< Mhubiri 11 >

1 Tupa mkate wako juu ya maji, kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.
Jette ton pain sur la face des eaux, car après beaucoup de jours tu le retrouveras;
2 Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
donnes-en une part à sept, et même à huit: car tu ne sais pas quel malheur peut arriver sur la terre.
3 Kama mawingu yamejaa maji, hunyesha mvua juu ya nchi. Kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, mahali ulipoangukia, hapo ndipo utakapolala.
Quand les nuées sont remplies de pluie, elles se vident sur la terre; et si un arbre tombe au midi ou au nord, il reste à la place où il est tombé.
4 Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.
Celui qui observe le vent ne sèmera point, et celui qui interroge les nuages ne moissonnera point.
5 Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
Comme tu ne sais pas quel est le chemin du vent et comment se forment les os dans le sein de la mère, ainsi tu ne connais pas l'œuvre de Dieu, qui fait toutes choses.
6 Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
Dès le matin sème ta semence, et le soir ne laisse pas reposer ta main, car tu ne sais pas ce qui réussira, ceci ou cela, ou si l'un et l'autre ne sont pas également bons.
7 Nuru ni tamu, tena inafurahisha macho kuona jua.
La lumière est douce, et c'est un plaisir pour l'œil de voir le soleil.
8 Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani, na aifurahie yote. Lakini na akumbuke siku za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.
Même si l'homme vit de nombreuses années, qu'il se réjouisse pendant toutes ces années, et qu'il pense aux jours de ténèbres, car ils seront nombreux: tout ce qui arrive est vanité.
9 Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana, moyo wako na ukupe furaha katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yaonayo, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
Jeune homme, réjouis-toi dans ta jeunesse; que ton cœur te donne de la joie dans les jours de ta jeunesse! Marche dans les voies de ton cœur, et selon les regards de tes yeux; mais sache que pour tout cela Dieu te fera venir en jugement.
10 Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.
Bannis de ton cœur le chagrin, et éloigne le mal de ta chair; la jeunesse et l'adolescence sont vanité.

< Mhubiri 11 >