< Mhubiri 12 >

1 Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku za taabu, wala haijakaribia miaka utakaposema, “Mimi sifurahii hiyo”:
Haue thou mynde on thi creatour in the daies of thi yongthe, bifore that the tyme of thi turment come, and the yeris of thi deth neiye, of whiche thou schalt seie, Tho plesen not me.
2 kabla jua na nuru, nao mwezi na nyota havijatiwa giza, kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
`Haue thou mynde on thi creatour, bifor that the sunne be derk, and the liyt, and sterrys, and the mone; and cloude turne ayen after reyn.
3 siku ile walinzi wa nyumba watakapotetemeka, nao watu wenye nguvu watakapojiinamisha, wakati wasagao watakapokoma kwa sababu ya uchache, nao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
Whanne the keperis of the hous schulen be mouyd, and strongeste men schulen tremble; and grynderis schulen be idel, whanne the noumbre schal be maad lesse, and seeris bi the hoolis schulen wexe derk;
4 wakati milango ya kuingia barabarani itakapofungwa na sauti ya kusaga kufifia; wakati watu wataamshwa kwa sauti ya ndege, lakini nyimbo zao zote zikififia;
and schulen close the doris in the street, in the lownesse of vois of a gryndere; and thei schulen rise at the vois of a brid, and alle the douytris of song schulen wexe deef.
5 wakati watu watakapoogopa kilichoinuka juu na hatari zitakazokuwepo barabarani; wakati mlozi utakapochanua maua na panzi kujikokota nawe usiwe na shauku ya kitu chochote. Ndipo mwanadamu aiendea nyumba yake ya milele nao waombolezaji wakizunguka barabarani.
And hiy thingis schulen drede, and schulen be aferd in the weie; an alemaunde tre schal floure, a locuste schal be maad fat, and capparis schal be distried; for a man schal go in to the hous of his euerlastyngnesse, and weileris schulen go aboute in the street.
6 Mkumbuke Muumba wako: kabla haijakatika kamba ya fedha, au bakuli la dhahabu halijavunjika; kabla mtungi kuvunjika kwenye chemchemi, au gurudumu kuvunjika kisimani,
Haue thou mynde on thi creatour, byfore that a siluerne roop be brokun, and a goldun lace renne ayen, and a watir pot be al to-brokun on the welle, and a wheele be brokun togidere on the cisterne;
7 nayo mavumbi kurudi ardhini yalikotoka, na roho kurudi kwa Mungu aliyeitoa.
and dust turne ayen in to his erthe, wherof it was, and the spirit turne ayen to God, that yaf it.
8 Mhubiri asema, “Ubatili! Ubatili! Kila kitu ni ubatili!”
The vanyte of vanytees, seide Ecclesiastes, the vanyte of vanytees, and alle thingis ben vanyte.
9 Mhubiri hakuwa tu na hekima, bali aliwagawia watu maarifa pia. Alitafakari na kutafiti na akaweka katika utaratibu mithali nyingi.
And whanne Ecclesiastes was moost wijs, he tauyte the puple, and he telde out the thingis whiche he dide,
10 Mhubiri alitafiti ili kupata maneno sahihi na kila alichoandika kilikuwa sawa na kweli.
and he souyte out wisdom, and made many parablis; he souyte profitable wordis, and he wroot moost riytful wordis, and ful of treuthe.
11 Maneno ya wenye hekima ni kama mchokoro, mithali zao zilizokusanywa pamoja ni kama misumari iliyogongomewa ikawa imara, yaliyotolewa na Mchungaji mmoja.
The wordis of wise men ben as prickis, and as nailis fastned deepe, whiche ben youun of o scheepherde bi the counsels of maistris.
12 Tena zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo, hakuna mwisho wa kutunga vitabu vingi, nako kusoma sana huuchosha mwili.
My sone, seke thou no more than these; noon ende is to make many bookis, and ofte thenkyng is turment of fleisch.
13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa: Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
Alle we here togydere the ende of spekyng. Drede thou God, and kepe hise heestis; `that is to seie, ech man.
14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au baya.
God schal brynge alle thingis in to dom, that ben don; for ech thing don bi errour, whether it be good, ether yuel.

< Mhubiri 12 >