< Mhubiri 10 >

1 Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
Des mouches mortes infectent et corrompent l'huile du parfumeur; de même un peu de folie l'emporte sur la sagesse et la gloire.
2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
Le cœur du sage est à sa droite, et le cœur de l'insensé, à sa gauche.
3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
Et aussi, quand l'insensé va dans le chemin, le sens lui manque, et il montre à tous qu'il est fou.
4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
Si l'esprit du prince s'élève contre toi, ne quitte point ta place; car le calme prévient de grandes fautes.
5 Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
Il est un mal que j'ai vu sous le soleil, comme une erreur qui provient du souverain:
6 Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
la folie occupe les postes élevés, et des riches sont assis dans de basses conditions.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
J'ai vu des esclaves portés sur des chevaux, et des princes aller à pied comme des esclaves.
8 Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
Celui qui creuse une fosse peut y tomber, et celui qui renverse une muraille peut être mordu par un serpent.
9 Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
Celui qui détache des pierres peut être blessé, et celui qui fend du bois peut se faire mal.
10 Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
Si le fer est émoussé et si l'on n'a pas aiguisé le tranchant, on devra redoubler de force; mais la sagesse est préférable pour le succès.
11 Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
Si le serpent mord faute d'enchantement, il n'y a pas d'avantage pour l'enchanteur.
12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
Les paroles de la bouche du sage sont pleines de grâce; mais les lèvres de l'insensé le dévorent.
13 Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
Le commencement des paroles de sa bouche est sottise, et la fin de son discours est démence furieuse.
14 naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
Et l'insensé multiplie les paroles!... L'homme ne sait pas ce qui arrivera, et qui lui dira ce qui sera après lui?
15 Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
Le travail de l'insensé le fatigue, lui qui ne sait pas même aller à la ville.
16 Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
Malheur à toi, pays dont le roi est un enfant, et dont les princes mangent dès le matin!
17 Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
Heureux es-tu, pays dont le roi est fils de nobles, et dont les princes mangent au temps convenable, pour soutenir leurs forces, et non pour se livrer à la boisson.
18 Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
Quand les mains sont paresseuses, la charpente s'affaisse, et quand les mains sont lâches, la maison ruisselle.
19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
On fait des repas pour goûter le plaisir; le vin rend la vie joyeuse, et l'argent répond à tout.
20 Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.
Même dans ta pensée ne maudis pas le roi, même dans ta chambre à coucher ne maudis pas le puissant; car l'oiseau du ciel emporterait ta voix, et l'animal ailé publierait tes paroles.

< Mhubiri 10 >