< Torati 5 >

1 Mose akawaita Israeli wote, akawaambia: Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata.
موسی به سخنانش ادامه داده، گفت: ای قوم اسرائیل، اکنون به فرایض و قوانینی که به شما می‌دهم، گوش کنید. آنها را یاد بگیرید و به دقت انجام دهید.
2 Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu.
یهوه، خدایمان در کوه حوریب عهدی با ما بست.
3 Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo.
این عهد را نه با پدرانمان بلکه با ما که امروز زنده هستیم بست.
4 Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima.
او در آن کوه از میان آتش رو در رو با شما سخن گفت.
5 (Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:
من به عنوان واسطه‌ای بین شما و خداوند ایستادم، زیرا شما از آن آتش می‌ترسیدید و بالای کوه پیش او نرفتید. او با من سخن گفت و من قوانینش را به شما سپردم. آنچه فرمود این است:
6 “Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
«من خداوند، خدای تو هستم، همان خدایی که تو را از اسارت و بندگی مصر آزاد کرد.
7 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
«تو را خدایان دیگر غیر از من نباشد.
8 Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.
«هیچگونه بُتی به شکل آنچه بالا در آسمان و آنچه بر زمین و آنچه در دریاست برای خود درست نکن.
9 Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
در برابر آنها زانو نزن و آنها را پرستش نکن، زیرا من که خداوند، خدای تو می‌باشم، خدای غیوری هستم و کسانی را که از من نفرت دارند مجازات می‌کنم. این مجازات شامل حال فرزندان آنها تا نسل سوم و چهارم نیز می‌گردد.
10 lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
اما بر کسانی که مرا دوست بدارند و دستورهای مرا پیروی کنند، تا هزار پشت رحمت می‌کنم.
11 Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
«نام یهوه، خدای خود را نابجا به کار نبر. اگر نام مرا با بی‌احترامی بر زبان بیاوری یا به آن قسم دروغ بخوری، تو را بی‌سزا نخواهم گذاشت.
12 Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza.
«روز شَبّات را به یاد داشته باش و آن را مقدّس بدار. من که خداوند، خدای تو هستم این را به تو امر می‌کنم.
13 Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote.
در هفته شش روز کار کن،
14 Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe.
ولی در روز هفتم که شَبّات یهوه خدای توست هیچ کاری نکن نه خودت، نه پسرت، نه دخترت، نه غلامت، نه کنیزت، نه مهمانانت و نه حتی چارپایانت. غلام و کنیزت باید مثل خودت استراحت کنند.
15 Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.
به یاد آور که در سرزمین مصر غلام بودی و من که خداوند، خدای تو هستم با قدرت و قوت عظیم خود تو را از آنجا بیرون آوردم. به این دلیل است که به تو امر می‌کنم شَبّات را نگه داری.
16 Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.
«پدر و مادر خود را گرامی بدار، زیرا این فرمان خداوند، خدای توست. اگر چنین کنی، در سرزمینی که خداوند، خدایت به تو خواهد بخشید، عمری طولانی و پربرکت خواهی داشت.
17 Usiue.
«قتل نکن.
18 Usizini.
«زنا نکن.
19 Usiibe.
«دزدی نکن.
20 Usimshuhudie jirani yako uongo.
«بر همنوع خود شهادت دروغ نده.
21 Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”
«به زن همسایه‌ات طمع نکن. و حسرت خانۀ همسایه خود، یا مزرعۀ او، یا غلام و کنیزش، یا گاو و الاغش، یا اموالش را نخور.»
22 Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.
این بود قوانینی که خداوند در کوه سینا به شما داد. او این قوانین را با صدای بلند از میان آتش و ابر غلیظ اعلام فرمود و غیر از این قوانین، قانون دیگری نداد. آنها را روی دو لوح سنگی نوشت و به من داد.
23 Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi.
ولی وقتی که آن صدای بلند از درون تاریکی به گوشتان رسید و آتش مهیب سر کوه را دیدید کلیهٔ رهبران قبایل و مشایخ شما نزد من آمدند
24 Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye.
و گفتند: «امروز خداوند، خدایمان جلال و عظمتش را به ما نشان داده است، ما حتی صدایش را از درون آتش شنیدیم. اکنون می‌دانیم که ممکن است خدا با انسان صحبت کند و او نمیرد.
25 Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi.
پس چرا جان خود را به خطر بیاندازیم؟ بدون شک اگر یهوه خدایمان دوباره با ما سخن بگوید خواهیم مرد. این آتش هولناک، ما را خواهد سوزانید.
26 Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi?
چه کسی می‌تواند صدای خدای زنده را که از درون آتش سخن می‌گوید، بشنود و زنده بماند؟
27 Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”
پس تو برو و به تمامی سخنانی که یهوه خدای ما می‌گوید گوش کن، بعد آمده، آنها را برای ما بازگو کن و ما آنها را پذیرفته، اطاعت خواهیم کرد.»
28 Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri.
خداوند درخواستتان را پذیرفت و به من گفت: «آنچه که قوم اسرائیل به تو گفتند شنیدم و آنچه گفتند نیکوست.
29 Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!
ای کاش همیشه چنین دلی داشته باشند و از من بترسند و تمام اوامر مرا بجا آورند. در آن صورت زندگی خودشان و زندگی فرزندانشان در تمام نسلها با خیر و برکت خواهد گذشت.
30 “Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao.
اکنون برو و به آنها بگو که به خیمه‌هایشان بازگردند.
31 Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”
سپس برگشته، اینجا در کنار من بایست و من تمامی اوامرم را به تو خواهم داد. تو باید آنها را به قوم تعلیم دهی تا فرایض و قوانین مرا در سرزمینی که به ایشان می‌دهم اطاعت کنند.»
32 Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto.
پس بایستی تمام اوامر یهوه، خدایتان را اطاعت کنید و دستورهای او را به دقت به‌جا آورید
33 Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.
و در طریقی که یهوه خدایتان به شما امر کرده گام بردارید و بمانید. اگر چنین کنید در سرزمینی که به تصرف درمی‌آورید زندگی طولانی و پربرکتی خواهید داشت.

< Torati 5 >