< Torati 33 >
1 Hii ndiyo baraka Mose mtu wa Mungu aliyotamka kwa Waisraeli kabla ya kifo chake.
A ovo je blagoslov kojim blagoslovi Mojsije èovjek Božji sinove Izrailjeve pred smrt svoju.
2 Alisema: “Bwana alikuja kutoka Mlima Sinai, akachomoza kama jua juu yao kutoka Mlima Seiri, akaangaza kutoka Mlima Parani. Alikuja pamoja na watakatifu makumi elfu kutoka kusini, kutoka materemko ya mlima wake.
I reèe: Gospod izide sa Sinaja, i pokaza im se sa Sira; zasja s gore Faranske, i doðe s mnoštvom tisuæa svetaca, a u desnici mu zakon ognjeni za njih.
3 Hakika ni wewe ambaye huwapenda watu, watakatifu wako wote wamo mkononi mwako. Miguuni pako wote wanasujudu na kutoka kwako wanapokea mafundisho,
Doista ljubi narode; svi su sveti njegovi u ruci tvojoj; i oni se slegoše k nogama tvojim da prime rijeèi tvoje.
4 sheria ile Mose aliyotupa sisi, tulio milki ya kusanyiko la Yakobo.
Mojsije nam dade zakon, našljedstvo zboru Jakovljevu.
5 Alikuwa mfalme juu ya Yeshuruni wakati viongozi wa watu walipokusanyika, pamoja na makabila ya Israeli.
Jer bijaše car u Izrailju, kad se sabirahu knezovi narodni, plemena Izrailjeva.
6 “Reubeni na aishi, asife, wala watu wake wasiwe wachache.”
Da živi Ruvim i ne umre, a ljudi njegovijeh da bude malo!
7 Akasema hili kuhusu Yuda: “Ee Bwana, sikia kilio cha Yuda, mlete kwa watu wake. Kwa mikono yake mwenyewe hujitetea. Naam, uwe msaada wake dhidi ya adui zake!”
A za Judu reèe: usliši Gospode glas Judin, i dovedi ga opet k narodu njegovu; ruke njegove neka vojuju za nj, a ti mu pomaži protiv neprijatelja njegovijeh.
8 Kuhusu Lawi alisema: “Thumimu yako na Urimu yako ulimpa, mtu yule uliyemfadhili. Ulimjaribu huko Masa na kushindana naye kwenye maji ya Meriba.
I za Levija reèe: tvoj Tumim i tvoj Urim neka budu u èovjeka tvojega svetoga, kojega si okušao u Masi i s kojim si se prepirao na vodi Merivi;
9 Alinena hivi kuhusu baba yake na mama yake, ‘Mimi siwahitaji kamwe.’ Akawasahau jamaa zake, asiwatambue hata watoto wake, lakini akaliangalia neno lako na kulilinda Agano lako.
Koji reèe ocu svojemu i materi svojoj: ne gledam na vas; koji ne poznaje braæe svoje i za sinove svoje ne zna; jer drže rijeèi tvoje, i zavjet tvoj èuvaju.
10 Humfundisha Yakobo mausia yako na Israeli sheria yako. Hufukiza uvumba mbele zako na sadaka nzima za kuteketezwa juu ya madhabahu yako.
Oni uèe uredbama tvojim Jakova i zakonu tvojemu Izrailja, i meæu kad pod nozdrve tvoje i žrtvu što se sažiže na oltar tvoj.
11 Ee Bwana, bariki ustadi wake wote, nawe upendezwe na kazi ya mikono yake. Vipige viuno vya wale wainukao dhidi yake; wapige adui zake hata wasiinuke tena.”
Blagoslovi, Gospode, vojsku njegovu, i neka ti milo bude djelo ruku njegovijeh; polomi bedre onima koji ustaju na nj i koji mrze na nj, da ne ustanu.
12 Kuhusu Benyamini akasema: “Mwache mpenzi wa Bwana apumzike salama kwake, kwa maana humkinga mchana kutwa, na yule Bwana ampendaye hupumzika kati ya mabega yake.”
Za Venijamina reèe: mili Gospodu nastavaæe bez straha s njim; zaklanjaæe ga svaki dan, i meðu pleæima njegovijem nastavaæe.
13 Kuhusu Yosefu akasema: “Bwana na aibariki nchi yake kwa umande wa thamani kutoka mbinguni juu, na vilindi vya maji vilivyotulia chini;
I za Josifa reèe: blagoslovena je zemlja njegova od Gospoda blagom s neba, rosom, i iz dubine ozdo,
14 pamoja na vitu vilivyo bora sana viletwavyo na jua, na vitu vizuri sana vinavyoweza kutolewa na mwezi;
I blagom koje dolazi od sunca, i blagom koje dolazi od mjeseca,
15 pamoja na zawadi bora sana za milima ya zamani na kwa wingi wa baraka za vilima vya milele;
I blagom starijeh brda i blagom vjeènijeh humova,
16 pamoja na baraka nzuri mno za ardhi na ukamilifu wake, na upendeleo wake yeye aliyeishi kwenye kichaka kilichokuwa kinawaka moto. Hivi vyote na vikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la uso la aliye mkuu miongoni mwa ndugu zake.
I blagom na zemlji i obiljem njezinijem, i milošæu onoga koji stoji u kupini. Neka to doðe na glavu Josifu i na tjeme odvojenome izmeðu braæe svoje.
17 Katika fahari yeye ni kama fahali mzaliwa wa kwanza; pembe zake ni pembe za nyati, na kwa pembe hizo atapiga mataifa, hata yaliyo miisho ya dunia. Hivyo ndivyo yalivyo makumi elfu ya Efraimu; hivyo ndivyo yalivyo maelfu ya Manase.”
Krasota je njegova kao u prvenca teleta, i rogovi njegovi kao rogovi u jednoroga; njima æe bosti narode sve do kraja zemlje; to je mnoštvo tisuæa Jefremovijeh i tisuæe Manasijine.
18 Kuhusu Zabuloni akasema: “Shangilia, Zabuloni, wakati wa kutoka nje, nawe Isakari, katika mahema yako.
A za Zavulona reèe: veseli se Zavulone izlaskom svojim, i Isahare šatorima svojim.
19 Watawaita mataifa kwenye mlima, na huko mtatoa dhabihu za haki; watajifurahisha kwa wingi uliojaza bahari, kwa hazina zilizofichwa mchangani.”
Narode æe sazvati na goru, ondje æe prinijeti žrtve pravedne; jer æe obilje morsko sisati i sakriveno blago u pijesku.
20 Kuhusu Gadi akasema: “Atabarikiwa yeye aongezaye milki ya Gadi! Gadi huishi huko kama simba, akirarua kwenye mkono au kichwa.
A za Gada reèe: blagosloven je koji širi Gada; on nastava kao lav, i kida ruku i glavu.
21 Alijichagulia nchi nzuri kuliko zote kwa ajili yake mwenyewe; fungu la kiongozi lilikuwa limehifadhiwa kwa ajili yake. Viongozi wa watu walipokusanyika, alitimiza haki ya mapenzi ya Bwana, na hukumu zake kuhusu Israeli.”
Izabra sebi prvo, jer ondje dobi dio od onoga koji dade zakon; zato æe iæi s knezovima narodnijem, i izvršivati pravdu Gospodnju i sudove njegove s Izrailjem.
22 Kuhusu Dani akasema: “Dani ni mwana simba, akiruka kutoka Bashani.”
A za Dana reèe: Dan je laviæ, koji æe iskakati iz Vasana.
23 Kuhusu Naftali akasema: “Naftali amejaa tele upendeleo wa Bwana, naye amejaa baraka yake; atarithi magharibi na kusini.”
I za Neftalima reèe: Neftalime, siti milosti i puni blagoslova Gospodnjega, zapad i jug uzmi.
24 Kuhusu Asheri akasema: “Aliyebarikiwa zaidi sana katika wana ni Asheri; yeye na apate upendeleo kwa ndugu zake, yeye na anawe miguu yake kwenye mafuta.
I za Asira reèe: Asir æe biti blagosloven mimo druge sinove, biæe mio braæi svojoj, zamakaæe u ulje nogu svoju.
25 Makomeo ya malango yako yawe chuma na shaba, nazo nguvu zako zitakuwa sawa na siku zako.
Gvožðe i mjed biæe pod obuæom tvojom; i dokle traju dani tvoji trajaæe snaga tvoja.
26 “Hakuna mwingine kama Mungu wa Yeshuruni, ambaye hupanda juu ya mbingu ili akusaidie, na juu ya mawingu katika utukufu wake.
Izrailju! niko nije kao Bog, koji ide po nebu tebi u pomoæ, i u velièanstvu svojem na oblacima.
27 Mungu wa milele ni kimbilio lako, na chini kuna mikono ya milele. Atamfukuza adui yako mbele yako, akisema, ‘Mwangamize yeye!’
Zaklon je Bog vjeèni i pod mišicom vjeènom; on æe odagnati ispred tebe neprijatelje tvoje, i reæi æe: zatri!
28 Hivyo Israeli ataishi salama peke yake. Mzao wa Yakobo ni salama katika nchi ya nafaka na divai mpya, mahali ambapo mbingu hudondosha umande.
Da bi nastavao Izrailj sam bezbrižno, izvor Jakovljev, u zemlji obilnoj žitom i vinom; i nebo æe njegovo kropiti rosom.
29 Ee Israeli, wewe umebarikiwa! Ni nani kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana? Yeye ni ngao yako na msaada wako, na upanga wako uliotukuka. Adui zako watatetemeka mbele yako, nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.”
Blago tebi, Izrailju! ko je kao ti, narod kojega je saèuvao Gospod, štit pomoæi tvoje, i maè slave tvoje? Neprijatelji æe se tvoji poniziti, a ti æeš gaziti visine njihove.