< Mhubiri 11 >
1 Tupa mkate wako juu ya maji, kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.
Send your bread out on the surface of the water, and many days later you will find it again.
2 Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
Share what you own with seven or eight people, for you never know what disaster could happen.
3 Kama mawingu yamejaa maji, hunyesha mvua juu ya nchi. Kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, mahali ulipoangukia, hapo ndipo utakapolala.
When the clouds are full they pour rain down upon the earth. Whether a tree falls to the north or to the south, it stays where it fell.
4 Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.
The farmer who pays attention to the direction of the wind knows when not to sow, and by watching the clouds knows when not to reap.
5 Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
Just as you don't know how the breath of life comes to the child in its mother's womb, so you can't understand the work of God, the Creator of everything.
6 Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
In the morning, sow your seed. In the evening, don't stop. For you have no way of knowing which crop will grow well—one may be profitable, or the other—or maybe both.
7 Nuru ni tamu, tena inafurahisha macho kuona jua.
How sweet it is to live in the light, to see the sun rise on another day.
8 Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani, na aifurahie yote. Lakini na akumbuke siku za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.
May you live for many years, and may you enjoy them all. But remember there will many days of darkness, and all that is to come is uncertain.
9 Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana, moyo wako na ukupe furaha katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yaonayo, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
Young people, enjoy your youth! Be happy with what's good! While you're young, let your mind guide your life, and do as you think best. But remember that God will judge you for all your thoughts and actions.
10 Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.
So don't let your mind worry, and avoid things that hurt your body. Even so, despite youth and enthusiasm, life is still so hard to understand!