< Mhubiri 3 >

1 Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:
For everything an appointed time and an time for every matter under the heavens.
2 wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa,
A time to bear a child and a time to die a time to plant and a time to pluck up [what] is planted.
3 wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga,
A time to kill and a time to heal a time to break down and a time to build.
4 wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,
A time to weep and a time to laugh a time to mourn and a time to dance.
5 wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia,
A time to throw away stones and a time to gather stones a time to embrace and a time to be far from embracing.
6 wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuweka na wakati wa kutupa,
A time to seek and a time to count as lost a time to keep and a time to throw away.
7 wakati wa kurarua na wakati wa kushona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza,
A time to tear and a time to sew a time to be silent and a time to speak.
8 wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
A time to love and a time to hate a time of warfare and a time of peace.
9 Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake?
What? [is] [the] profit of the worker in [that] which he [is] a laborer.
10 Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu.
I have seen the task which he has given God to [the] children of humankind to be busy with it.
11 Amefanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Pia ameiweka hiyo milele katika mioyo ya wanadamu, wala hawawezi kutambua kwa kina yale ambayo Mungu amefanya tangu mwanzo hadi mwisho.
Everything he has made beautiful in time its also perpetuity he has put in heart their because not which not he will find humankind the work which he has done God from beginning and to end.
12 Ninajua kwamba hakuna kitu bora kwa wanadamu kuliko kuwa na furaha na kutenda mema wakati wanapoishi.
I know that there not [is] good for them that except to rejoice and to do good in life his.
13 Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.
And also every person that he will eat and he will drink and he will see good in all toil his [is] a gift of God it.
14 Ninajua kwamba kila kitu anachokifanya Mungu kitadumu milele, hakuna kinachoweza kuongezwa au kupunguzwa. Mungu hufanya hivyo ili watu wamche yeye.
I know that all that he does God it it will be for ever to it not to add and from it not to take away and God he has acted that people will fear from to before him.
15 Chochote kilichopo kilishakuwepo, na kitakachokuwepo kimekwishakuwepo kabla; naye Mungu huyaita yale yaliyopita yarudi tena.
Whatever that is [has been] already it and [that] which [is] to be already it has been and God he will seek [what] was pursued.
16 Pia nikaona kitu kingine tena chini ya jua: Mahali pa kutolea hukumu, uovu ulikuwepo, mahali pa kupatia haki, uovu ulikuwepo.
And again I have seen under the sun [the] place of justice [was] there wickedness and [the] place of righteousness [was] there wickedness.
17 Nikafikiri moyoni mwangu, “Mungu atawaleta hukumuni wote wawili wenye haki na waovu, kwa maana kutakuwako na wakati kwa ajili ya kila jambo, wakati kwa ajili ya kila tendo.”
I said I in heart my the righteous and the wicked he will judge God for a time [is] for every matter and on every deed there.
18 Pia nikafikiri, “Kuhusu wanadamu, Mungu huwajaribu ili wajione kwamba wao ni kama wanyama.
I said I in heart my on cause of [the] children of humankind to test them God and to see that they [are] animal[s] they for themselves.
19 Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili.
For [the] fate of [the] children of humankind and [the] fate of animal[s] and fate one [belongs] to them like [the] death of this so [the] death of this and breath one [belongs] to all and [the] advantage of humankind [is] more than the animal[s] not for everything [is] futility.
20 Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.
Everything [is] going to place one everything it was from the dust and everything [is] returning to the dust.
21 Ni nani ajuaye kama roho ya mtu huenda juu na roho ya mnyama hushuka chini ardhini?”
Who? [is] knowing [the] spirit of [the] children of humankind that is going up it upwards and [the] spirit of the animal[s] that is going down it downwards to the earth.
22 Kwa hiyo nikaona kwamba hakuna kitu kilicho bora zaidi kwa mwanadamu kuliko kuifurahia kazi yake, kwa sababu hilo ndilo fungu lake. Kwa maana ni nani awezaye kumrudisha ili aje kuona kile kitakachotendeka baada yake?
And I saw that there not [is] good more than that he will be happy humankind in work his for that [is] portion his for who? will he bring him to look on whatever that will be after him.

< Mhubiri 3 >