< Torati 8 >

1 Uwe mwangalifu kufuata kila agizo ninalokupa wewe leo, ili mweze kuishi, kuongezeka na mweze kuingia mkamiliki nchi ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zenu.
Prends bien garde de pratiquer tous les préceptes, que moi, je te prescris aujourd’hui, afin que vous puissiez vivre, que vous vous multipliiez, et, qu’après y être entrés, vous possédiez la terre au sujet de laquelle le Seigneur a juré à vos pères.
2 Kumbuka jinsi Bwana Mungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la.
Et tu te souviendras de tout le chemin par lequel le Seigneur ton Dieu t’a conduit pendant quarante ans à travers le désert, pour t’affliger, t’éprouver et faire connaître ce qui se passait dans ton cœur: si tu garderais ses commandements, ou non.
3 Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Bwana.
Il t’a affligé par la faim, et il t’a donné pour nourriture la manne que tu ignorais, toi, et tes pères, afin de te montrer que ce n’est pas de pain seulement que l’homme vit, mais de toute parole qui sort de la bouche de Dieu.
4 Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini.
Ton vêtement dont tu étais couvert, n’a pas manqué par la vétusté, et ton pied n’a pas été déchiré en dessous, et voici la quarantième année.
5 Mjue basi ndani ya mioyo yenu kama mtu anavyomwadibisha mwanawe, ndivyo Bwana Mungu wako atawaadibisha ninyi.
C’est afin que tu penses en ton cœur, que comme un homme instruit son fils, ainsi le Seigneur ton Dieu t’a instruit;
6 Shikeni maagizo ya Bwana Mungu wenu mtembee katika njia zake na kumheshimu.
Afin que tu gardes les commandements du Seigneur ton Dieu, que tu marches dans ses voies, et que tu le craignes.
7 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi yenye vijito na mabwawa ya maji, yenye chemchemi zinazotiririka mabondeni na katika vilima;
Car le Seigneur ton Dieu t’introduira dans une terre bonne, terre de ruisseaux, d’eaux, et de fontaines, dans les champs et les montagnes de laquelle jaillissent des sources de fleuves.
8 nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu na mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni na asali;
Terre de blé, d’orge et de vignes, dans laquelle naissent les figuiers, les grenadiers et les oliviers; terre d’huile et de miel.
9 nchi ambayo chakula hakitapungua na hamtakosa chochote; nchi ambayo miamba yake ni chuma na mnaweza kuchimba shaba kutoka kwenye vilima.
Où tu mangeras ton pain sans en manquer jamais, où tu jouiras de l’abondance de toutes choses, dont les pierres sont du fer; et de ses montagnes on exploite des mines d’airain;
10 Wakati mtakapokwisha kula na kushiba, msifuni Bwana Mungu wenu kwa ajili ya nchi nzuri aliyowapa.
Afin que, lorsque tu auras mangé, et que tu te seras rassasié, tu bénisses le Seigneur ton Dieu pour la terre excellente qu’il t’a donnée.
11 Jihadharini msimsahau Bwana Mungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo.
Aie soin, et prends garde de n’oublier jamais le Seigneur ton Dieu, et de ne point négliger ses préceptes, ses ordonnances et ses cérémonies, que moi, je te prescris aujourd’hui;
12 Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo,
De peur qu’après que tu auras mangé, et que tu seras rassasié, que tu auras bâti de belles maisons, et que tu t’y seras établi,
13 na wakati makundi yenu ya ngʼombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa,
Et que tu auras eu des troupeaux de bœufs, et des troupeaux de brebis, et une abondance d’argent et d’or de toutes choses,
14 basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahau Bwana Mungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
Ton cœur ne s’élève, et que tu ne te souviennes plus du Seigneur ton Dieu, qui t’a retiré de la terre d’Egypte, de la maison de servitude;
15 Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu.
Qui a été ton guide dans le désert grand et terrible, dans lequel étaient des serpents au souffle brûlant, des scorpions et des dipsas, et où il n’y avait absolument aucune eau; qui a fait jaillir des ruisseaux de la pierre la plus dure,
16 Aliwapa mana ya kula jangwani, kitu ambacho baba zenu hawakukijua, ili kuwanyenyekesha na kuwajaribu ninyi ili mwishoni apate kuwatendea mema.
Et qui t’a nourri dans le désert d’une manne que n’ont pas connue tes pères. Et après qu’il t’a eu affligé et éprouvé, il a eu enfin pitié de toi,
17 Mnaweza kusema, “Uwezo wangu na nguvu za mikono yangu ndizo zilizonipatia utajiri huu.”
Afin que tu ne dises pas en ton cœur: C’est ma force, et la vigueur de ma main qui m’ont acquis toutes ces choses;
18 Lakini kumbukeni Bwana Mungu wenu, ndiye ambaye huwapa uwezo wa kupata utajiri, na hivyo kulithibitisha Agano lake, ambalo aliwaapia baba zenu, kama ilivyo leo.
Mais que tu te souviennes que c’est le Seigneur ton Dieu lui-même qui t’a donné des forces, afin qu’il accomplît ainsi l’alliance au sujet de laquelle il a juré à tes pères, comme le montre le présent jour.
19 Ikiwa mtamsahau Bwana Mungu wenu, mkaifuata miungu mingine, mkaiabudu na kuisujudia, ninashuhudia dhidi yenu leo kwamba hakika mtaangamizwa.
Mais si, oubliant le Seigneur ton Dieu, tu suis des dieux étrangers, et que tu les serves et les adores, voici maintenant que je te prédis que tu périras entièrement.
20 Kama mataifa Bwana aliyoyaangamiza mbele yenu, ndivyo ninyi mtakavyoangamizwa kwa kutokumtii Bwana Mungu wenu.
Comme les nations qu’a détruites le Seigneur à ton entrée, ainsi vous aussi, vous périrez, si vous êtes désobéissants à la voix du Seigneur votre Dieu.

< Torati 8 >