< Torati 5 >

1 Mose akawaita Israeli wote, akawaambia: Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata.
Then Moses called all the Israelites together and told them: Listen, people of Israel to the rules and regulations that I'm giving you today. Learn them and make sure you follow them carefully.
2 Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu.
Remember that the Lord our God made an agreement with us at Horeb.
3 Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo.
He didn't make this agreement with our fathers, but with us, all of those who are still alive today.
4 Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima.
The Lord talked with you person to person from the fire on the mountain.
5 (Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:
This was the time when I stood between the Lord and you to tell you what the Lord said, because you were afraid of the fire and refused to go up the mountain. He told you,
6 “Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
“I am the Lord your God, who led you out of Egypt, out of the prison-house of slavery.
7 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
You must not have any other gods except me.
8 Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.
You must not make for yourself any kind of idol, whether in the form of anything in the heavens above, or on the earth beneath, or in the waters below.
9 Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
You must not bow down before them or worship them; for I am the Lord your God and I am passionately exclusive. I lay the consequences of the sin of those who hate me on their sons, grandsons, and great-grandsons;
10 lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
but I show trustworthy love to the thousands of generations who love me and keep my commandments.
11 Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
You must not use the name of the Lord your God in a wrong way, for the Lord will not forgive anyone who uses his name in a wrong way.
12 Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza.
Remember the Sabbath day to keep it holy, as the Lord as the Lord your God has commanded you to do.
13 Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote.
You have six days to work and earn your living,
14 Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe.
but the seventh day is the Sabbath to honor the Lord your God. On this day you must not do any work—not you, not your son or daughter, not your male slave or female slave or your ox or donkey or any of your livestock, and not the foreigner who is staying with you, so that your male slave and females slave can have the same rest as you.
15 Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.
Remember that you were once slaves in Egypt, and that the Lord your God led you out from there with his great power and incredible strength. This is why the Lord your God has ordered you to keep the Sabbath day.
16 Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.
Honor your father and your mother, as the Lord your God has commanded you to do, so that you may live a long time and do well in the land that the Lord your God is giving you.
17 Usiue.
You must not kill people.
18 Usizini.
You must not commit adultery.
19 Usiibe.
You must not steal.
20 Usimshuhudie jirani yako uongo.
You must not give false evidence against others.
21 Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”
You must not desire to have anyone else's wife. You must not desire to have their house or field, or their male slave or female slave, or their ox or donkey, or anything that belongs to them.”
22 Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.
In a loud voice the Lord gave these commandments to all of you, speaking from the fire, the cloud, and the deep darkness that covered the mountain. He didn't add anything else. He wrote them down on two tablets of stone and gave them to me.
23 Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi.
When you heard the voice that came from the darkness while the mountain was on fire, all your tribal leaders and elders came to me,
24 Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye.
and said, “Listen, the Lord our God has revealed glory and majesty to us, and we have heard his voice that came from the fire. Today we have seen that human beings can don't die even when God speaks with them.
25 Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi.
But we could still die, couldn't we? This enormous fire is going to burn us up, and we'll die if the Lord our God continues to speak to us.
26 Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi?
Has anybody else ever heard the living God speak from the fire and survived, we have?
27 Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”
You go and listen to everything the Lord our God tells you. Then you can repeat to us everything the Lord our God tells you. We promise to listen and obey.”
28 Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri.
The Lord heard what you told me, and he said to me, “I've heard what these people told you. All that they've said is good.
29 Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!
I only wish they really did respect me and always kept my commandments so that they and their children would do well for all time.
30 “Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao.
Go and tell them: ‘You need to return to your tents.’
31 Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”
But you are to stay here with me so that I can give you all the commandments and rules and regulations you are to teach them to follow in the country that I am giving them to take over and own.”
32 Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto.
So make sure you do what the Lord your God has ordered you to do—don't go astray in any direction.
33 Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.
Follow all the ways the Lord your God has shown you, so that you do well and live long lives in the country that you will occupy.

< Torati 5 >