< Torati 4 >

1 Sikia sasa, ee Israeli, amri na sheria nitakazokufundisha wewe. Zifuate ili upate kuishi na uingie kuimiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zako anawapa.
Now, therefore, O Israel, hearken thou unto the statutes, and unto the regulations, which, I, am teaching you, to do [them], —to the end ye may live and enter and possess the land, which, Yahweh, the God of your fathers, is giving unto you.
2 Usiongeze wala usipunguze chochote ninachowaamuru ninyi, ila myashike maagizo ya Bwana Mungu wenu ambayo nawapa.
Ye shall not add unto the word which, I, am commanding you, neither shall ye take away therefrom, —that ye may keep the commandments of Yahweh your God, which, I, am commanding you.
3 Mliona kwa macho yenu wenyewe kile Bwana alichokifanya kule Baal-Peori. Bwana Mungu wenu aliwaangamiza kutoka miongoni mwenu kila mmoja aliyemfuata Baali wa Peori,
Yours are the eyes, that have seen what Yahweh did in Baal-peor, for every man who went after Baal-peor, did Yahweh thy God destroy out of thy midst;
4 lakini ninyi nyote mlioshikamana na Bwana kwa uthabiti, Mungu wenu, mko hai mpaka leo.
but, ye who kept on cleaving unto Yahweh your God, alive, are ye all to-day.
5 Tazama, nimewafundisha amri na sheria kama Bwana Mungu wangu alivyoniamuru mimi, ili mzifuate katika nchi mnayoiingia kuimiliki.
See! I have taught you statutes, and regulations, as Yahweh my God commanded me, —that ye should do so, in the midst of the land whereinto ye are entering to possess it.
6 Zishikeni kwa uangalifu, kwa kuwa hii itaonyesha hekima na ufahamu wenu kwa mataifa, ambayo yatasikia kuhusu amri zote hizi, nao watasema, “Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na ufahamu.”
Therefore shall ye observe, and do [them], for that, will be your wisdom, and discernment, in the eyes of the peoples, —who will hear all these statutes, and will say—Nevertheless, a people wise and discerning, is this great nation.
7 Ni taifa gani jingine lililo kubwa kiasi cha kuwa na miungu yao iliyo karibu nao kama Bwana Mungu wetu alivyo karibu nasi wakati wowote tunapomwomba?
For what great nation is there which hath gods nigh unto it, —like Yahweh our God, whensoever we have cried out unto him.
8 Nalo ni taifa gani jingine lililo kubwa hivi lenye kuwa na amri na sheria za haki kama hizi ninazoweka mbele yenu leo?
Or what great nation which hath righteous statutes and regulations, like all this law, which, I, am setting before you to-day?
9 Mwe waangalifu, na makini ili msije mkasahau mambo ambayo mliyaona kwa macho yenu, wala kuyaacha yaondoke moyoni mwenu siku zote za uhai wenu. Mwafundishe hayo watoto wenu na watoto wao baada yao.
Only take thou heed to thyself and keep thy soul diligently, so that thou forget not the things which thine own eyes have seen, and so that they go not out of thy heart, all the days of thy life, —but thou shalt make them known unto thy sons and unto thy sons’ sons: —
10 Kumbuka siku uliyosimama mbele za Bwana Mungu wako kule Horebu, wakati aliponiambia, “Wakutanishe watu mbele yangu wasikie maneno yangu ili kwamba waweze kujifunza kuniheshimu kwa muda wote watakaoishi katika nchi, nao waweze kuwafundisha watoto wao maneno hayo.”
What day thou didst stand before Yahweh thy God, in Horeb, when Yahweh said unto me, Gather unto me the people, that I may let them hear my words, —which they must learn that they may revere me all the days which they are living upon the soil, their children also, must they teach.
11 Mlisogea karibu na mkasimama chini ya mlima wakati ulipowaka moto mpaka mbinguni juu, pamoja na mawingu meusi na giza nene.
So ye drew near and stood, under the mountain. Now, the mountain, was burning with fire, up to the midst of the heavens, —darkness, cloud, and thick gloom.
12 Ndipo Bwana alipozungumza nanyi kutoka moto. Mkasikia sauti ya maneno lakini hamkuona umbo, kulikuwa na sauti tu.
Then spake Yahweh unto you out of the midst of the fire, —a voice of words, ye were hearing, no form, were ye seeing, there was only a voice.
13 Aliwatangazia Agano lake na Amri Kumi, ambazo aliwaamuru mzifuate, kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe.
Then declared he unto you his covenant which he commanded you to do, the ten words, —and wrote them upon two tables of stone.
14 Naye Bwana alinielekeza wakati huo kuwafundisha ninyi sheria na amri ambazo mnapaswa kuzifuata katika nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki.
And unto me, gave Yahweh command, at that time, to teach you statutes and regulations, —that ye should do them, in the land whereinto ye are passing over to possess it.
15 Hamkuona umbo la aina yoyote siku ambayo Bwana alizungumza nanyi kule Horebu kutoka kwenye moto. Kwa hiyo mjihadhari kwa uangalifu sana,
Ye must take diligent heed, therefore unto your own souls, for ye saw no manner of form, on the day Yahweh spake unto you in Horeb out of the midst of the fire;
16 ili msije mkajichafua na kujitengenezea sanamu au kinyago chenye umbo lolote kama la mwanaume au mwanamke,
lest ye should break faith, and make you an image, a form of any likeness, —a model of male or female;
17 au kama mnyama aliye juu ya nchi au ndege yeyote arukaye angani,
a model of any beast that is in the earth, —a model of any winged bird, that flieth in the heavens;
18 au kama kiumbe kitambaacho juu ya ardhi au samaki yeyote aliye ndani ya maji.
a model of any thing that creepeth on the ground, —a model of any fish that is in the waters beneath the earth;
19 Na utazamapo juu angani na ukaliona jua, mwezi na nyota na vyote vinavyoipamba mbingu, usije ukashawishiwa kuviinamia na kuviabudu vile ambavyo Bwana Mungu wenu alivyogawia mataifa yote chini ya mbingu.
or lest thou shouldest lift up thine eyes towards the heavens and see the sun and the moon, and the stars—all the host of the heavens, and shouldest be seduced, and shouldest bow thyself down to them and he led to serve them, —the which Yahweh thy God hath assigned unto all the peoples under all the heavens;
20 Lakini kwenu ninyi, Bwana amewatoa kutoka kwenye tanuru ya kuyeyushia chuma, katika Misri kuwa watu wa urithi wake kama mlivyo sasa.
whereas you, hath Yahweh taken, and brought you forth out of a smelting-pot of iron, out of Egypt, —that ye might become his own inherited people as at this day.
21 Bwana alinikasirikia kwa sababu yenu na akaapa kwamba sitavuka Yordani kuingia katika nchi nzuri Bwana Mungu wenu anayowapa kuwa urithi wenu.
But, Yahweh shewed himself angry with me, for your sakes, —and sware that I should not pass over the Jordan, and that I should not enter into the good land, which, Yahweh thy God, is giving unto thee as an inheritance;
22 Nitakufa katika nchi hii; sitavuka Yordani, lakini ninyi ni karibu mvuke mkaimiliki ile nchi nzuri.
for, I, am about to die in this land, I am not to pass over the Jordan, —but, ye, are to pass over, and possess this good land.
23 Jihadharini msilisahau Agano la Bwana Mungu wenu lile alilofanya nanyi; msijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote ambacho Bwana Mungu wenu amewakataza.
Take heed to yourselves lest ye forget the covenant of Yahweh your God, which he hath solemnised with you, —and so make for yourselves an image, the form of anything, the which Yahweh thy God hath forbidden thee;
24 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni moto ulao, Mungu mwenye wivu.
seeing that as for Yahweh thy God, a consuming fire, he is, —a jealous GOD.
25 Baada ya kuwa na watoto na wajukuu na kuishi katika nchi hiyo siku nyingi, tena kama mkijichafua na kutengeneza sanamu ya aina yoyote, mkifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wenu na kumfanya awe na hasira,
When thou shalt beget sons, and sons’ sons, and become careless in the land and break faith and make an image the form of any thing, and shalt do the thing that is wicked in the eyes of Yahweh thy God provoking him to anger,
26 ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yenu siku hii kwamba mtaangamia mara moja kutoka nchi ile ambayo mnavuka Yordani kuimiliki. Hamtaishi kule kwa muda mrefu bali kwa hakika mtaangamizwa.
I take both the heavens and the earth to witness against you to-day, that ye shall, perish, speedily, from off the land which ye are passing over the Jordan to possess, —ye shall not prolong your days thereupon; for, ye shall surely be laid waste;
27 Bwana atawatawanya miongoni mwa mataifa, na ni wachache wenu tu watakaosalia miongoni mwa mataifa hayo ambayo Bwana atawafukuzia.
and Yahweh will scatter you among the peoples, —and ye shall have left remaining of you men easily counted, among the nations whither Yahweh will drive you;
28 Huko mtaabudu miungu ya miti na mawe iliyotengenezwa na watu, ambayo haiwezi kuona au kusikia wala kula au kunusa.
and ye will serve there gods made by the hands of man, —wood or stone, which neither see nor hear nor eat nor smell.
29 Lakini kama mtamtafuta Bwana Mungu wenu, mtampata; kama mtamtafuta kwa moyo wenu wote na kwa roho yote.
If thou shalt seek from thence, Yahweh thy God, then shalt thou find him, —when thou shalt search after him with all thy heart, and with all thy soul.
30 Wakati mnapokuwa katika dhiki, nayo mambo haya yote yamewatokea siku hizo, ndipo mtamrudia Bwana Mungu wenu na kumtii.
In thy distress, when all these things have found thee out—in the afterpart of the days, thou wilt return unto Yahweh thy God, and wilt hearken to his voice.
31 Kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu mwenye huruma, hatawaacha au kuwaangamiza wala kusahau Agano alilofanya na baba zenu, alilowathibitishia kwa kiapo.
For, a GOD of compassion, is Yahweh thy God, he will not forsake thee neither will he destroy thee, —nor forget the covenant of thy fathers which he sware unto them.
32 Sasa uliza kuhusu siku za zamani, zamani kabla ya wakati wako, tangu siku ile Mungu alipomuumba mtu juu ya nchi, uliza kutoka mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho mwingine wa mbingu. Je, kumepata kutokea jambo jingine lililo kubwa kama hili, au kuna jambo jingine kama hilo limepata kusikiwa?
For ask, I pray you, of the former days which were before thee, even from the day when God created man upon the earth, yea from one end of the heavens even to the other end of the heavens, —whether aught was ever brought to pass, like this great thing, or was ever heard of like it:
33 Je, kuna watu wengine wowote waliosikia sauti ya Mungu ikizungumza kwenye moto, kama mlivyosikia, nao wakaishi?
Did a people ever hear the voice of a god speaking out of the midst of fire, as, thou, didst hear, and yet live?
34 Je, kuna mungu yeyote amepata kujaribu mwenyewe kuchukua taifa moja kutoka taifa lingine, kwa mapigo, kwa ishara za miujiza na maajabu, kwa vita, kwa mkono wenye nguvu na mkono ulionyooshwa au kwa matendo makuu ya kutisha, kama yale ambayo Bwana Mungu wenu aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu?
Or did a god ever make trial of entering in to take unto him a nation out of the midst of a nation, by provings, by signs and by wonders and by fighting, and by a firm hand and by a stretched-out arm, and by great terrors, —according to all that Yahweh your God did for you in Egypt, before your eyes?
35 Mlionyeshwa mambo haya ili mpate kujua kuwa Bwana ndiye Mungu; hakuna mwingine ila yeye.
Thou, wast allowed to see that thou mightest know, that Yahweh, he is God, there is none other than he alone.
36 Kutoka mbinguni amewasikizisha sauti yake ili kuwaadilisha. Hapa duniani aliwaonyesha moto wake mkubwa, nanyi mlisikia maneno yake kutoka kwenye ule moto.
Out of the heavens, he let thee hear his voice to instruct thee, —and, upon the earth, he let thee see his great fire, and his own words, thou didst hear out of the midst of the fire.
37 Kwa sababu aliwapenda baba zenu na alichagua wazao wao baada yao, aliwatoa katika nchi ya Misri kwa Uwepo wake na kwa uwezo wake mkuu,
And because that he loved thy fathers, therefore chose he his seed after him, —and brought thee forth with his presence with his great might, out of Egypt;
38 aliwafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi na kuwaleta ninyi katika nchi yao na akawapa ninyi kuwa urithi wenu, kama ilivyo leo.
to dispossess nations, greater and stronger than thou from before thee, —to bring thee in. to give unto thee their land for an inheritance: As at this day.
39 Kubalini na mweke moyoni leo kuwa Bwana ndiye Mungu mbinguni juu na duniani chini. Hakuna mwingine.
So then thou must consider to-day, and bring it back to thy heart, that, Yahweh, he is God in the heavens above and upon the earth beneath, —there is none other.
40 Mshike amri na maagizo yake ninayowapa leo, ili mpate kufanikiwa ninyi na watoto wenu baada yenu, na mpate kuishi maisha marefu katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu siku zote.
So shalt thou keep his statutes and his commandments which, I, am commanding thee to-day, that it may go well with thee, and with thy sons after thee, —and to the end thou mayest prolong thy days upon the soil, which Yahweh thy God, is giving thee, all the days.
41 Kisha Mose akatenga miji mitatu mashariki ya Yordani,
Then, did Moses set apart three cities, over the Jordan, —towards the rising of the sun:
42 ambayo mtu yeyote aliyemuua mtu angeweza kukimbilia ikiwa amemuua jirani yake bila kukusudia na bila kuwa na chuki naye siku zilizopita. Angeweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake.
that the manslayer might flee thither who should slay his neighbour unawares, he, not having hated him, aforetime, —and might flee unto one of these cities, and live:
43 Miji hiyo ilikuwa: Bezeri katika tambarare ya jangwa kwa ajili ya Wareubeni; Ramothi katika nchi ya Gileadi kwa ajili ya Wagadi; nao mji wa Golani katika nchi ya Bashani kwa ajili ya Wamanase.
namely Bezer, in the desert of the table-land, for the Reubenites, —and Ramoth in Gilead for the Gadites, and Golan in Bashan, for the Manassites.
44 Hii ndiyo sheria Mose aliyoweka mbele ya Waisraeli.
This, then is the law which Moses set before the sons of Israel:
45 Haya ndiyo masharti, amri na sheria Mose aliyowapa wana wa Israeli wakati walitoka Misri,
These, are the testimonies, and the statutes and the regulations, —which Moses spake unto the sons of Israel when they came forth out of Egypt:
46 nao walikuwa katika bonde karibu na Beth-Peori mashariki ya Yordani, katika nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, naye alishindwa na Mose na Waisraeli walipokuja toka Misri.
over the Jordan in the valley over against Beth-peor, in the land of Sihon king of the Amorites, who dwelt in Heshbon, —whom Moses and the sons of Israel smote, when they came forth out of Egypt:
47 Waliimiliki nchi yake na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, wafalme wawili Waamori waliotawala mashariki ya Yordani.
so they took possession of his land, and the land of Og king of Bashan the two kings of the Amorites, who were over the Jordan, —towards the rising of the sun;
48 Nchi hii ilienea kutoka Aroeri ukingoni mwa Bonde la Arnoni mpaka Mlima Sioni (yaani Hermoni),
from Aroer which is on the edge of the ravine of Arnon, even unto Mount Sion, the same, is Hermon;
49 pamoja na eneo lote la Araba mashariki ya Yordani, na kuenea mpaka Bahari ya Araba kwenye miteremko ya Pisga.
and all the waste plain over the Jordan, towards sunrise, even unto the sea of the waste plain, —under the slopes of the Pisgah.

< Torati 4 >