovo delo je za njegova usta, pa vendar apetit ni potešen.
8 Mtu mwenye hekima ana faida gani zaidi ya mpumbavu? Mtu maskini anapata faida gani kwa kujua jinsi ya kujistahi mbele ya watu wengine?
Kajti kaj ima modri več kakor bedak? Kaj ima ubogi, da zna hoditi pred živečimi?
9 Ni bora kile ambacho jicho linakiona kuliko hamu isiyotoshelezwa. Hili nalo ni ubatili, ni kukimbiza upepo.
Boljši je pogled oči kakor tavanje poželenja. Tudi to je ničevost in draženje duha.
10 Lolote lililopo limekwisha kupewa jina, naye mwanadamu alivyo ameshajulikana; hakuna mtu awezaye kushindana na mwenye nguvu kuliko yeye.
To, kar je bilo, je že imenovano in je znano, da je to človek; niti se ne more pričkati s tistim, ki je mogočnejši kakor on.
11 Maneno yanavyokuwa mengi, ndivyo yanavyokosa maana, Je, hilo linamfaidia vipi yeyote?
Ker je tukaj mnogo stvari, ki povečujejo ničevost, kaj je človek boljši?
12 Kwa maana ni nani anayejua lililo jema kwa ajili ya maisha ya mwanadamu, katika siku chache na za ubatili anazopita kama kivuli? Ni nani awezaye kumwambia yatakayotokea chini ya jua baada ya yeye kuondoka?
Kajti kdo ve kaj je boljše za človeka v tem življenju, vse dni njegovega praznega življenja, ki jih preživlja kakor senca? Kajti kdo lahko človeku pove kaj bo za njim pod soncem?

< Mhubiri 6 >