< Torati 8 >

1 Uwe mwangalifu kufuata kila agizo ninalokupa wewe leo, ili mweze kuishi, kuongezeka na mweze kuingia mkamiliki nchi ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zenu.
“You must faithfully obey all the commandments that I am giving you today. If you do that, you will live [a long time], you will become very numerous, and you will occupy the land that Yahweh solemnly promised your ancestors that he would give [to you].
2 Kumbuka jinsi Bwana Mungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la.
And do not forget how Yahweh our God led us as we traveled through the desert during these past 40 years. He [caused you to have many problems/difficulties], because he wanted to cause you to realize that you needed to trust him and not yourselves. And he wanted to test you, to find out what you intended to do [IDM], whether you would obey his commandments or not.
3 Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Bwana.
So he caused you to have/experience difficulties. He allowed you to become hungry. Then he gave you manna [food from heaven], food that you and your ancestors had never eaten before. He did that to teach you that people need food [for their bodies]; but [they also need food for their spirits, which comes from paying attention to] everything that Yahweh says [MTY].
4 Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini.
During those 40 years [of walking through the desert], our clothes did not wear out and our feet did not swell [from walking a very long way through the desert].
5 Mjue basi ndani ya mioyo yenu kama mtu anavyomwadibisha mwanawe, ndivyo Bwana Mungu wako atawaadibisha ninyi.
Do not forget that Yahweh our God disciplines us, like parents discipline their children.
6 Shikeni maagizo ya Bwana Mungu wenu mtembee katika njia zake na kumheshimu.
“Do obey the commandments of Yahweh our God, and conduct your lives as he wants you to do, and revere him.
7 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi yenye vijito na mabwawa ya maji, yenye chemchemi zinazotiririka mabondeni na katika vilima;
He is about to bring you into a good/fertile land, which has streams which flow down from the hills and pour/flow out of springs in the valleys.
8 nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu na mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni na asali;
It is a land on which wheat and barley grow, a land where there are fig trees and pomegranates, and a land where there are olive trees and honey.
9 nchi ambayo chakula hakitapungua na hamtakosa chochote; nchi ambayo miamba yake ni chuma na mnaweza kuchimba shaba kutoka kwenye vilima.
It is a land where there will be plenty of food for you, where you will (not lack anything/have everything that you need) [LIT], a land which has iron [ore] in its rocks and from which you can dig copper [ore] from its hills.
10 Wakati mtakapokwisha kula na kushiba, msifuni Bwana Mungu wenu kwa ajili ya nchi nzuri aliyowapa.
[Every day] you will eat until your stomachs are full, and you will thank Yahweh our God for the fertile/good land that he has given you.
11 Jihadharini msimsahau Bwana Mungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo.
But, [when that happens], be sure not to forget Yahweh our God by disobeying his commandments and rules and regulations that I am giving to you today.
12 Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo,
When your stomachs are full [every day], and when you have built good houses and are living in them,
13 na wakati makundi yenu ya ngʼombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa,
and when the number of your cattle and sheep has greatly increased, and when you have accumulated a large amount of silver and gold, and the amount of all your other possessions has greatly increased,
14 basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahau Bwana Mungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
be sure that you do not become proud [IDM] and forget Yahweh our God, who rescued your ancestors from being slaves in Egypt and brought them out from there.
15 Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu.
Do not forget that he led them [while they traveled] through that huge and terrible desert, where there were poisonous snakes and scorpions. And do not forget that where the ground was very dry and there was no water, he caused water to flow for them out of (solid/very hard) rock.
16 Aliwapa mana ya kula jangwani, kitu ambacho baba zenu hawakukijua, ili kuwanyenyekesha na kuwajaribu ninyi ili mwishoni apate kuwatendea mema.
Do not forget that in that desert he gave your ancestors manna to eat, food that they had never eaten before. He [caused them to have/experience many problems/difficulties], because he wanted them to realize that they needed to trust him and not themselves. And he wanted to test them, to find out whether they intended to obey him, in order that when [those difficulties] ended, he would do many good things for them.
17 Mnaweza kusema, “Uwezo wangu na nguvu za mikono yangu ndizo zilizonipatia utajiri huu.”
Be sure that you do not think to yourselves, ‘I have acquired all these things by my own power [MTY] and ability.’
18 Lakini kumbukeni Bwana Mungu wenu, ndiye ambaye huwapa uwezo wa kupata utajiri, na hivyo kulithibitisha Agano lake, ambalo aliwaapia baba zenu, kama ilivyo leo.
Do not forget that it is Yahweh our God who has enabled you to become rich. He does this because he faithfully does what he solemnly promised our ancestors that he would do.
19 Ikiwa mtamsahau Bwana Mungu wenu, mkaifuata miungu mingine, mkaiabudu na kuisujudia, ninashuhudia dhidi yenu leo kwamba hakika mtaangamizwa.
“solemnly warn you that if you forget Yahweh our God and turn to other gods and start to serve them and worship them, you will certainly be destroyed.
20 Kama mataifa Bwana aliyoyaangamiza mbele yenu, ndivyo ninyi mtakavyoangamizwa kwa kutokumtii Bwana Mungu wenu.
If you do not obey Yahweh our God, he will certainly destroy you just like he will destroy the people-groups that you will fight against.”

< Torati 8 >