< Torati 9 >

1 Sikiliza, ee Israeli. Sasa mnakaribia kuvuka Yordani mwingie na kuwafukuza mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi pamoja na miji mikubwa yenye kuta zilizofika juu angani.
Hear, O Israel: Thou are to pass over the Jordan this day, to go in to dispossess nations greater and mightier than thyself, cities great and fortified up to heaven,
2 Watu ni wenye nguvu na warefu, ni wana wa Waanaki! Mnafahamu habari zao na mmesikia inavyosemekana: “Ni nani awezaye kusimama dhidi ya Waanaki?”
a people great and tall, the sons of the Anakim, whom thou know, and of whom thou have heard say, Who can stand before the sons of Anak?
3 Kuweni na hakika leo kwamba Bwana Mungu wenu ndiye atakayetangulia kuvuka mbele yenu kama moto uteketezao. Atawaangamiza; atawatiisha mbele yenu. Nanyi mtawafukuza na kuwaangamiza mara moja, kama Bwana alivyowaahidi.
Know therefore this day, that Jehovah thy God is he who goes over before thee as a devouring fire. He will destroy them, and he will bring them down before thee. So thou shall drive them out, and make them to perish quickly, as Jehovah has spoken to thee.
4 Baada ya Bwana Mungu wenu kuwafukuza mbele yenu, msiseme mioyoni mwenu, “Bwana ametuleta hapa kuimiliki nchi hii kwa sababu ya haki yetu.” La, ni kwa sababu ya uovu wa mataifa haya ndiyo Bwana anawafukuza mbele yenu.
Do not speak thou in thy heart, after Jehovah thy God has thrust them out from before thee, saying, For my righteousness Jehovah has brought me in to possess this land. Whereas for the wickedness of these nations Jehovah drives them out from before thee.
5 Si kwa sababu ya haki yenu wala uadilifu wenu kwamba mtaimiliki nchi yao; lakini kwa sababu ya uovu wa mataifa haya, Bwana Mungu wenu atawafukuza mbele yenu, ili kutimiza lile alilowaapia baba zenu Abrahamu, Isaki na Yakobo.
Not for thy righteousness, or for the uprightness of thy heart, do thou go in to possess their land, but for the wickedness of these nations Jehovah thy God drives them out from before thee, and that he may establish the word which Jehovah swore to thy fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob.
6 Basi mjue, si kwa sababu ya haki yenu Bwana Mungu wenu anawapa nchi hii nzuri kuimiliki, kwa kuwa ninyi ni taifa lenye shingo ngumu.
Know therefore, that Jehovah thy God does not give thee this good land to possess it for thy righteousness, for thou are a stiff-necked people.
7 Kumbukeni hili, kamwe msisahau jinsi mlivyomkasirisha Bwana Mungu wenu kwa hasira huko jangwani. Tangu siku mlipotoka Misri mpaka mlipofika hapa, mmekuwa waasi dhidi ya Bwana.
Remember, do not thou forget how thou provoked Jehovah thy God to wrath in the wilderness. From the day that thou went forth out of the land of Egypt, until ye came to this place, ye have been rebellious against Jehovah.
8 Kule Horebu mliamsha ghadhabu ya Bwana, kwa hiyo alikasirika vya kutosha hata akataka kuwaangamiza.
Also in Horeb ye provoked Jehovah to wrath, and Jehovah was angry with you to destroy you.
9 Nilipopanda mlimani kupokea mbao za mawe, mbao za Agano lile Bwana alilofanya nanyi, nilikaa mlimani siku arobaini usiku na mchana, sikula mkate wala sikunywa maji.
When I was gone up onto the mount to receive the tablets of stone, even the tablets of the covenant which Jehovah made with you, then I abode on the mount forty days and forty nights. I neither ate bread nor drank water.
10 Bwana alinipa mbao mbili za mawe zilizoandikwa kwa kidole cha Mungu. Juu ya mbao hizo kulikuwepo amri zote ambazo Bwana aliwatangazia kule mlimani kwa njia ya moto, siku ya kusanyiko.
And Jehovah delivered to me the two tablets of stone written with the finger of God. And on them was according to all the words, which Jehovah spoke with you in the mount out of the midst of the fire in the day of the assembly.
11 Mwisho wa siku arobaini usiku na mchana, Bwana alinipa mbao mbili za mawe, mbao za Agano.
And it came to pass, at the end of forty days and forty nights, that Jehovah gave me the two tablets of stone, even the tablets of the covenant.
12 Kisha Bwana akaniambia, “Shuka chini mara moja, kwa sababu watu wako ambao umewatoa katika nchi ya Misri wamepotoka. Wamegeukia mbali haraka kutoka lile nililowaagiza, wamejitengenezea sanamu ya kusubu.”
And Jehovah said to me, Arise, get thee down quickly from here, for thy people that thou have brought forth out of Egypt have corrupted themselves. They have quickly turned aside out of the way which I commanded them. They have made them a molten image.
13 Naye Bwana akaniambia, “Nimewaona watu hawa nao ni watu wenye shingo ngumu sana!
Furthermore Jehovah spoke to me, saying, I have seen this people, and, behold, it is a stiff-necked people.
14 Niache, ili nipate kuwaangamiza na kufuta jina lao kutoka chini ya mbingu. Nami nitakufanya kuwa taifa lenye nguvu zaidi na kuwa wengi kuliko wao.”
Let me alone, that I may destroy them, and blot out their name from under heaven, and I will make of thee a nation mightier and greater than they.
15 Kwa hiyo niligeuka na kuteremka kutoka mlimani kwani mlima ulikuwa ukiwaka moto. Pia vibao vile viwili vya Agano vilikuwa mikononi mwangu.
So I turned and came down from the mount, and the mount was burning with fire. And the two tablets of the covenant were in my two hands.
16 Nilipotazama, niliona kuwa mmefanya dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu; mmejifanyia sanamu ya kusubu katika umbo la ndama. Mmegeuka upesi kutoka njia ile Bwana aliyowaagiza.
And I looked, and, behold, ye had sinned against Jehovah your God. Ye had made you a molten calf. Ye had turned aside quickly out of the way which Jehovah had commanded you.
17 Kwa hiyo nilichukua vibao vile viwili nikavitupa na kuvipasua vipande vipande mbele ya macho yenu.
And I took hold of the two tablets, and cast them out of my two hands, and broke them before your eyes.
18 Ndipo tena nikasujudu mbele za Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana. Sikula mkate wala sikunywa maji, kwa sababu ya dhambi yote mliyoifanya, mkifanya lile lililo ovu mbele za Bwana na kumkasirisha.
And I fell down before Jehovah, as at the first, forty days and forty nights. I neither ate bread nor drank water, because of all your sin which ye sinned, in doing that which was evil in the sight of Jehovah, to provoke him to anger.
19 Niliogopa hasira na ghadhabu ya Bwana, kwa kuwa aliwakasirikia vya kutosha na kutaka kuwaangamiza. Lakini Bwana alinisikiliza tena.
For I was afraid of the anger and hot displeasure with which Jehovah was angry against you to destroy you. But Jehovah hearkened to me that time also.
20 Bali yeye alimkasirikia Aroni kiasi cha kutaka kumwangamiza, nami wakati huo nilimwombea Aroni pia.
And Jehovah was very angry with Aaron to destroy him. And I prayed for Aaron also at the same time.
21 Kisha nikachukua ile sanamu ya ndama mliyoitengeneza na kuichoma kwenye moto. Nikaiponda na kuisaga ikawa unga laini kama vumbi, nikatupa lile vumbi kwenye kijito kilichotiririka toka mlimani.
And I took your sin, the calf which ye had made, and burnt it with fire, and stamped it, grinding it very small, until it was as fine as dust. And I cast the dust of it into the brook that descended out of the mount.
22 Pia mlimkasirisha Bwana huko Tabera, Masa na Kibroth-Hataava.
And at Taberah, and at Massah, and at Kibroth-hattaavah, ye provoked Jehovah to wrath.
23 Vilevile wakati Bwana alipowatuma kutoka Kadesh-Barnea, alisema, “Kweeni, mkaimiliki nchi ambayo nimewapa.” Lakini mliasi dhidi ya agizo la Bwana Mungu wenu. Hamkumtegemea wala kumtii.
And when Jehovah sent you from Kadesh-barnea, saying, Go up and possess the land which I have given you, then ye rebelled against the commandment of Jehovah your God, and ye did not believe him, nor hearken to his voice.
24 Mmekuwa waasi dhidi ya Bwana tangu nilipowajua ninyi.
Ye have been rebellious against Jehovah from the day that I knew you.
25 Nilianguka kifudifudi mbele za Bwana kwa zile siku arobaini usiku na mchana kwa sababu Bwana alikuwa amesema angewaangamiza ninyi.
So I fell down before Jehovah the forty days and forty nights that I fell down, because Jehovah had said he would destroy you.
26 Nilimwomba Bwana na kusema, “Ee Bwana Mwenyezi, usiangamize watu wako, urithi wako mwenyewe ule ulioukomboa kwa uweza wako mkuu na kuwatoa katika nchi ya Misri kwa mkono wenye nguvu.
And I prayed to Jehovah, and said, O lord Jehovah, destroy not thy people and thine inheritance, that thou have redeemed through thy greatness, that thou have brought forth out of Egypt with a mighty hand.
27 Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaki na Yakobo. Usiangalie ukaidi wa watu hawa, uovu wao wala dhambi yao.
Remember thy servants, Abraham, Isaac, and Jacob. Look not to the stubbornness of this people, nor to their profaneness, nor to their sin,
28 Watu wa nchi ile uliyotutoa sisi wasije wakasema, ‘Ni kwa sababu Bwana hakuweza kuwachukua mpaka nchi aliyokuwa amewaahidia, kwa sababu aliwachukia, akawaleta ili aje kuwaua jangwani.’
lest the land from where thou brought us out say, Because Jehovah was not able to bring them into the land which he promised to them, and because he hated them, he has brought them out to kill them in the wilderness.
29 Bali wao ni watu wako, urithi wako ule ulioutoa Misri kwa uweza wako mkuu na kwa mkono wako ulionyooka.”
Yet they are thy people and thine inheritance, which thou brought out by thy great power and by thine outstretched arm.

< Torati 9 >