< Torati 5 >
1 Mose akawaita Israeli wote, akawaambia: Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata.
And Moses called all Israel, and said unto them, Hear, O Israel, the statutes and the ordinances which I speak in your ears this day, that ye may learn them, and that ye may observe to do them.
2 Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu.
The Lord our God made a covenant with us in Horeb.
3 Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo.
Not with our fathers did the Lord make this covenant, but with us, we who are here all of us alive this day.
4 Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima.
Face to face did the Lord speak with you on the mount, out of the midst of the fire,
5 (Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:
(I was standing between the Lord and between you at that time, to announce to you the word of the Lord; for ye were afraid by reason of the fire, and ye went not up into the mount; ) saying,
6 “Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
I am the Lord thy God, who have brought thee out of the land of Egypt, from the house of slavery.
7 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Thou shalt have no other gods before me.
8 Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.
Thou shalt not make unto thyself any graven image, any likeness of any thing that is in the heavens above, or that is on the earth beneath, or that is in the water under the earth:
9 Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Thou shalt not bow thyself down unto them, nor serve them; for I the Lord thy God am a jealous God, visiting the iniquity of the fathers upon the children, and upon the third and upon the fourth generation of them that hate me,
10 lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
And showing kindness unto the thousandth generation of them that love me, and keep my commandments.
11 Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
Thou shalt not take the name of the Lord thy God in vain; for the Lord will not hold him guiltless that taketh his name in vain.
12 Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza.
Keep the sabbath-day to sanctify it, as the Lord thy God hath commanded thee.
13 Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote.
Six days shalt thou labor, and do all thy work;
14 Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe.
But the seventh day is the sabbath in honor of the Lord thy God; on it thou shalt not do any work, neither thou, nor thy son, nor thy daughter, nor thy man-servant, nor thy maid-servant, nor thy ox, nor thy ass, nor any of thy cattle, nor thy stranger that is within thy gates: in order that thy man-servant and thy maid-servant may rest as well as thou.
15 Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.
And thou shalt remember that thou hast been a servant in the land of Egypt, and that the Lord thy God brought thee out from there by a mighty hand and by an outstretched arm; therefore hath the Lord thy God commanded thee to observe the sabbath-day.
16 Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.
Honor thy father and thy mother, as the Lord thy God hath commanded thee: in order that thy days may be prolonged, and in order that it may go well with thee, in the land which the Lord thy God giveth thee.
Neither shalt thou commit adultery.
Neither shalt thou steal.
20 Usimshuhudie jirani yako uongo.
Neither shalt thou bear false witness against thy neighbor.
21 Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”
Neither shalt thou covet thy neighbor's wife. Neither shalt thou desire thy neighbor's house, nor his field, nor his man-servant, nor his maid-servant, nor his ox, nor his ass, nor anything that is thy neighbor's.
22 Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.
These words did the Lord speak unto all your assembly on the mount out of the midst of the fire, of the cloud, and of the thick darkness, with a great voice, but he did so no more; and he wrote them on two tables of stone, and he gave them unto me.
23 Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi.
And it came to pass, when ye heard the voice out of the midst of the darkness, while the mount was burning with fire, that ye came near unto me, even all the heads of your tribes, and your elders;
24 Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye.
And ye said, Behold, the Lord our God hath caused us to see his glory and his greatness, and his voice have we heard out of the midst of the fire: this day have we seen that God can speak with man, who nevertheless may live.
25 Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi.
But now why should we die? for this great fire may consume us; if we continue to hear the voice of the Lord our God any more, then shall we die.
26 Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi?
For where is there any flesh, that hath heard the voice of the living God speaking out of the midst of the fire, like us, and hath remained alive?
27 Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”
Do thou approach, and hear all that the Lord our God may say; and thou shalt speak unto us all that the Lord our God may speak unto thee; and we will hear and do it.
28 Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri.
And the Lord heard the voice of your words, while ye were speaking unto me; and the Lord said unto me, I have heard the voice of the words of this people, which they have spoken unto thee: they have done well in all that they have spoken.
29 Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!
Who would grant that this their heart might remain in them, to fear me, and to keep all my commandments at all times; in order that it might be well with them, and with their children for ever!
30 “Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao.
Go, say to them, Return you unto your tents.
31 Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”
But as for thee, remain thou here by me, and I will speak unto thee all the commandments, and the statutes, and the ordinances, which thou shalt teach them, that they may do them in the land which I give them to possess it.
32 Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto.
Observe ye then to do as the Lord your God hath commanded you: ye shall not turn aside to the right or to the left.
33 Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.
altogether in the way, which the Lord your God hath commanded you, shall ye walk; in order that ye may live, and that it may be well with you, and that ye may remain many days in the land which ye will possess.