< Mhubiri 12 >

1 Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku za taabu, wala haijakaribia miaka utakaposema, “Mimi sifurahii hiyo”:
While you are still young, keep thinking about [God], who created you. Do that before [you are old] and you experience many troubles, during the years when you say “I no [longer] enjoy being alive.”
2 kabla jua na nuru, nao mwezi na nyota havijatiwa giza, kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
[When you become old], the light from the sun and moon and stars will [seem] dim [to you], and [it will seem that the rain] clouds [always] return [quickly] after it rains.
3 siku ile walinzi wa nyumba watakapotetemeka, nao watu wenye nguvu watakapojiinamisha, wakati wasagao watakapokoma kwa sababu ya uchache, nao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
Then your [arms that you use to protect] [MET] your bodies will shake/tremble, and your [legs that support] [MET] your bodies will become weak. Many of your [teeth that you use to] grind/chew [your food] will fall out, and your [eyes that you use to] look out of windows will not see clearly.
4 wakati milango ya kuingia barabarani itakapofungwa na sauti ya kusaga kufifia; wakati watu wataamshwa kwa sauti ya ndege, lakini nyimbo zao zote zikififia;
Your [ears] [MET] will not hear the noise in the streets, and you will not be able to hear clearly the sound of people grinding grain with millstones. You will be awakened in the morning by hearing the birds singing/chirping, [but] you will not be able to hear well the songs that (the birds/people) sing.
5 wakati watu watakapoogopa kilichoinuka juu na hatari zitakazokuwepo barabarani; wakati mlozi utakapochanua maua na panzi kujikokota nawe usiwe na shauku ya kitu chochote. Ndipo mwanadamu aiendea nyumba yake ya milele nao waombolezaji wakizunguka barabarani.
You will be afraid to be in high places and afraid of dangers on the roads that you walk on. [Your hair] will become [white like] [MET] the flowers of almond trees. [When you try to walk], you will drag yourself along like [MET] grasshoppers, and you will no longer desire [to have sex]. Then you will [die and] go to your eternal home, and people who will mourn for you will be in the streets.
6 Mkumbuke Muumba wako: kabla haijakatika kamba ya fedha, au bakuli la dhahabu halijavunjika; kabla mtungi kuvunjika kwenye chemchemi, au gurudumu kuvunjika kisimani,
[Think much about God now, because] soon our lives will end, [like] [MET] silver chains or golden bowls that break easily, or like pitchers/jugs that are broken at the water fountain, or like broken pulleys at a well.
7 nayo mavumbi kurudi ardhini yalikotoka, na roho kurudi kwa Mungu aliyeitoa.
Then our corpses will [decay and] become dirt again, and our spirits will return to God, the one who gave us our spirits.
8 Mhubiri asema, “Ubatili! Ubatili! Kila kitu ni ubatili!”
[So] I say [again] that it is difficult to understand why everything happens; everything is mysterious.
9 Mhubiri hakuwa tu na hekima, bali aliwagawia watu maarifa pia. Alitafakari na kutafiti na akaweka katika utaratibu mithali nyingi.
I was considered to be a very wise man, and I taught the people many things. I assembled/collected and wrote down many proverbs, and I carefully thought about and studied them.
10 Mhubiri alitafiti ili kupata maneno sahihi na kila alichoandika kilikuwa sawa na kweli.
I searched for the right words, and what I have written is reliable and true.
11 Maneno ya wenye hekima ni kama mchokoro, mithali zao zilizokusanywa pamoja ni kama misumari iliyogongomewa ikawa imara, yaliyotolewa na Mchungaji mmoja.
The things that [I and other] wise people say [teach people what they should do]; they are like [SIM] (goads/sharp sticks that people use to strike animals to direct where they should go). They are like [SIM] nails that stick out of pieces of wood. They are given to us by [God, who is like] [MET] our shepherd.
12 Tena zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo, hakuna mwisho wa kutunga vitabu vingi, nako kusoma sana huuchosha mwili.
[So], my son, pay careful attention to what I have written, and choose carefully what you read that others have written, [because] writing proverbs/books is endless, and [trying to] study them all will cause you to become exhausted.
13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa: Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
[Now] you have heard all [that I have told you], and here is the conclusion: Revere God, and obey his commandments, because those commandments summarize everything that people should do.
14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au baya.
And do not forget that God will judge everything that we do, good things and bad things, [even] things that we do secretly.

< Mhubiri 12 >