< Mhubiri 11 >

1 Tupa mkate wako juu ya maji, kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.
Cast thy bread upon the waters; for after many days thou shalt find it.
2 Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
Give a portion to seven, yea, to eight; for thou knowest not what evil shall be upon the earth.
3 Kama mawingu yamejaa maji, hunyesha mvua juu ya nchi. Kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, mahali ulipoangukia, hapo ndipo utakapolala.
When the clouds are full of rain, they empty upon the earth; and when a tree falleth to the south or the north, in the place where the tree falleth, there it shall be.
4 Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.
He that watcheth the wind will not sow, and he that gazeth upon the clouds will not reap.
5 Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
As thou knowest not the way of the wind, nor how the bones are formed in the womb of her that is with child, so thou canst not know the work of God, who doeth all things.
6 Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
In the morning sow thy seed, and in the evening withhold not thy hand! For thou knowest not whether this shall prosper, or that, or whether both of them shall be alike good.
7 Nuru ni tamu, tena inafurahisha macho kuona jua.
Truly the light is sweet, and a pleasant thing it is for the eyes to behold the sun.
8 Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani, na aifurahie yote. Lakini na akumbuke siku za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.
Yea, though a man live many years, let him rejoice in them all, and let him think of the days of darkness; for they shall be many. All that cometh is vanity.
9 Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana, moyo wako na ukupe furaha katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yaonayo, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
Rejoice, O young man, in thy youth, and let thy heart cheer thee in the days of thy youth, and walk in the ways of thy heart, and in the sight of thine eyes! but know thou, that for all these things God will bring thee into judgment.
10 Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.
Therefore remove sorrow from thy heart, and put away evil from thy body! for childhood and youth are vanity.

< Mhubiri 11 >