< Torati 1 >
1 Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
These bee the wordes which Moses spake vnto all Israel, on this side Iorden in the wildernesse, in the plaine, ouer against the red Sea, betweene Paran and Tophel, and Laban, and Hazeroth, and Di-zahab.
2 (Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
There are eleuen dayes iourney from Horeb vnto Kadesh-barnea, by the way of mout Seir.
3 Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
And it came to passe in the first day of the eleuenth moneth, in the fourtieth yeere that Moses spake vnto the children of Israel according vnto all that the Lord had giuen him in commandement vnto them,
4 Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
After that he had slaine Sihon the king of the Amorites which dwelt in Heshbon, and Og king of Bashan, which dwelt at Ashtaroth in Edrei.
5 Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
On this side Iorden in the lande of Moab began Moses to declare this lawe, saying,
6 Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
The Lord our God spake vnto vs in Horeb, saying, Ye haue dwelt long ynough in this mount,
7 Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
Turne you and depart, and goe vnto the mountaine of the Amorites, and vnto all places neere thereunto in the plaine, in the mountaine, or in the valley: both Southwarde, and to the Sea side, to the land of the Canaanites, and vnto Lebanon: euen vnto the great riuer, the riuer Perath.
8 Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
Beholde, I haue set the land before you: go in and possesse that land which the Lord sware vnto your fathers, Abraham, Izhak, and Iaakob, to giue vnto them and to their seede after them.
9 Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
And I spake vnto you the same time, saying, I am not able to beare you my selfe alone:
10 Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
The Lord your God hath multiplied you: and beholde, ye are this day as the starres of heauen in nomber:
11 Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
(The Lord God of your fathers make you a thousand times so many moe as ye are, and blesse you, as he hath promised you)
12 Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
Howe can I alone beare your combrance and your charge, and your strife?
13 Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
Bring you men of wisedome and of vnderstanding, and knowen among your tribes, and I will make them rulers ouer you:
14 Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
Then ye answered me and said, The thing is good that thou hast commanded vs to doe.
15 Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
So I tooke the chiefe of your tribes wise and knowen men, and made them rulers ouer you, captaines ouer thousands, and captaines ouer hundreds, and captaines ouer fiftie, and captaines ouer tenne, and officers among your tribes.
16 Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
And I charged your iudges that same time, saying, Heare the controuersies betweene your brethren, and iudge righteously betweene euery man and his brother, and the stranger that is with him.
17 Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
Ye shall haue no respect of person in iudgement, but shall heare the small aswell as the great: yee shall not feare the face of man: for the iudgement is Gods: and the cause that is too hard for you, bring vnto me, and I will heare it.
18 Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
Also I commanded you the same time all the things which ye should doe.
19 Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
Then we departed from Horeb, and went through all that great and terrible wildernesse (as yee haue seene) by the way of the mountaine of the Amorites, as the Lord our God commanded vs: and we came to Kadesh-barnea.
20 Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
And I saide vnto you, Yee are come vnto the mountaine of the Amorites, which the Lord our God doeth giue vnto vs.
21 Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
Beholde, the Lord thy God hath layde the land before thee: go vp and possesse it, as the Lord the God of thy fathers hath saide vnto thee: feare not, neither be discouraged.
22 Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
Then ye came vnto me euery one, and said, We wil send men before vs, to search vs out the land and to bring vs word againe, what way we must go vp by, and vnto what cities we shall come.
23 Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
So the saying pleased me well, and I tooke twelue men of you, of euery tribe one.
24 Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
Who departed, and went vp into the mountaine, and came vnto the riuer Eshcol, and searched out the land.
25 Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
And tooke of the fruite of the land in their hands, and brought it vnto vs, and brought vs worde againe, and sayd, It is a good land, which the Lord our God doeth giue vs.
26 Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
Notwithstanding, ye would not go vp, but were disobedient vnto the commandement of the Lord your God,
27 Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
And murmured in your tentes, and sayd, Because the Lord hated vs, therefore hath hee brought vs out of the land of Egypt, to deliuer vs into the hand of the Amorites, and to destroy vs.
28 Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
Whither shall we go vp? our brethren haue discouraged our hearts, saying, The people is greater, and taller then we: the cities are great and walled vp to heauen: and moreouer we haue seene the sonnes of the Anakims there.
29 Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
But I sayd vnto you, Dread not, nor be afrayd of them.
30 Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
The Lord your God, who goeth before you, he shall fight for you, according to all that he did vnto you in Egypt before your eyes,
31 na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
And in the wildernesse, where thou hast seene how the Lord thy God bare thee, as a man doeth beare his sonne, in all the way which ye haue gone, vntill ye came vnto this place.
32 Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
Yet for all this ye did not beleeue the Lord your God,
33 ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
Who went in the way before you, to search you out a place to pitch your tentes in, in fire by night, that ye might see what way to goe, and in a cloude by day.
34 Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
Then the Lord heard the voyce of your wordes, and was wroth, and sware, saying,
35 “Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
Surely there shall not one of these men of this froward generation, see that good land, which I sware to giue vnto your fathers,
36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
Saue Caleb the sonne of Iephunneh: he shall see it, and to him will I giue the land that he hath troden vpon, and to his children, because he hath constantly followed the Lord.
37 Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
Also the Lord was angry with me for your sakes, saying, Thou also shalt not goe in thither,
38 Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
But Ioshua the sonne of Nun which standeth before thee, he shall go in thither: incourage him: for he shall cause Israel to inherite it.
39 Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
Moreouer, your children, which ye sayd should be a praye, and your sonnes, which in that day had no knowledge betweene good and euill, they shall go in thither, and vnto them wil I giue it, and they shall possesse it.
40 Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
But as for you, turne backe, and take your iourney into the wildernesse by the way of the red Sea.
41 Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
Then ye answered and sayd vnto me, We haue sinned against the Lord, we wil go vp, and fight, according to all that the Lord our God hath commanded vs: and ye armed you euery man to the warre, and were ready to goe vp into the mountaine.
42 Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
But the Lord said vnto me, Say vnto them, Goe not vp, neither fight, (for I am not among you) least ye fall before your enemies.
43 Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
And when I told you, ye would not heare, but rebelled against the commandement of the Lord, and were presumptuous, and went vp into the mountaine.
44 Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
Then the Amorites which dwelt in that mountaine came out against you, and chased you (as bees vse to doe) and destroied you in Seir, euen vnto Hormah.
45 Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
And when ye came againe, ye wept before the Lord, but the Lord would not heare your voyce, nor incline his eares vnto you.
46 Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.
So ye abode in Kadesh a long time, according to the time that ye had remained before.