< Mhubiri 10 >
1 Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
Las moscas muertas pueden hacer que el aceite perfumado huela mal. Del mismo modo, un poco de insensatez supera a la gran sabiduría y al honor.
2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
La mente del sabio elige el lado correcto, pero la mente del insensato va hacia la izquierda.
3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
Sólo la forma en que los necios andan por el camino demuestra que no tienen sentido común, dejando en claro a todos su estupidez.
4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
Si tu superior se enfada contigo, no te rindas y te vayas. Si mantienes la calma, incluso los errores graves pueden resolverse.
5 Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
También me di cuenta de que hay otro mal aquí en la tierra: los gobernantes cometen un gran error
6 Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
cuando ponen a los tontos en altos cargos, mientras que los que están ampliamente cualificados son puestos en posiciones bajas.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
He visto a esclavos montando a caballo, mientras los príncipes caminan por el suelo como esclavos.
8 Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
Si cavas un pozo, puedes caerte dentro. Si derribas un muro, te puede morder una serpiente.
9 Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
Si extraes piedra, puedes lesionarte. Si partes troncos, podrías herirte.
10 Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
Si tu hacha está desafilada y no la afilas, tienes que usar mucha más fuerza. Conclusión: ser sabio trae buenos resultados.
11 Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
Si la serpiente muerde al encantador de serpientes antes de ser encantada, ¡no hay beneficio para el encantador de serpientes!
12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
Las palabras sabias son beneficiosas, pero los necios se destruyen a sí mismos con lo que dicen.
13 Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
Los insensatos comienzan diciendo tonterías y terminan diciendo tonterías perversas.
14 naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
Los insensatos no paran de hablar, pero nadie sabe lo que va a pasar, así que ¿quién puede decir lo que depara el futuro?
15 Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
El trabajo hace que los insensatos se desgasten tanto que no pueden lograr nada.
16 Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
Estás en problemas si el rey de tu país es joven, y si tus líderes están ocupados festejando desde la mañana.
17 Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
Tienes suerte si tu rey viene de una familia noble, y si tus líderes festejan a la hora apropiada para darse energía, y no para emborracharse.
18 Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
La gente perezosa deja que sus techos se derrumben; la gente ociosa no repara sus casas con goteras.
19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
Una buena comida trae placer; el vino hace la vida agradable; el dinero cubre todas las necesidades.
20 Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.
No hables mal del rey, ni siquiera en tus pensamientos. No hables mal de los dirigentes, incluso en la intimidad de tu habitación. Un pájaro puede oír lo que dices y salir volando para contarles.