< Mhubiri 10 >
1 Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
[A few] dead flies in [a bottle of] perfume cause [all] the perfume to stink. Similarly [SIM], a small amount of acting foolishly can have a greater effect than acting wisely.
2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
If people think sensibly, it will lead them to do what is right; if they think foolishly, it causes them to do what is wrong.
3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
Even while foolish people walk along the road, they show that they do not have good sense; they show everyone that they are not wise.
4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
Do not quit working for a ruler when he is angry with you; if you remain calm, he will [probably] stop being angry.
5 Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
There is something [else] that I have seen here on this earth, something that rulers sometimes do that is wrong/inappropriate:
6 Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
They appoint foolish people to have important positions, while they appoint rich [people] to have unimportant positions.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
They allow slaves [to ride] on horses [like rich people usually do], [but] they force officials to walk [like slaves usually do].
8 Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
[It is possible that] those who dig pits will fall into one of those pits. [It is possible that] someone who tears down a wall will be bitten by a snake [that is in that wall].
9 Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
If you work in a quarry, [it is possible that] a stone [will fall on you and] injure you. [It is possible that] men who split logs will be injured by one of those logs.
10 Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
If your axe is not sharp [DOU], you will need to work harder [to cut down a tree], but by being wise, you will succeed.
11 Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
If a snake bites a man before he charms/tames it, his ability to charm snakes will not benefit him.
12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
Wise people say [MTY] what is sensible, and because of that, people honor them; but foolish people are destroyed by what they say [MTY].
13 Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
When foolish people start to talk, they say things that are foolish, and they end by saying things that are both wicked and foolish.
14 naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
They talk (too much/without ceasing). None of us knows what will happen in the future, or what will happen after we die.
15 Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
Foolish people become [so] exhausted by the work that they do that they are unable to find the road to their town/homes.
16 Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
Terrible things will happen to the people of a nation whose ruler is a foolish young man, and whose [other] leaders continually eat, all day long, every day.
17 Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
[But] a nation will prosper if its ruler is from a (noble/well-educated) family, and if its [other] leaders feast [only] at the proper times, and [if they eat and drink only] to be strong, not to become drunk.
18 Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
Some men are very lazy [and do not repair the rafters], with the result that the rafters sag [and collapse]; and if they do not repair the roof, water will leak into the house [when it rains].
19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
Eating food and drinking wine causes us to laugh and be happy, [but] we are able to enjoy those things only if we have money [to buy them].
20 Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.
Do not even think about cursing the king, or cursing rich [people, even] when you are [alone] in your bedroom, because [it is possible that] a little bird will hear [what you are saying], [and] tell those people what you said [about them].