< Mhubiri 11 >
1 Tupa mkate wako juu ya maji, kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.
Jette ton pain sur la face des eaux, car avec le temps tu le retrouveras.
2 Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
Fais-en part à sept, et même à huit; car tu ne sais pas quel mal peut venir sur la terre.
3 Kama mawingu yamejaa maji, hunyesha mvua juu ya nchi. Kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, mahali ulipoangukia, hapo ndipo utakapolala.
Quand les nuées sont pleines, elles répandent de la pluie sur la terre; et quand un arbre tombe, au midi, ou au nord, au lieu où l'arbre est tombé, il demeure.
4 Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.
Celui qui observe le vent, ne sèmera point; et celui qui regarde les nuées, ne moissonnera point.
5 Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
Comme tu ne sais pas quel est le chemin du vent, ni comment se forment les os dans le sein de celle qui est enceinte; de même tu ne connais pas l'œuvre de Dieu, qui a fait toutes choses.
6 Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
Sème ta semence dès le matin, et ne laisse pas reposer ta main le soir; car tu ne sais pas ce qui réussira, ceci ou cela, ou si les deux seront également bons.
7 Nuru ni tamu, tena inafurahisha macho kuona jua.
La lumière est douce, et il est agréable aux yeux de voir le soleil.
8 Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani, na aifurahie yote. Lakini na akumbuke siku za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.
Et si un homme vit un grand nombre d'années, qu'il se réjouisse pendant toutes ces années, et qu'il se souvienne des jours de ténèbres, qui sont nombreux. Tout ce qui vient est vanité.
9 Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana, moyo wako na ukupe furaha katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yaonayo, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
Jeune homme, réjouis-toi dans ton jeune âge, et que ton cœur te rende content aux jours de ta jeunesse; et marche comme ton cœur te mène, et selon le regard de tes yeux; mais sache que pour toutes ces choses Dieu te fera venir en jugement.
10 Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.
Bannis le chagrin de ton cœur, et éloigne les maux de ta chair; car le jeune âge et l'adolescence ne sont que vanité.