< Mhubiri 10 >

1 Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
Dead flies make the oil of the perfumer loathsome and corrupt; thus doth a little folly weigh down wisdom and honor.
2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
A wise man's mind is at his right hand; but a fool's mind is at his left.
3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
Yea, even when the fool walketh in the way, his understanding faileth him, and he saith to every one that he is a fool.
4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
If the anger of a ruler rise up against thee, leave not thy place! for gentleness pacifieth great offences.
5 Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
There is an evil which I have seen under the sun; an error which proceedeth from a ruler.
6 Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
Folly is set in many high stations, and the noble sit in a low place.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
I have seen servants upon horses, and princes walking as servants on foot.
8 Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
He that diggeth a pit shall fall into it; and whoso breaketh down a wall, a serpent shall bite him.
9 Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
Whoso removeth stones shall be hurt therewith, and he that cleaveth wood shall be endangered thereby.
10 Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
If the iron be blunt, and one do not whet the edge, then must he put forth more strength; but an advantage for giving success hath wisdom.
11 Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
If a serpent bite before he is charmed, then there is no advantage to the charmer.
12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
The words of a wise man's mouth are gracious; but the lips of a fool are his destruction.
13 Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
The beginning of the words of his mouth is folly, and the end of his talk is mischievous madness.
14 naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
A fool also multiplieth words, though no man knoweth what shall be; and who can tell him what shall be after him?
15 Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
The labor of the foolish man wearieth him, because he knoweth not how to go to the city.
16 Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
Woe to thee, O land, when thy king is a child, and thy princes feast in the morning!
17 Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
Happy thou, O land, when thy king is a noble, and thy princes eat in due season, for strength, and not for drunkenness!
18 Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
By much slothfulness the building decayeth; and by the slackness of the hands the house leaketh.
19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
A feast is made for laughter, and wine makes merry; but money answereth all things.
20 Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.
Curse not the king; no, not in thy thought; and curse not the rich in thy bed-chamber! for a bird of the air shall carry the voice; and that which hath wings shall tell the matter.

< Mhubiri 10 >