< Mhubiri 11 >
1 Tupa mkate wako juu ya maji, kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.
Send bread your on [the] surface of the waters for in [the] abundance of days you will find it.
2 Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
Give a portion to seven and also to eight for not you know what? will it be calamity on the earth.
3 Kama mawingu yamejaa maji, hunyesha mvua juu ya nchi. Kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, mahali ulipoangukia, hapo ndipo utakapolala.
If they will be filled the clouds rain on the earth they will pour [it] out and whether it falls a tree at the south and or at the north [the] place where it falls the tree there it will be.
4 Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.
[one who] watches for A wind not he will sow and [one who] looks on the clouds not he will reap.
5 Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
Just as not you [are] knowing what? [is] [the] way of the wind like bones in [the] womb of the full [woman] thus not you know [the] work of God who he makes everything.
6 Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
In the morning sow seed your and to the evening may not you give rest to hand your for not you [are] knowing where? this will it succeed ¿ this or? this and or? [will] both of them as one [be] good.
7 Nuru ni tamu, tena inafurahisha macho kuona jua.
And [is] sweet the light and [is] good for the eyes to see the sun.
8 Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani, na aifurahie yote. Lakini na akumbuke siku za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.
That except years [surely] a multitude will live person in all of them let him be take pleasure and he may remember [the] days of darkness for [surely] many will be all that has come [is] futility.
9 Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana, moyo wako na ukupe furaha katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yaonayo, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
Rejoice O young man in youth your and let it make good you heart your in [the] days of youth your and walk in [the] ways of heart your and in [the] sight of eyes your and know that on all these [things] he will bring you God in judgment.
10 Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.
And remove vexation from heart your and put away evil from flesh your for youth and the black hair [are] futility.