< Torati 4 >
1 Sikia sasa, ee Israeli, amri na sheria nitakazokufundisha wewe. Zifuate ili upate kuishi na uingie kuimiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zako anawapa.
Maintenant, Israël, écoute les préceptes et les ordonnances que moi je t’enseigne, afin que les pratiquant, tu vives, et que tu possèdes, en y entrant, la terre que le Seigneur Dieu de vos pères va vous donner.
2 Usiongeze wala usipunguze chochote ninachowaamuru ninyi, ila myashike maagizo ya Bwana Mungu wenu ambayo nawapa.
Vous n’ajouterez point à la parole que je vous dis, et vous n’en retrancherez point: gardez les commandements du Seigneur votre Dieu que moi, je vous prescris.
3 Mliona kwa macho yenu wenyewe kile Bwana alichokifanya kule Baal-Peori. Bwana Mungu wenu aliwaangamiza kutoka miongoni mwenu kila mmoja aliyemfuata Baali wa Peori,
Vos yeux ont vu tout ce qu’a fait le Seigneur contre Béelphégor, comment il a brisé tous ses adorateurs du milieu de vous.
4 lakini ninyi nyote mlioshikamana na Bwana kwa uthabiti, Mungu wenu, mko hai mpaka leo.
Mais vous qui êtes attachés au Seigneur votre Dieu, vous vivez tous jusqu’au présent jour.
5 Tazama, nimewafundisha amri na sheria kama Bwana Mungu wangu alivyoniamuru mimi, ili mzifuate katika nchi mnayoiingia kuimiliki.
Vous savez que je vous ai enseigné les préceptes et les lois, comme m’a commandé le Seigneur mon Dieu: ainsi, vous les pratiquerez dans la terre que vous allez posséder;
6 Zishikeni kwa uangalifu, kwa kuwa hii itaonyesha hekima na ufahamu wenu kwa mataifa, ambayo yatasikia kuhusu amri zote hizi, nao watasema, “Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na ufahamu.”
Vous les observerez et les accomplirez par vos œuvres. Car telles sont votre sagesse et votre intelligence devant les peuples, afin qu’entendant parler de tous ces préceptes, ils disent: Voici un peuple sage et intelligent, une grande nation.
7 Ni taifa gani jingine lililo kubwa kiasi cha kuwa na miungu yao iliyo karibu nao kama Bwana Mungu wetu alivyo karibu nasi wakati wowote tunapomwomba?
Et il n’est point d’autre nation, si grande qu’elle soit, qui ait des dieux s’approchant délie, comme notre Dieu, qui est présent à toutes nos prières.
8 Nalo ni taifa gani jingine lililo kubwa hivi lenye kuwa na amri na sheria za haki kama hizi ninazoweka mbele yenu leo?
Quelle est, en effet, l’autre nation assez illustre pour qu’elle ait des cérémonies, des ordonnances justes, et toute cette loi que j’exposerai aujourd’hui devant vos yeux?
9 Mwe waangalifu, na makini ili msije mkasahau mambo ambayo mliyaona kwa macho yenu, wala kuyaacha yaondoke moyoni mwenu siku zote za uhai wenu. Mwafundishe hayo watoto wenu na watoto wao baada yao.
Garde-toi donc toi-même et ton âme soigneusement. N’oublie point les paroles qu’ont vues tes yeux, et qu’elles ne sortent point de ton cœur tous les jours de ta vie. Tu les enseigneras à tes fils et à tes petits-fils,
10 Kumbuka siku uliyosimama mbele za Bwana Mungu wako kule Horebu, wakati aliponiambia, “Wakutanishe watu mbele yangu wasikie maneno yangu ili kwamba waweze kujifunza kuniheshimu kwa muda wote watakaoishi katika nchi, nao waweze kuwafundisha watoto wao maneno hayo.”
Depuis le jour que tu t’es trouvé devant le Seigneur ton Dieu à Horeb, quand le Seigneur me parla, disant: Assemble auprès de moi le peuple, afin qu’ils entendent mes paroles, et qu’ils apprennent à me craindre tout le temps qu’ils vivront sur la terre, et qu’ils instruisent leurs enfants.
11 Mlisogea karibu na mkasimama chini ya mlima wakati ulipowaka moto mpaka mbinguni juu, pamoja na mawingu meusi na giza nene.
Et vous vous approchâtes du pied de la montagne, qui brûlait jusqu’au ciel; et il y avait sur elle des ténèbres, un nuage et une obscurité.
12 Ndipo Bwana alipozungumza nanyi kutoka moto. Mkasikia sauti ya maneno lakini hamkuona umbo, kulikuwa na sauti tu.
Et le Seigneur vous parla du milieu du feu. Vous entendîtes la voix de ses paroles, mais de forme, vous n’en vîtes absolument point.
13 Aliwatangazia Agano lake na Amri Kumi, ambazo aliwaamuru mzifuate, kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe.
Il vous fit connaître son alliance, qu’il vous ordonna d’accomplir, et les dix paroles qu’il écrivit sur deux tables de pierre.
14 Naye Bwana alinielekeza wakati huo kuwafundisha ninyi sheria na amri ambazo mnapaswa kuzifuata katika nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki.
Et à moi, il me commanda, en ce temps-là, de vous enseigner des cérémonies et des ordonnances que vous deviez accomplir dans la terre que vous allez posséder.
15 Hamkuona umbo la aina yoyote siku ambayo Bwana alizungumza nanyi kule Horebu kutoka kwenye moto. Kwa hiyo mjihadhari kwa uangalifu sana,
Gardez donc soigneusement vos âmes. Vous n’avez vu aucune représentation au jour que le Seigneur vous parla à Horeb, du milieu du feu;
16 ili msije mkajichafua na kujitengenezea sanamu au kinyago chenye umbo lolote kama la mwanaume au mwanamke,
De peur que, séduits, vous ne vous fassiez quelque représentation taillée au ciseau, ou bien quelque image d’homme ou de femme;
17 au kama mnyama aliye juu ya nchi au ndege yeyote arukaye angani,
Quelque représentation de toutes les bêtes qui sont sur la terre, ou des oiseaux qui volent sous le ciel,
18 au kama kiumbe kitambaacho juu ya ardhi au samaki yeyote aliye ndani ya maji.
Et des reptiles qui se meuvent sur la terre, ou des poissons qui sous la terre demeurent dans les eaux;
19 Na utazamapo juu angani na ukaliona jua, mwezi na nyota na vyote vinavyoipamba mbingu, usije ukashawishiwa kuviinamia na kuviabudu vile ambavyo Bwana Mungu wenu alivyogawia mataifa yote chini ya mbingu.
De peur que, les yeux levés au ciel, tu ne voies le soleil, la lune et tous les astres du ciel, et que, séduit par l’erreur, tu ne les adores, et tu n’offres un culte à des choses que le Seigneur ton Dieu a créées pour servir à toutes les nations qui sont sous le ciel.
20 Lakini kwenu ninyi, Bwana amewatoa kutoka kwenye tanuru ya kuyeyushia chuma, katika Misri kuwa watu wa urithi wake kama mlivyo sasa.
Pour vous, le Seigneur vous a tirés et ramenés de la fournaise de fer de l’Egypte, pour avoir un peuple héréditaire, comme il est au présent jour.
21 Bwana alinikasirikia kwa sababu yenu na akaapa kwamba sitavuka Yordani kuingia katika nchi nzuri Bwana Mungu wenu anayowapa kuwa urithi wenu.
Et le Seigneur s’est irrité contre moi, à cause de vos discours, et il a juré que je ne passerai pas le Jourdain, et que je n’entrerai pas dans la terre excellente qu’il va vous donner.
22 Nitakufa katika nchi hii; sitavuka Yordani, lakini ninyi ni karibu mvuke mkaimiliki ile nchi nzuri.
Voici donc que je meurs en ce pays; je ne passerai point le Jourdain; vous, vous le passerez, et vous posséderez cette belle terre.
23 Jihadharini msilisahau Agano la Bwana Mungu wenu lile alilofanya nanyi; msijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote ambacho Bwana Mungu wenu amewakataza.
Prends garde d’oublier jamais l’alliance du Seigneur ton Dieu, qu’il a établie avec toi, et de te faire quelque représentation taillée au ciseau des choses dont le Seigneur a défendu d’en faire,
24 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni moto ulao, Mungu mwenye wivu.
Parce que le Seigneur ton Dieu est un feu consumant, un Dieu jaloux.
25 Baada ya kuwa na watoto na wajukuu na kuishi katika nchi hiyo siku nyingi, tena kama mkijichafua na kutengeneza sanamu ya aina yoyote, mkifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wenu na kumfanya awe na hasira,
Si vous engendrez des enfants et des petits-enfants, et que vous demeuriez dans cette terre, et que, séduits, vous fassiez quelque représentation, commettant le mal devant le Seigneur votre Dieu, en sorte que vous le provoquiez au courroux,
26 ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yenu siku hii kwamba mtaangamia mara moja kutoka nchi ile ambayo mnavuka Yordani kuimiliki. Hamtaishi kule kwa muda mrefu bali kwa hakika mtaangamizwa.
J’invoque à témoin aujourd’hui le ciel et la terre que bientôt vous serez exterminés de la terre, que, le Jourdain passé, vous allez posséder; vous n’y habiterez pas longtemps, mais le Seigneur vous détruira,
27 Bwana atawatawanya miongoni mwa mataifa, na ni wachache wenu tu watakaosalia miongoni mwa mataifa hayo ambayo Bwana atawafukuzia.
Et vous dispersera dans tous les peuples, et vous resterez en petit nombre parmi les nations, chez lesquelles le Seigneur doit vous conduire.
28 Huko mtaabudu miungu ya miti na mawe iliyotengenezwa na watu, ambayo haiwezi kuona au kusikia wala kula au kunusa.
Et là vous servirez des dieux qui ont été fabriqués par la main des hommes, du bois et de la pierre, qui ne voient, ni n’entendent, ni ne mangent, ni ne flairent.
29 Lakini kama mtamtafuta Bwana Mungu wenu, mtampata; kama mtamtafuta kwa moyo wenu wote na kwa roho yote.
Mais, lorsque tu chercheras là le Seigneur ton Dieu, tu le trouveras, si cependant c’est de tout ton cœur que tu le cherches, et dans toute l’affliction de ton âme.
30 Wakati mnapokuwa katika dhiki, nayo mambo haya yote yamewatokea siku hizo, ndipo mtamrudia Bwana Mungu wenu na kumtii.
Après que te seront arrivées toutes les choses qui ont été prédites, tu reviendras, dans le dernier temps, au Seigneur ton Dieu, et tu écouteras sa voix,
31 Kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu mwenye huruma, hatawaacha au kuwaangamiza wala kusahau Agano alilofanya na baba zenu, alilowathibitishia kwa kiapo.
Parce que c’est un Dieu miséricordieux, le Seigneur ton Dieu; il ne t’abandonnera point, et il ne te détruira pas entièrement, et il n’oubliera pas l’alliance qu’il a jurée à tes pères.
32 Sasa uliza kuhusu siku za zamani, zamani kabla ya wakati wako, tangu siku ile Mungu alipomuumba mtu juu ya nchi, uliza kutoka mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho mwingine wa mbingu. Je, kumepata kutokea jambo jingine lililo kubwa kama hili, au kuna jambo jingine kama hilo limepata kusikiwa?
Demande aux jours anciens qui ont été avant toi, depuis le jour que Dieu a créé l’homme sur la terre, depuis une extrémité du ciel jusqu’à l’autre extrémité, s’il a été fait jamais une chose semblable, ou si jamais il a été connu
33 Je, kuna watu wengine wowote waliosikia sauti ya Mungu ikizungumza kwenye moto, kama mlivyosikia, nao wakaishi?
Qu’un peuple ait entendu la voix de Dieu, parlant du milieu du feu, comme tu l’as entendue, en conservant la vie;
34 Je, kuna mungu yeyote amepata kujaribu mwenyewe kuchukua taifa moja kutoka taifa lingine, kwa mapigo, kwa ishara za miujiza na maajabu, kwa vita, kwa mkono wenye nguvu na mkono ulionyooshwa au kwa matendo makuu ya kutisha, kama yale ambayo Bwana Mungu wenu aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu?
Si Dieu a entrepris devenir et de prendre pour lui une nation au milieu des nations, par des épreuves, des signes et des prodiges, par la guerre, par une main forte, un bras étendu et d’horribles visions, selon tout ce qu’a fait pour vous le Seigneur votre Dieu dans l’Egypte, tes yeux le voyant,
35 Mlionyeshwa mambo haya ili mpate kujua kuwa Bwana ndiye Mungu; hakuna mwingine ila yeye.
Afin que tu susses que c’est le Seigneur lui-même qui est Dieu, et qu’il n’en est pas d’autre que lui.
36 Kutoka mbinguni amewasikizisha sauti yake ili kuwaadilisha. Hapa duniani aliwaonyesha moto wake mkubwa, nanyi mlisikia maneno yake kutoka kwenye ule moto.
Du haut du ciel il t’a fait entendre sa voix pour l’instruire, et sur la terre il t’a montré son feu très ardent, et tu as entendu ses paroles qui sortaient du milieu du feu
37 Kwa sababu aliwapenda baba zenu na alichagua wazao wao baada yao, aliwatoa katika nchi ya Misri kwa Uwepo wake na kwa uwezo wake mkuu,
Parce qu’il a aimé tes pères, et qu’il a choisi leur postérité après eux; et il t’a retiré de l’Egypte, te précédant avec sa grande puissance,
38 aliwafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi na kuwaleta ninyi katika nchi yao na akawapa ninyi kuwa urithi wenu, kama ilivyo leo.
Pour détruire à ton entrée des nations très grandes et plus fortes que loi, et pour l’introduire, et te donner leur terre en possession, comme tu vois au présent jour.
39 Kubalini na mweke moyoni leo kuwa Bwana ndiye Mungu mbinguni juu na duniani chini. Hakuna mwingine.
Sache donc aujourd’hui, et pense en ton cœur, que c’est le Seigneur lui-même qui est Dieu dans le ciel en haut, et sur la terre en bas, et qu’il n’en est pas d’autre.
40 Mshike amri na maagizo yake ninayowapa leo, ili mpate kufanikiwa ninyi na watoto wenu baada yenu, na mpate kuishi maisha marefu katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu siku zote.
Garde ses préceptes et ses commandements, que moi, je te prescris, afin que bien l’arrivé, à toi et à tes fils après toi, et que tu demeures longtemps sur la terre que le Seigneur ton Dieu va te donner.
41 Kisha Mose akatenga miji mitatu mashariki ya Yordani,
Alors Moïse sépara trois villes au-delà du Jourdain vers la partie orientale,
42 ambayo mtu yeyote aliyemuua mtu angeweza kukimbilia ikiwa amemuua jirani yake bila kukusudia na bila kuwa na chuki naye siku zilizopita. Angeweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake.
Afin que s’y réfugie celui qui sans le vouloir aura tué son prochain, et qui n’aura pas été son ennemi un ou deux jours auparavant, et qu’il puisse se retirer dans une de ces villes:
43 Miji hiyo ilikuwa: Bezeri katika tambarare ya jangwa kwa ajili ya Wareubeni; Ramothi katika nchi ya Gileadi kwa ajili ya Wagadi; nao mji wa Golani katika nchi ya Bashani kwa ajili ya Wamanase.
Bosor dans le désert, qui est située dans la plate campagne de la tribu de Ruben; Ramolli en Galaad, qui est dans la tribu de Gad, et Golan en Basan, qui est dans la tribu de Manassé.
44 Hii ndiyo sheria Mose aliyoweka mbele ya Waisraeli.
Telle est la loi que Moïse exposa devant les enfants d’Israël;
45 Haya ndiyo masharti, amri na sheria Mose aliyowapa wana wa Israeli wakati walitoka Misri,
Et telles sont les lois, les cérémonies et les ordonnances qu’il annonça aux enfants d’Israël, quand ils furent sortis de l’Egypte,
46 nao walikuwa katika bonde karibu na Beth-Peori mashariki ya Yordani, katika nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, naye alishindwa na Mose na Waisraeli walipokuja toka Misri.
Au delà du Jourdain dans la vallée, contre le temple de Phogor dans la terre de Séhon, roi de l’Amorrhéen, qui habita à Hésébon, et que battit Moïse. Les enfants d Israël aussi, sortis de l’Egypte,
47 Waliimiliki nchi yake na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, wafalme wawili Waamori waliotawala mashariki ya Yordani.
Possédèrent sa terre, et la terre d’Og, roi de Basan, deux rois des Amorrhéens qui étaient au-delà du Jourdain, vers le levant,
48 Nchi hii ilienea kutoka Aroeri ukingoni mwa Bonde la Arnoni mpaka Mlima Sioni (yaani Hermoni),
Depuis Aroër qui est sur le bord du torrent d’Arnon, jusqu’à la montagne de Sion, qui est appelée aussi Hermon,
49 pamoja na eneo lote la Araba mashariki ya Yordani, na kuenea mpaka Bahari ya Araba kwenye miteremko ya Pisga.
Toute la plaine au-delà du Jourdain, vers la partie orientale, jusqu’à la mer du désert, et jusqu’au pied de la montagne de Phasga.