< Torati 4 >

1 Sikia sasa, ee Israeli, amri na sheria nitakazokufundisha wewe. Zifuate ili upate kuishi na uingie kuimiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zako anawapa.
Now therefore listen, O Israel, to the statutes and to the judgments, which I teach you, for to do them, that you may live, and go in and possess the land which the LORD God of your fathers gives you.
2 Usiongeze wala usipunguze chochote ninachowaamuru ninyi, ila myashike maagizo ya Bwana Mungu wenu ambayo nawapa.
You shall not add to the word which I command you, neither shall you diminish anything from it, that you may keep the commandments of the LORD your God which I command you.
3 Mliona kwa macho yenu wenyewe kile Bwana alichokifanya kule Baal-Peori. Bwana Mungu wenu aliwaangamiza kutoka miongoni mwenu kila mmoja aliyemfuata Baali wa Peori,
Your eyes have seen what the LORD did because of Baalpeor: for all the men that followed Baalpeor, the LORD your God has destroyed them from among you.
4 lakini ninyi nyote mlioshikamana na Bwana kwa uthabiti, Mungu wenu, mko hai mpaka leo.
But you that did join to the LORD your God are alive every one of you this day.
5 Tazama, nimewafundisha amri na sheria kama Bwana Mungu wangu alivyoniamuru mimi, ili mzifuate katika nchi mnayoiingia kuimiliki.
Behold, I have taught you statutes and judgments, even as the LORD my God commanded me, that you should do so in the land where you go to possess it.
6 Zishikeni kwa uangalifu, kwa kuwa hii itaonyesha hekima na ufahamu wenu kwa mataifa, ambayo yatasikia kuhusu amri zote hizi, nao watasema, “Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na ufahamu.”
Keep therefore and do them; for this is your wisdom and your understanding in the sight of the nations, which shall hear all these statutes, and say, Surely this great nation is a wise and understanding people.
7 Ni taifa gani jingine lililo kubwa kiasi cha kuwa na miungu yao iliyo karibu nao kama Bwana Mungu wetu alivyo karibu nasi wakati wowote tunapomwomba?
For what nation is there so great, who has God so near to them, as the LORD our God is in all things that we call on him for?
8 Nalo ni taifa gani jingine lililo kubwa hivi lenye kuwa na amri na sheria za haki kama hizi ninazoweka mbele yenu leo?
And what nation is there so great, that has statutes and judgments so righteous as all this law, which I set before you this day?
9 Mwe waangalifu, na makini ili msije mkasahau mambo ambayo mliyaona kwa macho yenu, wala kuyaacha yaondoke moyoni mwenu siku zote za uhai wenu. Mwafundishe hayo watoto wenu na watoto wao baada yao.
Only take heed to yourself, and keep your soul diligently, lest you forget the things which your eyes have seen, and lest they depart from your heart all the days of your life: but teach them your sons, and your sons’ sons;
10 Kumbuka siku uliyosimama mbele za Bwana Mungu wako kule Horebu, wakati aliponiambia, “Wakutanishe watu mbele yangu wasikie maneno yangu ili kwamba waweze kujifunza kuniheshimu kwa muda wote watakaoishi katika nchi, nao waweze kuwafundisha watoto wao maneno hayo.”
Specially the day that you stood before the LORD your God in Horeb, when the LORD said to me, Gather me the people together, and I will make them hear my words, that they may learn to fear me all the days that they shall live on the earth, and that they may teach their children.
11 Mlisogea karibu na mkasimama chini ya mlima wakati ulipowaka moto mpaka mbinguni juu, pamoja na mawingu meusi na giza nene.
And you came near and stood under the mountain; and the mountain burned with fire to the middle of heaven, with darkness, clouds, and thick darkness.
12 Ndipo Bwana alipozungumza nanyi kutoka moto. Mkasikia sauti ya maneno lakini hamkuona umbo, kulikuwa na sauti tu.
And the LORD spoke to you out of the middle of the fire: you heard the voice of the words, but saw no similitude; only you heard a voice.
13 Aliwatangazia Agano lake na Amri Kumi, ambazo aliwaamuru mzifuate, kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe.
And he declared to you his covenant, which he commanded you to perform, even ten commandments; and he wrote them on two tables of stone.
14 Naye Bwana alinielekeza wakati huo kuwafundisha ninyi sheria na amri ambazo mnapaswa kuzifuata katika nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki.
And the LORD commanded me at that time to teach you statutes and judgments, that you might do them in the land where you go over to possess it.
15 Hamkuona umbo la aina yoyote siku ambayo Bwana alizungumza nanyi kule Horebu kutoka kwenye moto. Kwa hiyo mjihadhari kwa uangalifu sana,
Take you therefore good heed to yourselves; for you saw no manner of similitude on the day that the LORD spoke to you in Horeb out of the middle of the fire:
16 ili msije mkajichafua na kujitengenezea sanamu au kinyago chenye umbo lolote kama la mwanaume au mwanamke,
Lest you corrupt yourselves, and make you a graven image, the similitude of any figure, the likeness of male or female,
17 au kama mnyama aliye juu ya nchi au ndege yeyote arukaye angani,
The likeness of any beast that is on the earth, the likeness of any winged fowl that flies in the air,
18 au kama kiumbe kitambaacho juu ya ardhi au samaki yeyote aliye ndani ya maji.
The likeness of any thing that creeps on the ground, the likeness of any fish that is in the waters beneath the earth:
19 Na utazamapo juu angani na ukaliona jua, mwezi na nyota na vyote vinavyoipamba mbingu, usije ukashawishiwa kuviinamia na kuviabudu vile ambavyo Bwana Mungu wenu alivyogawia mataifa yote chini ya mbingu.
And lest you lift up your eyes to heaven, and when you see the sun, and the moon, and the stars, even all the host of heaven, should be driven to worship them, and serve them, which the LORD your God has divided to all nations under the whole heaven.
20 Lakini kwenu ninyi, Bwana amewatoa kutoka kwenye tanuru ya kuyeyushia chuma, katika Misri kuwa watu wa urithi wake kama mlivyo sasa.
But the LORD has taken you, and brought you forth out of the iron furnace, even out of Egypt, to be to him a people of inheritance, as you are this day.
21 Bwana alinikasirikia kwa sababu yenu na akaapa kwamba sitavuka Yordani kuingia katika nchi nzuri Bwana Mungu wenu anayowapa kuwa urithi wenu.
Furthermore the LORD was angry with me for your sakes, and swore that I should not go over Jordan, and that I should not go in to that good land, which the LORD your God gives you for an inheritance:
22 Nitakufa katika nchi hii; sitavuka Yordani, lakini ninyi ni karibu mvuke mkaimiliki ile nchi nzuri.
But I must die in this land, I must not go over Jordan: but you shall go over, and possess that good land.
23 Jihadharini msilisahau Agano la Bwana Mungu wenu lile alilofanya nanyi; msijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote ambacho Bwana Mungu wenu amewakataza.
Take heed to yourselves, lest you forget the covenant of the LORD your God, which he made with you, and make you a graven image, or the likeness of any thing, which the LORD your God has forbidden you.
24 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni moto ulao, Mungu mwenye wivu.
For the LORD your God is a consuming fire, even a jealous God.
25 Baada ya kuwa na watoto na wajukuu na kuishi katika nchi hiyo siku nyingi, tena kama mkijichafua na kutengeneza sanamu ya aina yoyote, mkifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wenu na kumfanya awe na hasira,
When you shall beget children, and children’s children, and you shall have remained long in the land, and shall corrupt yourselves, and make a graven image, or the likeness of any thing, and shall do evil in the sight of the LORD your God, to provoke him to anger:
26 ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yenu siku hii kwamba mtaangamia mara moja kutoka nchi ile ambayo mnavuka Yordani kuimiliki. Hamtaishi kule kwa muda mrefu bali kwa hakika mtaangamizwa.
I call heaven and earth to witness against you this day, that you shall soon utterly perish from off the land where you go over Jordan to possess it; you shall not prolong your days on it, but shall utterly be destroyed.
27 Bwana atawatawanya miongoni mwa mataifa, na ni wachache wenu tu watakaosalia miongoni mwa mataifa hayo ambayo Bwana atawafukuzia.
And the LORD shall scatter you among the nations, and you shall be left few in number among the heathen, where the LORD shall lead you.
28 Huko mtaabudu miungu ya miti na mawe iliyotengenezwa na watu, ambayo haiwezi kuona au kusikia wala kula au kunusa.
And there you shall serve gods, the work of men’s hands, wood and stone, which neither see, nor hear, nor eat, nor smell.
29 Lakini kama mtamtafuta Bwana Mungu wenu, mtampata; kama mtamtafuta kwa moyo wenu wote na kwa roho yote.
But if from there you shall seek the LORD your God, you shall find him, if you seek him with all your heart and with all your soul.
30 Wakati mnapokuwa katika dhiki, nayo mambo haya yote yamewatokea siku hizo, ndipo mtamrudia Bwana Mungu wenu na kumtii.
When you are in tribulation, and all these things are come on you, even in the latter days, if you turn to the LORD your God, and shall be obedient to his voice;
31 Kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu mwenye huruma, hatawaacha au kuwaangamiza wala kusahau Agano alilofanya na baba zenu, alilowathibitishia kwa kiapo.
(For the LORD your God is a merciful God; ) he will not forsake you, neither destroy you, nor forget the covenant of your fathers which he swore to them.
32 Sasa uliza kuhusu siku za zamani, zamani kabla ya wakati wako, tangu siku ile Mungu alipomuumba mtu juu ya nchi, uliza kutoka mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho mwingine wa mbingu. Je, kumepata kutokea jambo jingine lililo kubwa kama hili, au kuna jambo jingine kama hilo limepata kusikiwa?
For ask now of the days that are past, which were before you, since the day that God created man on the earth, and ask from the one side of heaven to the other, whether there has been any such thing as this great thing is, or has been heard like it?
33 Je, kuna watu wengine wowote waliosikia sauti ya Mungu ikizungumza kwenye moto, kama mlivyosikia, nao wakaishi?
Did ever people hear the voice of God speaking out of the middle of the fire, as you have heard, and live?
34 Je, kuna mungu yeyote amepata kujaribu mwenyewe kuchukua taifa moja kutoka taifa lingine, kwa mapigo, kwa ishara za miujiza na maajabu, kwa vita, kwa mkono wenye nguvu na mkono ulionyooshwa au kwa matendo makuu ya kutisha, kama yale ambayo Bwana Mungu wenu aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu?
Or has God assayed to go and take him a nation from the middle of another nation, by temptations, by signs, and by wonders, and by war, and by a mighty hand, and by a stretched out arm, and by great terrors, according to all that the LORD your God did for you in Egypt before your eyes?
35 Mlionyeshwa mambo haya ili mpate kujua kuwa Bwana ndiye Mungu; hakuna mwingine ila yeye.
To you it was showed, that you might know that the LORD he is God; there is none else beside him.
36 Kutoka mbinguni amewasikizisha sauti yake ili kuwaadilisha. Hapa duniani aliwaonyesha moto wake mkubwa, nanyi mlisikia maneno yake kutoka kwenye ule moto.
Out of heaven he made you to hear his voice, that he might instruct you: and on earth he showed you his great fire; and you heard his words out of the middle of the fire.
37 Kwa sababu aliwapenda baba zenu na alichagua wazao wao baada yao, aliwatoa katika nchi ya Misri kwa Uwepo wake na kwa uwezo wake mkuu,
And because he loved your fathers, therefore he chose their seed after them, and brought you out in his sight with his mighty power out of Egypt;
38 aliwafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi na kuwaleta ninyi katika nchi yao na akawapa ninyi kuwa urithi wenu, kama ilivyo leo.
To drive out nations from before you greater and mightier than you are, to bring you in, to give you their land for an inheritance, as it is this day.
39 Kubalini na mweke moyoni leo kuwa Bwana ndiye Mungu mbinguni juu na duniani chini. Hakuna mwingine.
Know therefore this day, and consider it in your heart, that the LORD he is God in heaven above, and on the earth beneath: there is none else.
40 Mshike amri na maagizo yake ninayowapa leo, ili mpate kufanikiwa ninyi na watoto wenu baada yenu, na mpate kuishi maisha marefu katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu siku zote.
You shall keep therefore his statutes, and his commandments, which I command you this day, that it may go well with you, and with your children after you, and that you may prolong your days on the earth, which the LORD your God gives you, for ever.
41 Kisha Mose akatenga miji mitatu mashariki ya Yordani,
Then Moses severed three cities on this side Jordan toward the sun rise;
42 ambayo mtu yeyote aliyemuua mtu angeweza kukimbilia ikiwa amemuua jirani yake bila kukusudia na bila kuwa na chuki naye siku zilizopita. Angeweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake.
That the slayer might flee thither, which should kill his neighbor unawares, and hated him not in times past; and that fleeing to one of these cities he might live:
43 Miji hiyo ilikuwa: Bezeri katika tambarare ya jangwa kwa ajili ya Wareubeni; Ramothi katika nchi ya Gileadi kwa ajili ya Wagadi; nao mji wa Golani katika nchi ya Bashani kwa ajili ya Wamanase.
Namely, Bezer in the wilderness, in the plain country, of the Reubenites; and Ramoth in Gilead, of the Gadites; and Golan in Bashan, of the Manassites.
44 Hii ndiyo sheria Mose aliyoweka mbele ya Waisraeli.
And this is the law which Moses set before the children of Israel:
45 Haya ndiyo masharti, amri na sheria Mose aliyowapa wana wa Israeli wakati walitoka Misri,
These are the testimonies, and the statutes, and the judgments, which Moses spoke to the children of Israel, after they came forth out of Egypt.
46 nao walikuwa katika bonde karibu na Beth-Peori mashariki ya Yordani, katika nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, naye alishindwa na Mose na Waisraeli walipokuja toka Misri.
On this side Jordan, in the valley over against Bethpeor, in the land of Sihon king of the Amorites, who dwelled at Heshbon, whom Moses and the children of Israel smote, after they were come forth out of Egypt:
47 Waliimiliki nchi yake na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, wafalme wawili Waamori waliotawala mashariki ya Yordani.
And they possessed his land, and the land of Og king of Bashan, two kings of the Amorites, which were on this side Jordan toward the sun rise;
48 Nchi hii ilienea kutoka Aroeri ukingoni mwa Bonde la Arnoni mpaka Mlima Sioni (yaani Hermoni),
From Aroer, which is by the bank of the river Arnon, even to mount Sion, which is Hermon,
49 pamoja na eneo lote la Araba mashariki ya Yordani, na kuenea mpaka Bahari ya Araba kwenye miteremko ya Pisga.
And all the plain on this side Jordan eastward, even to the sea of the plain, under the springs of Pisgah.

< Torati 4 >