< Torati 5 >
1 Mose akawaita Israeli wote, akawaambia: Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata.
Moïse appela tout Israël, et leur dit: « Écoutez, Israël, les lois et les ordonnances que je prononce aujourd'hui à vos oreilles, afin que vous les appreniez et que vous ayez soin de les mettre en pratique. »
2 Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu.
Yahvé, notre Dieu, a fait alliance avec nous à Horeb.
3 Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo.
Yahvé n'a pas fait cette alliance avec nos pères, mais avec nous, même nous, qui sommes tous ici, vivants, aujourd'hui.
4 Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima.
Yahvé vous a parlé face à face sur la montagne, au milieu du feu,
5 (Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:
(je me tenais alors entre Yahvé et vous, pour vous montrer la parole de Yahvé; car vous aviez peur à cause du feu, et vous n'êtes pas montés sur la montagne) en disant,
6 “Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
« Je suis Yahvé ton Dieu, qui t'a fait sortir du pays d'Égypte, de la maison de servitude.
7 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
« Tu n'auras pas d'autres dieux devant moi.
8 Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.
« Tu ne te feras pas d'image taillée, ni de représentation de ce qui est dans les cieux en haut, ni de ce qui est sur la terre en bas, ni de ce qui est dans les eaux sous la terre.
9 Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Tu ne te prosterneras pas devant elles et tu ne les serviras pas, car moi, Yahvé ton Dieu, je suis un Dieu jaloux, qui punit l'iniquité des pères sur les enfants, sur la troisième et la quatrième génération de ceux qui me haïssent
10 lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
et qui fait preuve de bonté envers les milliers de ceux qui m'aiment et qui gardent mes commandements.
11 Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
« Tu n'abuseras pas du nom de Yahvé ton Dieu, car Yahvé ne laissera pas impuni celui qui abusera de son nom.
12 Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza.
« Observe le jour du sabbat, pour le sanctifier, comme Yahvé ton Dieu te l'a ordonné.
13 Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote.
Tu travailleras six jours, et tu feras tout ton ouvrage;
14 Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe.
mais le septième jour est un sabbat pour l'Éternel, ton Dieu, où tu ne feras aucun ouvrage, ni toi, ni ton fils, ni ta fille, ni ton serviteur, ni ta servante, ni ton bœuf, ni ton âne, ni aucun de tes animaux, ni l'étranger qui est dans tes portes, afin que ton serviteur et ta servante se reposent aussi bien que toi.
15 Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.
Tu te souviendras que tu as été esclave au pays d'Égypte, et que Yahvé ton Dieu t'en a fait sortir par une main puissante et un bras étendu. C'est pourquoi Yahvé ton Dieu t'a ordonné d'observer le jour du sabbat.
16 Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.
« Honore ton père et ta mère, comme Yahvé ton Dieu te l'a ordonné, afin que tes jours se prolongent et que tu sois heureux dans le pays que Yahvé ton Dieu te donne.
« Tu ne commettras pas de meurtre.
« Tu ne commettras pas d'adultère.
20 Usimshuhudie jirani yako uongo.
« Tu ne porteras pas de faux témoignage contre ton prochain.
21 Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”
« Tu ne convoiteras pas la femme de ton prochain. Tu ne convoiteras pas non plus la maison de ton prochain, ni son champ, ni son serviteur, ni sa servante, ni son bœuf, ni son âne, ni rien de ce qui appartient à ton prochain. »
22 Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.
Yahvé adressa ces paroles à toute votre assemblée sur la montagne, du milieu du feu, de la nuée et de l'obscurité, avec une voix forte. Il n'ajouta rien de plus. Il les a écrites sur deux tables de pierre et me les a données.
23 Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi.
Lorsque vous avez entendu la voix au milieu des ténèbres, pendant que la montagne était embrasée, vous vous êtes approchés de moi, tous les chefs de vos tribus et vos anciens,
24 Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye.
et vous avez dit: « Voici que Yahvé, notre Dieu, nous a montré sa gloire et sa grandeur, et nous avons entendu sa voix au milieu du feu. Nous avons vu aujourd'hui que Dieu parle à l'homme et qu'il vit.
25 Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi.
Maintenant donc, pourquoi mourrions-nous? Car ce grand feu va nous consumer. Si nous entendons encore la voix de Yahvé notre Dieu, nous mourrons.
26 Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi?
Car qui, de toute chair, a entendu comme nous la voix du Dieu vivant, parlant du milieu du feu, et a vécu?
27 Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”
Approchez-vous, et écoutez tout ce que l'Éternel, notre Dieu, dira, et dites-nous tout ce que l'Éternel, notre Dieu, vous dira; nous l'écouterons et nous le ferons. »
28 Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri.
L'Éternel a entendu la voix de tes paroles quand tu m'as parlé, et l'Éternel m'a dit: « J'ai entendu la voix des paroles de ce peuple, qu'il t'a dites. Ils ont bien dit tout ce qu'ils ont dit.
29 Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!
Oh! s'il y avait en eux un cœur tel qu'ils me craignent et gardent toujours tous mes commandements, afin que tout aille bien pour eux et pour leurs enfants à jamais!
30 “Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao.
Allez leur dire: « Retournez dans vos tentes ».
31 Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”
Mais toi, reste ici près de moi, et je te dirai tous les commandements, les lois et les ordonnances que tu leur enseigneras, afin qu'ils les mettent en pratique dans le pays dont je leur donne la possession. »
32 Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto.
Tu feras donc ce que Yahvé ton Dieu t'a ordonné. Tu ne te détourneras ni à droite ni à gauche.
33 Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.
Tu marcheras dans toute la voie que l'Éternel, ton Dieu, t'a prescrite, afin que tu vives et que tu sois heureux, et afin que tu prolonges tes jours dans le pays dont tu auras la possession.