< Torati 6 >
1 Haya ndiyo maagizo, amri na sheria ambazo Bwana Mungu wenu aliniagiza niwafundishe ninyi ili mpate kuyashika katika nchi ambayo ninyi mnavuka Yordani kuimiliki,
(and this *L(P)*) [the] commandment [the] statute: decree and [the] justice: judgement which to command LORD God your to/for to learn: teach [obj] you to/for to make: do in/on/with land: country/planet which you(m. p.) to pass there [to] to/for to possess: take her
2 ili kwamba ninyi, watoto wenu na watoto wao baada yao wamche Bwana Mungu wenu siku zote kwa kushika amri na maagizo yake yote ninayowapa, ili mweze kuyafurahia maisha marefu.
because to fear: revere [obj] LORD God your to/for to keep: obey [obj] all statute his and commandment his which I to command you you(m. s.) and son: child your and son: child son: child your all day life your and because to prolong [emph?] day your
3 Sikia, ee Israeli, nawe uwe mwangalifu kutii ili upate kufanikiwa na kuongezeka sana katika nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi ninyi.
and to hear: hear Israel and to keep: careful to/for to make: do which be good to/for you and which to multiply [emph?] much like/as as which to speak: promise LORD God father your to/for you land: country/planet to flow: flowing milk and honey
4 Sikia, ee Israeli: Bwana Mungu wako, Bwana ni mmoja.
to hear: hear Israel LORD God our LORD one
5 Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.
and to love: lover [obj] LORD God your in/on/with all heart your and in/on/with all soul your and in/on/with all much your
6 Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako.
and to be [the] word [the] these which I to command you [the] day upon heart your
7 Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo.
and to sharpen them to/for son: child your and to speak: speak in/on/with them in/on/with to dwell you in/on/with house: home your and in/on/with to go: walk you in/on/with way: journey and in/on/with to lie down: lay down you and in/on/with to arise: rise you
8 Zifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako.
and to conspire them to/for sign: indicator upon hand your and to be to/for phylacteries between eye your
9 Ziandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.
and to write them upon doorpost house: home your and in/on/with gate your
10 Wakati Bwana Mungu wako atakapokuleta katika nchi aliyowaapia baba zako, Abrahamu, Isaki na Yakobo, kukupa wewe, nchi kubwa, ina miji inayopendeza ambayo hukuijenga,
and to be for to come (in): bring you LORD God your to(wards) [the] land: country/planet which to swear to/for father your to/for Abraham to/for Isaac and to/for Jacob to/for to give: give to/for you city great: large and pleasant which not to build
11 nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina nyingi ambavyo hukuvijaza, visima ambavyo hukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukupanda wewe, basi, utakapokula na kushiba,
and house: home full all goodness which not to fill and pit to hew which not to hew vineyard and olive which not to plant and to eat and to satisfy
12 jihadhari usije ukamwacha Bwana, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
to keep: careful to/for you lest to forget [obj] LORD which to come out: send you from land: country/planet Egypt from house: home servant/slave
13 Utamcha Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake na kuapa kwa jina lake.
[obj] LORD God your to fear: revere and [obj] him to serve and in/on/with name his to swear
14 Usifuate miungu mingine, miungu ya mataifa yanayokuzunguka;
not to go: follow [emph?] after God another from God [the] people which around you
15 kwa kuwa Bwana Mungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka uso wa nchi.
for God jealous LORD God your in/on/with entrails: among your lest to be incensed face: anger LORD God your in/on/with you and to destroy you from upon face: surface [the] land: planet
16 Usimjaribu Bwana Mungu wako kama ulivyofanya huko Masa.
not to test [obj] LORD God your like/as as which to test in/on/with Massah
17 Utayashika maagizo ya Bwana Mungu wako kwa bidii, na masharti na amri alizokupa.
to keep: careful to keep: obey [emph?] [obj] commandment LORD God your and testimony his and statute: decree his which to command you
18 Fanya lililo haki na jema mbele za Bwana, ili upate kufanikiwa, uweze kuingia na kuimiliki nchi nzuri ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zako,
and to make: do [the] upright and [the] pleasant in/on/with eye: seeing LORD because be good to/for you and to come (in): come and to possess: take [obj] [the] land: country/planet [the] pleasant which to swear LORD to/for father your
19 kuwafukuza kwa nguvu adui zako mbele yako kama Bwana alivyosema.
to/for to thrust [obj] all enemy your from face: before your like/as as which to speak: promise LORD
20 Siku zijazo, mtoto wako atakapokuuliza, “Ni nini maana ya masharti haya, amri na sheria hizi ambazo Bwana Mungu wako alikuagiza wewe?”
for to ask you son: child your tomorrow to/for to say what? [the] testimony and [the] statute: decree and [the] justice: judgement which to command LORD God our [obj] you
21 Mwambie: “Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, lakini Bwana alitutoa sisi kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu.
and to say to/for son: child your servant/slave to be to/for Pharaoh in/on/with Egypt and to come out: send us LORD from Egypt in/on/with hand: power strong
22 Bwana akapeleka mbele yetu ishara za miujiza na maajabu makubwa na ya kutisha mno juu ya Misri na Farao pamoja na nyumba yake yote.
and to give: give LORD sign: miraculous and wonder great: large and bad: harmful in/on/with Egypt in/on/with Pharaoh and in/on/with all house: household his to/for eye: before(the eyes) our
23 Lakini Mungu akatutoa huko, akatuleta na kutupa nchi hii ambayo aliwaahidi baba zetu kwa kiapo.
and [obj] us to come out: send from there because to come (in): bring [obj] us to/for to give: give to/for us [obj] [the] land: country/planet which to swear to/for father our
24 Bwana akatuagiza tutii amri hizi zote na kumcha Bwana Mungu wetu, ili tupate kustawi na kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo.
and to command us LORD to/for to make: do [obj] all [the] statute: decree [the] these to/for to fear: revere [obj] LORD God our to/for good to/for us all [the] day: always to/for to live us like/as [the] day: today [the] this
25 Kama tukizitii kwa bidii amri hizi zote mbele za Bwana Mungu wetu, kama alivyotuamuru sisi, hiyo itakuwa haki yetu.”
and righteousness to be to/for us for to keep: careful to/for to make: do [obj] all [the] commandment [the] this to/for face: before LORD God our like/as as which to command us