< Mhubiri 10 >

1 Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
Dead flies cause the oil of the perfumer to send forth an evil odor; so does a little folly outweigh wisdom and honor.
2 Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
A wise man's heart is at his right hand, but a fool's heart at his left.
3 Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
Yes also, when the fool walks by the way, his understanding fails him, and he says to everyone that he is a fool.
4 Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
If the spirit of the ruler rises up against you, do not leave your place; for gentleness lays great offenses to rest.
5 Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
There is an evil which I have seen under the sun, the sort of error which proceeds from the ruler.
6 Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
Folly is set in great dignity, and the rich sit in a low place.
7 Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
I have seen servants on horses, and princes walking like servants on the earth.
8 Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
He who digs a pit may fall into it; and whoever breaks through a wall may be bitten by a serpent.
9 Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
Whoever carves out stones may be injured by them. Whoever splits wood may be endangered thereby.
10 Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
If the axe is blunt, and one doesn't sharpen the edge, then he must use more strength; but skill brings success.
11 Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
If the serpent bites before it is charmed, then is there no profit for the charmer's tongue.
12 Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
The words of a wise man's mouth are gracious; but a fool is swallowed by his own lips.
13 Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
The beginning of the words of his mouth is foolishness; and the end of his talk is mischievous madness.
14 naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
A fool also multiplies words. Man doesn't know what will be; and that which will be after him, who can tell him?
15 Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
The labor of fools wearies every one of them; for he doesn't know how to go to the city.
16 Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
Woe to you, land, when your king is a child, and your princes eat in the morning.
17 Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
Blessed are you, land, when your king is the son of nobles, and your princes eat in due season, for strength, and not for drunkenness.
18 Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
By slothfulness the roof sinks in; and through idleness of the hands the house leaks.
19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
A feast is made for laughter, and wine makes the life glad; and money is the answer for all things.
20 Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.
Do not curse the king, no, not in your thoughts; and do not curse the rich in your bedchamber: for a bird of the sky may carry your voice, and that which has wings may tell the matter.

< Mhubiri 10 >