< Mhubiri 10 >
1 Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
Flies of death it causes to stink it ferments [the] oil of a perfumer [is] weighty more than wisdom more than honor folly a little.
2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
[the] heart of A wise [person] [is] to right [hand] his and [the] heart of a fool [is] to left [hand] his.
3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
And also on the way (like when a fool *Q(K)*) [is] going heart his is lacking and he says to everyone [is] a fool he.
4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
If [the] spirit of the ruler it will go up towards you place your may not you leave for calmness it will cause to rest sins great.
5 Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
There [is] an evil [which] I have seen under the sun like an inadvertence that [is] going forth from to before the ruler.
6 Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
It is put folly in high places many and rich [people] in the low place they sit.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
I have seen slaves on horses and princes [who] walk like slaves on the ground.
8 Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
[one who] digs A pit in it he will fall and [one who] breaks through a wall it will bite him a snake.
9 Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
[one who] quarries Stones he will be hurt by them [one who] cleaves wood he will be endangered by them.
10 Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
If it is blunt the iron [axe] and he not faces he has sharpened and strength he will make strong and [is] advantage (to give success *Q(k)*) wisdom.
11 Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
If it will bite the snake with not charming and there not [is] profit for [the] master of the tongue.
12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
[the] words of [the] mouth of A wise [person] [are] favor and [the] lips of a fool it swallows him.
13 Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
[the] beginning of [the] words of Mouth his [is] folly and [the] end of mouth his [is] madness evil.
14 naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
And the fool he multiplies words not he knows the person what? that will be and which it will be from after him who? will he tell to him.
15 Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
[the] toil of Fools it wearies him that not he knows to walk to a city.
16 Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
Woe! to you O land that king your [is] a youth and princes your in the morning they eat.
17 Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
How blessed [are] you O land that king your [is] a son of nobles and princes your at the appropriate time they eat for strength and not for drinking.
18 Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
In laziness it sinks the rafter[s] and in lowering of hands it leaks the house.
19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
For laughter [people are] making food and wine it makes glad life and money it answers everything.
20 Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.
Also in mind your a king may not you curse and in [the] chambers of lying down your may not you curse a rich [person] for bird of the heavens it will carry the sound and an owner (of wings *Q(K)*) it will tell [the] matter.