< Torati 9 >
1 Sikiliza, ee Israeli. Sasa mnakaribia kuvuka Yordani mwingie na kuwafukuza mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi pamoja na miji mikubwa yenye kuta zilizofika juu angani.
Sh'ma ·Hear obey·, Israel [God prevails]! You are to pass over the Jordan [Descender] today, to go in to dispossess nations greater and mightier than yourself, cities great and fortified up to the sky,
2 Watu ni wenye nguvu na warefu, ni wana wa Waanaki! Mnafahamu habari zao na mmesikia inavyosemekana: “Ni nani awezaye kusimama dhidi ya Waanaki?”
a people great and tall, the sons of the Anakim, whom you know, and of whom you have sh'ma ·heard obeyed· it said, “Who can stand before the sons of Anak?”
3 Kuweni na hakika leo kwamba Bwana Mungu wenu ndiye atakayetangulia kuvuka mbele yenu kama moto uteketezao. Atawaangamiza; atawatiisha mbele yenu. Nanyi mtawafukuza na kuwaangamiza mara moja, kama Bwana alivyowaahidi.
Know therefore today, that Adonai your God is he who goes over before you as a devouring fire. He will destroy them, and he will bring them down before you. So you shall drive them out, and make them perish quickly, as Adonai has spoken to you.
4 Baada ya Bwana Mungu wenu kuwafukuza mbele yenu, msiseme mioyoni mwenu, “Bwana ametuleta hapa kuimiliki nchi hii kwa sababu ya haki yetu.” La, ni kwa sababu ya uovu wa mataifa haya ndiyo Bwana anawafukuza mbele yenu.
Don’t say in your heart, after Adonai your God has thrust them out from before you, saying, “For my righteousness Adonai has brought me in to possess this land;” because Adonai drives them out before you because of the wickedness of these nations.
5 Si kwa sababu ya haki yenu wala uadilifu wenu kwamba mtaimiliki nchi yao; lakini kwa sababu ya uovu wa mataifa haya, Bwana Mungu wenu atawafukuza mbele yenu, ili kutimiza lile alilowaapia baba zenu Abrahamu, Isaki na Yakobo.
Not for your righteousness, or for the uprightness of your heart, do you go in to possess their land; but for the wickedness of these nations Adonai your God does drive them out from before you, and that he may establish the word which Adonai swore to your fathers, to Abraham [Father of a multitude], to Isaac [Laughter], and to Jacob [Supplanter].
6 Basi mjue, si kwa sababu ya haki yenu Bwana Mungu wenu anawapa nchi hii nzuri kuimiliki, kwa kuwa ninyi ni taifa lenye shingo ngumu.
Know therefore, that Adonai your God does not give you this good land to possess for your righteousness; for you are a stiff-necked people.
7 Kumbukeni hili, kamwe msisahau jinsi mlivyomkasirisha Bwana Mungu wenu kwa hasira huko jangwani. Tangu siku mlipotoka Misri mpaka mlipofika hapa, mmekuwa waasi dhidi ya Bwana.
Remember, and don’t forget, how you provoked Adonai your God to wrath in the wilderness. From the day that you left the land of Egypt [Abode of slavery], until you came to this place, you have been rebellious against Adonai.
8 Kule Horebu mliamsha ghadhabu ya Bwana, kwa hiyo alikasirika vya kutosha hata akataka kuwaangamiza.
Also in Horeb [Desert] you provoked Adonai to wrath, and Adonai was angry with you to destroy you.
9 Nilipopanda mlimani kupokea mbao za mawe, mbao za Agano lile Bwana alilofanya nanyi, nilikaa mlimani siku arobaini usiku na mchana, sikula mkate wala sikunywa maji.
When I had gone up onto the mountain to receive the stone tablets, even the tablets of the covenant which Adonai made with you, then I stayed on the mountain forty days and forty nights. I neither ate bread nor drank water.
10 Bwana alinipa mbao mbili za mawe zilizoandikwa kwa kidole cha Mungu. Juu ya mbao hizo kulikuwepo amri zote ambazo Bwana aliwatangazia kule mlimani kwa njia ya moto, siku ya kusanyiko.
Adonai delivered to me the two stone tablets written with God’s finger. On them were all the words which Adonai spoke with you on the mountain out of the middle of the fire in the day of the assembly.
11 Mwisho wa siku arobaini usiku na mchana, Bwana alinipa mbao mbili za mawe, mbao za Agano.
It came to pass at the end of forty days and forty nights, that Adonai gave me the two stone tablets, even the tablets of the covenant.
12 Kisha Bwana akaniambia, “Shuka chini mara moja, kwa sababu watu wako ambao umewatoa katika nchi ya Misri wamepotoka. Wamegeukia mbali haraka kutoka lile nililowaagiza, wamejitengenezea sanamu ya kusubu.”
Adonai said to me, “Arise, get down quickly from here; for your people whom you have brought out of Egypt [Abode of slavery] have corrupted themselves. They have quickly turned aside out of the way which I enjoined them. They have made a molten image for themselves!”
13 Naye Bwana akaniambia, “Nimewaona watu hawa nao ni watu wenye shingo ngumu sana!
Furthermore Adonai spoke to me, saying, “I have seen this people, and behold, it is a stiff-necked people.
14 Niache, ili nipate kuwaangamiza na kufuta jina lao kutoka chini ya mbingu. Nami nitakufanya kuwa taifa lenye nguvu zaidi na kuwa wengi kuliko wao.”
Leave me alone, that I may destroy them, and blot out their name from under the sky; and I will make of you a nation mightier and greater than they.”
15 Kwa hiyo niligeuka na kuteremka kutoka mlimani kwani mlima ulikuwa ukiwaka moto. Pia vibao vile viwili vya Agano vilikuwa mikononi mwangu.
So I turned and came down from the mountain, and the mountain was burning with fire. The two tablets of the covenant were in my two hands.
16 Nilipotazama, niliona kuwa mmefanya dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu; mmejifanyia sanamu ya kusubu katika umbo la ndama. Mmegeuka upesi kutoka njia ile Bwana aliyowaagiza.
I looked, and behold, you had sinned ·deviated (from the standard goal)· against Adonai your God. You had made yourselves a molten calf. You had turned aside quickly out of the way which Adonai had enjoined you.
17 Kwa hiyo nilichukua vibao vile viwili nikavitupa na kuvipasua vipande vipande mbele ya macho yenu.
I took hold of the two tablets, and threw them out of my two hands, and broke them before your eyes.
18 Ndipo tena nikasujudu mbele za Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana. Sikula mkate wala sikunywa maji, kwa sababu ya dhambi yote mliyoifanya, mkifanya lile lililo ovu mbele za Bwana na kumkasirisha.
I fell down before Adonai, as at the first, forty days and forty nights. I neither ate bread nor drank water, because of all your habitual sins ·missing the marks· which you sinned ·deviated (from the standard goal)·, in doing that which was evil in Adonai’s sight, to provoke him to anger.
19 Niliogopa hasira na ghadhabu ya Bwana, kwa kuwa aliwakasirikia vya kutosha na kutaka kuwaangamiza. Lakini Bwana alinisikiliza tena.
I was terrified that because of how angry Adonai was at you, of how heatedly displeased he was, that he would destroy you. But Adonai sh'ma ·heard obeyed· me that time too.
20 Bali yeye alimkasirikia Aroni kiasi cha kutaka kumwangamiza, nami wakati huo nilimwombea Aroni pia.
Adonai was angry enough with Aaron [Light-bringer] to destroy him. I prayed for Aaron [Light-bringer] also at the same time.
21 Kisha nikachukua ile sanamu ya ndama mliyoitengeneza na kuichoma kwenye moto. Nikaiponda na kuisaga ikawa unga laini kama vumbi, nikatupa lile vumbi kwenye kijito kilichotiririka toka mlimani.
I took your habitual sin ·missing the mark·, the calf which you had made, and burned it with fire, and crushed it, grinding it very small, until it was as fine as dust. I threw its dust into the brook that descended out of the mountain.
22 Pia mlimkasirisha Bwana huko Tabera, Masa na Kibroth-Hataava.
At Taberah, and at Massah [Testing], and at Kibroth Hattaavah, you provoked Adonai to wrath.
23 Vilevile wakati Bwana alipowatuma kutoka Kadesh-Barnea, alisema, “Kweeni, mkaimiliki nchi ambayo nimewapa.” Lakini mliasi dhidi ya agizo la Bwana Mungu wenu. Hamkumtegemea wala kumtii.
When Adonai sent you from Kadesh Barnea [Consecrated Son-inconstant], saying, “Go up and possess the land which I have given you,” you rebelled against the order of Adonai your God, and you didn’t trust him, nor sh'ma ·hear obey· his voice.
24 Mmekuwa waasi dhidi ya Bwana tangu nilipowajua ninyi.
You have been rebellious against Adonai from the day that I knew you.
25 Nilianguka kifudifudi mbele za Bwana kwa zile siku arobaini usiku na mchana kwa sababu Bwana alikuwa amesema angewaangamiza ninyi.
So I fell down before Adonai the forty days and forty nights that I fell down, because Adonai had said he would destroy you.
26 Nilimwomba Bwana na kusema, “Ee Bwana Mwenyezi, usiangamize watu wako, urithi wako mwenyewe ule ulioukomboa kwa uweza wako mkuu na kuwatoa katika nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu.
I prayed to Adonai, and said, “'Adonay Adonai [Lord Yahweh], don’t destroy your people and your inheritance, that you have redeemed through your greatness, that you have brought out of Egypt [Abode of slavery] with a mighty hand.
27 Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaki na Yakobo. Usiangalie ukaidi wa watu hawa, uovu wao wala dhambi yao.
Remember your servants, Abraham [Father of a multitude], Isaac [Laughter], and Jacob [Supplanter]. Don’t look at the stubbornness of this people, nor at their ethical wickedness, nor at their habitual sin ·missing the mark·,
28 Watu wa nchi ile uliyotutoa sisi wasije wakasema, ‘Ni kwa sababu Bwana hakuweza kuwachukua mpaka nchi aliyokuwa amewaahidia, kwa sababu aliwachukia, akawaleta ili aje kuwaua jangwani.’
lest the land you brought us out from say, ‘Because Adonai was not able to bring them into the land which he promised to them, and because he hated them, he has brought them out to kill them in the wilderness.’
29 Bali wao ni watu wako, urithi wako ule ulioutoa Misri kwa uweza wako mkuu na kwa mkono wako ulionyooka.”
Yet they are your people and your inheritance, which you brought out by your great power and by your outstretched arm.”