< Torati 5 >

1 Mose akawaita Israeli wote, akawaambia: Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata.
And Moses calleth unto all Israel, and saith unto them, 'Hear, Israel, the statutes and the judgments which I am speaking in your ears to-day, and ye have learned them, and have observed to do them.
2 Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu.
Jehovah our God made with us a covenant in Horeb;
3 Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo.
not with our fathers hath Jehovah made this covenant, but with us; we — these — here to-day — all of us alive.
4 Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima.
Face to face hath Jehovah spoken with you, in the mount, out of the midst of the fire;
5 (Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:
I am standing between Jehovah and you, at that time, to declare to you the word of Jehovah, for ye have been afraid from the presence of the fire, and ye have not gone up into the mount; saying:
6 “Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
'I Jehovah [am] thy God, who hath brought thee out from the land of Egypt, from a house of servants.
7 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
'Thou hast no other gods in My presence.
8 Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.
'Thou dost not make to thee a graven image, any similitude which [is] in the heavens above, and which [is] in the earth beneath, and which [is] in the waters under the earth;
9 Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
thou dost not bow thyself to them nor serve them, for I Jehovah thy God [am] a zealous God, charging iniquity of fathers on children, and on a third [generation], and on a fourth, to those hating Me;
10 lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
and doing kindness to thousands, to those loving Me, and to those keeping My commands.
11 Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
'Thou dost not take up the Name of Jehovah thy God for a vain thing, for Jehovah doth not acquit him who taketh up His Name for a vain thing.
12 Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza.
'Observe the day of the sabbath — to sanctify it, as Jehovah thy God hath commanded thee;
13 Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote.
six days thou dost labour, and hast done all thy work,
14 Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe.
and the seventh day [is] a sabbath to Jehovah thy God; thou dost not do any work, thou, and thy son, and thy daughter, and thy man-servant, and thy handmaid, and thine ox, and thine ass, and all thy cattle, and thy sojourner who [is] within thy gates; so that thy man-servant, and thy handmaid doth rest like thyself;
15 Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.
and thou hast remembered that a servant thou hast been in the land of Egypt, and Jehovah thy God is bringing thee out thence by a strong hand, and by a stretched-out arm; therefore hath Jehovah thy God commanded thee to keep the day of the sabbath.
16 Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.
'Honour thy father and thy mother, as Jehovah thy God hath commanded thee, so that thy days are prolonged, and so that it is well with thee, on the ground which Jehovah thy God is giving to thee.
17 Usiue.
'Thou dost not murder.
18 Usizini.
'Thou dost not commit adultery.
19 Usiibe.
'Thou dost not steal.
20 Usimshuhudie jirani yako uongo.
'Thou dost not answer against thy neighbour — a false testimony.
21 Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”
'Thou dost not desire thy neighbour's wife; nor dost thou covet thy neighbour's house, his field, and his man-servant, and his handmaid, his ox, and his ass, and anything which [is] thy neighbour's.
22 Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.
'These words hath Jehovah spoken unto all your assembly, in the mount out of the midst of the fire, of the cloud, and of the thick darkness — a great voice; and He hath not added, and He writeth them on two tables of stone, and giveth them unto me.
23 Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi.
'And it cometh to pass as ye hear the voice out of the midst of the darkness, and of the mountain burning with fire, that ye come near unto me, all the heads of your tribes, and your elders,
24 Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye.
and say, Lo, Jehovah our God hath shewed us His honour, and His greatness; and His voice we have heard out of the midst of the fire; this day we have seen that God doth speak with man — and he hath lived.
25 Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi.
'And, now, why do we die? for consume us doth this great fire — if we add to hear the voice of Jehovah our God any more — then we have died.
26 Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi?
For who of all flesh [is] he who hath heard the voice of the living God speaking out of the midst of the fire like us — and doth live?
27 Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”
Draw near thou, and hear all that which Jehovah our God saith, and thou, thou dost speak unto us all that which Jehovah our God speaketh unto thee, and we have hearkened, and done it.
28 Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri.
'And Jehovah heareth the voice of your words, in your speaking unto me, and Jehovah saith unto me, I have heard the voice of the words of this people which they have spoken unto thee; they have done well [in] all that they have spoken.
29 Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!
O that their heart had been thus to them, to fear Me, and to keep My commands all the days, that it may be well with them, and with their sons — to the age!
30 “Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao.
'Go, say to them, Turn back for yourselves, to your tents;
31 Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”
and thou here stand thou with Me, and let Me speak unto thee all the command, and the statutes, and the judgments which thou dost teach them, and they have done in the land which I am giving to them to possess it.
32 Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto.
'And ye have observed to do as Jehovah your God hath commanded you, ye turn not aside — right or left;
33 Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.
in all the way which Jehovah your God hath commanded you ye walk, so that ye live, and [it is] well with you, and ye have prolonged days in the land which ye possess.

< Torati 5 >