< Torati 6 >

1 Haya ndiyo maagizo, amri na sheria ambazo Bwana Mungu wenu aliniagiza niwafundishe ninyi ili mpate kuyashika katika nchi ambayo ninyi mnavuka Yordani kuimiliki,
And these [are] the commands, and the ordinances, and the judgments, as many as the Lord our God gave commandment to teach you to do so in the land on which ye enter to inherit it.
2 ili kwamba ninyi, watoto wenu na watoto wao baada yao wamche Bwana Mungu wenu siku zote kwa kushika amri na maagizo yake yote ninayowapa, ili mweze kuyafurahia maisha marefu.
That ye may fear the Lord your God, keep ye all his ordinances, and his commandments, which I command thee to-day, thou, and thy sons, and thy sons' sons, all the days of thy life, that ye may live many days.
3 Sikia, ee Israeli, nawe uwe mwangalifu kutii ili upate kufanikiwa na kuongezeka sana katika nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi ninyi.
Hear, therefore, O Israel, and observe to do them, that it may be well with thee, and that ye may be greatly multiplied, as the Lord God of thy fathers said that he would give thee a land flowing with milk and honey: and these [are] the ordinances, and the judgments, which the Lord commanded the children of Israel in the wilderness, when they had gone forth from the land of Egypt.
4 Sikia, ee Israeli: Bwana Mungu wako, Bwana ni mmoja.
Hear, O Israel, The Lord our God is one Lord.
5 Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.
And thou shalt love the Lord thy God with all thy mind, and with all thy soul, and all thy strength.
6 Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako.
And these words, all that I command thee this day, shall be in thy heart and in thy soul.
7 Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo.
And thou shalt teach them to thy children, and thou shalt speak of them sitting in the house, and walking by the way, and lying down, and rising up.
8 Zifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako.
And thou shalt fasten them for a sign upon thy hand, and it shall be immoveable before thine eyes.
9 Ziandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.
And ye shall write them on the lintels of your houses and of your gates.
10 Wakati Bwana Mungu wako atakapokuleta katika nchi aliyowaapia baba zako, Abrahamu, Isaki na Yakobo, kukupa wewe, nchi kubwa, ina miji inayopendeza ambayo hukuijenga,
And it shall come to pass when the Lord thy God shall have brought thee into the land which he sware to thy fathers, to Abraam, and to Isaac, and to Jacob, to give thee great and beautiful cities which thou didst not build,
11 nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina nyingi ambavyo hukuvijaza, visima ambavyo hukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hukupanda wewe, basi, utakapokula na kushiba,
houses full of all good things which thou didst not fill, wells dug in the rock which thou didst not dig, vineyards and oliveyards which thou didst not plant, then having eaten and been filled,
12 jihadhari usije ukamwacha Bwana, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
beware lest thou forget the Lord thy God that brought thee forth out of the land of Egypt, out of the house of bondage.
13 Utamcha Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake na kuapa kwa jina lake.
Thou shalt fear the Lord thy God, and him only shalt thou serve; and thou shalt cleave to him, and by his name thou shalt swear.
14 Usifuate miungu mingine, miungu ya mataifa yanayokuzunguka;
Go ye not after other gods of the gods of the nations round about you;
15 kwa kuwa Bwana Mungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka uso wa nchi.
for the Lord thy God in the midst of thee [is] a jealous God, lest the Lord thy God be very angry with thee, and destroy thee from off the face of the earth.
16 Usimjaribu Bwana Mungu wako kama ulivyofanya huko Masa.
Thou shalt not tempt the Lord thy God, as ye tempted him in the temptation.
17 Utayashika maagizo ya Bwana Mungu wako kwa bidii, na masharti na amri alizokupa.
Thou shalt by all means keep the commands of the Lord thy God, the testimonies, and the ordinances, which he commanded thee.
18 Fanya lililo haki na jema mbele za Bwana, ili upate kufanikiwa, uweze kuingia na kuimiliki nchi nzuri ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zako,
And thou shalt do that which is pleasing and good before the Lord thy God, that it may be well with thee, and that thou mayest go in and inherit the good land, which the Lord sware to your fathers,
19 kuwafukuza kwa nguvu adui zako mbele yako kama Bwana alivyosema.
to chase all thine enemies from before thy face, as the Lord said.
20 Siku zijazo, mtoto wako atakapokuuliza, “Ni nini maana ya masharti haya, amri na sheria hizi ambazo Bwana Mungu wako alikuagiza wewe?”
And it shall come to pass when thy son shall ask thee at a future time, saying, What are the testimonies, and the ordinances, and the judgments, which the Lord our God has commanded us?
21 Mwambie: “Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, lakini Bwana alitutoa sisi kutoka Misri kwa mkono wenye nguvu.
Then shalt thou say to thy son, We were slaves to Pharao in the land of Egypt, and the Lord brought us forth thence with a mighty hand, and with a high arm.
22 Bwana akapeleka mbele yetu ishara za miujiza na maajabu makubwa na ya kutisha mno juu ya Misri na Farao pamoja na nyumba yake yote.
And the Lord wrought signs and great and grievous wonders in Egypt, on Pharao and on his house before us.
23 Lakini Mungu akatutoa huko, akatuleta na kutupa nchi hii ambayo aliwaahidi baba zetu kwa kiapo.
And he brought us out thence to give us this land, which he sware to give to our fathers.
24 Bwana akatuagiza tutii amri hizi zote na kumcha Bwana Mungu wetu, ili tupate kustawi na kuendelea kuwa hai kama ilivyo leo.
And the Lord charged us to observe all these ordinances; to fear the Lord our God, that it may be well with us for ever, that we may live, as even to-day.
25 Kama tukizitii kwa bidii amri hizi zote mbele za Bwana Mungu wetu, kama alivyotuamuru sisi, hiyo itakuwa haki yetu.”
And there shall be mercy to us, if we take heed to keep all these commands before the Lord our God, as he has commanded us.

< Torati 6 >