< Torati 33 >
1 Hii ndiyo baraka Mose mtu wa Mungu aliyotamka kwa Waisraeli kabla ya kifo chake.
Voici la bénédiction dont Moïse, homme de Dieu, bénit les enfants d’Israël avant sa mort.
2 Alisema: “Bwana alikuja kutoka Mlima Sinai, akachomoza kama jua juu yao kutoka Mlima Seiri, akaangaza kutoka Mlima Parani. Alikuja pamoja na watakatifu makumi elfu kutoka kusini, kutoka materemko ya mlima wake.
Il dit donc: Le Seigneur est venu de Sinaï, et il s’est levé pour nous de Séir; il a apparu de la montagne de Pharan, et avec lui des milliers de saints. En sa main droite était une loi de feu.
3 Hakika ni wewe ambaye huwapenda watu, watakatifu wako wote wamo mkononi mwako. Miguuni pako wote wanasujudu na kutoka kwako wanapokea mafundisho,
Il a aimé des peuples; tous les saints sont dans sa main; et ceux qui s’approchent de ses pieds recevront de sa doctrine.
4 sheria ile Mose aliyotupa sisi, tulio milki ya kusanyiko la Yakobo.
Moïse nous a prescrit une loi, héritage de la multitude de Jacob.
5 Alikuwa mfalme juu ya Yeshuruni wakati viongozi wa watu walipokusanyika, pamoja na makabila ya Israeli.
Il sera roi chez le peuple très juste, les princes du peuple étant assemblés avec les tribus d’Israël.
6 “Reubeni na aishi, asife, wala watu wake wasiwe wachache.”
Que Ruben vive, et qu’il ne meure pas, mais qu’il soit en petit nombre.
7 Akasema hili kuhusu Yuda: “Ee Bwana, sikia kilio cha Yuda, mlete kwa watu wake. Kwa mikono yake mwenyewe hujitetea. Naam, uwe msaada wake dhidi ya adui zake!”
Voici la bénédiction de Juda: Ecoutez, Seigneur, la voix de Juda et introduisez-le auprès de son peuple; ses mains combattront pour lui, et il sera son aide contre ses adversaires.
8 Kuhusu Lawi alisema: “Thumimu yako na Urimu yako ulimpa, mtu yule uliyemfadhili. Ulimjaribu huko Masa na kushindana naye kwenye maji ya Meriba.
À Lévi aussi il dit: Seigneur, votre perfection et votre doctrine sont à l’homme, votre saint, que vous avez éprouvé par une tentation, et jugé aux Eaux de contradiction;
9 Alinena hivi kuhusu baba yake na mama yake, ‘Mimi siwahitaji kamwe.’ Akawasahau jamaa zake, asiwatambue hata watoto wake, lakini akaliangalia neno lako na kulilinda Agano lako.
Qui a dit à son père et à sa mère: Je ne vous connais pas; et à ses frères: Je ne sais qui vous êtes; et ils n’ont pas connu leurs enfants. Ceux-là ont gardé votre parole, et ont observé votre alliance,
10 Humfundisha Yakobo mausia yako na Israeli sheria yako. Hufukiza uvumba mbele zako na sadaka nzima za kuteketezwa juu ya madhabahu yako.
Vos ordonnances, ô Jacob! et votre loi, ô Israël. Ils offriront de l’encens dans votre fureur, et un holocauste sur votre autel.
11 Ee Bwana, bariki ustadi wake wote, nawe upendezwe na kazi ya mikono yake. Vipige viuno vya wale wainukao dhidi yake; wapige adui zake hata wasiinuke tena.”
Bénissez, Seigneur, sa force, et recevez les œuvres de ses mains. Frappez le dos de ses ennemis, et que ceux qui le haïssent ne se relèvent point.
12 Kuhusu Benyamini akasema: “Mwache mpenzi wa Bwana apumzike salama kwake, kwa maana humkinga mchana kutwa, na yule Bwana ampendaye hupumzika kati ya mabega yake.”
Et à Benjamin il dit: Le bien-aimé du Seigneur habitera avec confiance en lui; il demeurera tout le jour comme dans une chambre nuptiale, et il se reposera entre ses bras.
13 Kuhusu Yosefu akasema: “Bwana na aibariki nchi yake kwa umande wa thamani kutoka mbinguni juu, na vilindi vya maji vilivyotulia chini;
À Joseph aussi il dit: Que la terre de Joseph soit remplie de la bénédiction du Seigneur, des fruits du ciel, de la rosée, et de l’abîme qui est en bas;
14 pamoja na vitu vilivyo bora sana viletwavyo na jua, na vitu vizuri sana vinavyoweza kutolewa na mwezi;
De toutes les sortes de fruits que mûrissent le soleil et la lune;
15 pamoja na zawadi bora sana za milima ya zamani na kwa wingi wa baraka za vilima vya milele;
Des fruits du sommet des montagnes antiques et de ceux des collines éternelles,
16 pamoja na baraka nzuri mno za ardhi na ukamilifu wake, na upendeleo wake yeye aliyeishi kwenye kichaka kilichokuwa kinawaka moto. Hivi vyote na vikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la uso la aliye mkuu miongoni mwa ndugu zake.
De tous les grains de la terre et de son abondance. Que la bénédiction de celui qui a apparu dans un buisson vienne sur la tête de Joseph, et sur la tête de celui qui est nazaréen entre ses frères.
17 Katika fahari yeye ni kama fahali mzaliwa wa kwanza; pembe zake ni pembe za nyati, na kwa pembe hizo atapiga mataifa, hata yaliyo miisho ya dunia. Hivyo ndivyo yalivyo makumi elfu ya Efraimu; hivyo ndivyo yalivyo maelfu ya Manase.”
Sa beauté est comme celle du premier-né d’un taureau; les cornes du rhinocéros sont ses cornes; avec elles il fera sauter en l’air des nations jusqu’aux extrémités de la terre. Telle seront les troupes nombreuses d’Ephraïm, et tels les milliers de Manassé,
18 Kuhusu Zabuloni akasema: “Shangilia, Zabuloni, wakati wa kutoka nje, nawe Isakari, katika mahema yako.
Et à Zabulon il dit: Réjouis-toi, Zabulon, dans ta sortie, et, Issachar, dans tes tabernacles.
19 Watawaita mataifa kwenye mlima, na huko mtatoa dhabihu za haki; watajifurahisha kwa wingi uliojaza bahari, kwa hazina zilizofichwa mchangani.”
Ils appelleront des peuples sur la montagne; là, ils immoleront des victimes de justice. Ils suceront comme le lait les eaux débordantes de la mer, et les trésors cachés dans les sables.
20 Kuhusu Gadi akasema: “Atabarikiwa yeye aongezaye milki ya Gadi! Gadi huishi huko kama simba, akirarua kwenye mkono au kichwa.
Et à Gad il dit: Béni Gad dans son étendue! il s’est reposé comme un lion, puis il a saisi un bras et une tête.
21 Alijichagulia nchi nzuri kuliko zote kwa ajili yake mwenyewe; fungu la kiongozi lilikuwa limehifadhiwa kwa ajili yake. Viongozi wa watu walipokusanyika, alitimiza haki ya mapenzi ya Bwana, na hukumu zake kuhusu Israeli.”
Et il a vu sa primauté, qui est que dans son partage était placé un docteur: et il a été avec les princes d’un peuple, et il a exécuté les justices du Seigneur et son jugement avec Israël.
22 Kuhusu Dani akasema: “Dani ni mwana simba, akiruka kutoka Bashani.”
À Dan aussi il dit: Dan est le petit d’un lion, il se répandra de Basan au loin.
23 Kuhusu Naftali akasema: “Naftali amejaa tele upendeleo wa Bwana, naye amejaa baraka yake; atarithi magharibi na kusini.”
Et à Nephtali il dit: Nephtali jouira de l’abondance et il sera rempli des bénédictions du Seigneur; il possédera la mer et le midi.
24 Kuhusu Asheri akasema: “Aliyebarikiwa zaidi sana katika wana ni Asheri; yeye na apate upendeleo kwa ndugu zake, yeye na anawe miguu yake kwenye mafuta.
À Aser aussi il dit: Béni Aser entre les fils d’Israël! qu’il soit agréable à ses frères, et qu’il trempe son pied dans l’huile.
25 Makomeo ya malango yako yawe chuma na shaba, nazo nguvu zako zitakuwa sawa na siku zako.
Le fer et l’airain seront sa chaussure. Ta vieillesse sera comme les jours de ta jeunesse.
26 “Hakuna mwingine kama Mungu wa Yeshuruni, ambaye hupanda juu ya mbingu ili akusaidie, na juu ya mawingu katika utukufu wake.
Il n’est pas un autre Dieu comme le Dieu du peuple très juste; celui qui monte sur le ciel est ton aide. Par sa magnificence les nuées courent de toutes parts;
27 Mungu wa milele ni kimbilio lako, na chini kuna mikono ya milele. Atamfukuza adui yako mbele yako, akisema, ‘Mwangamize yeye!’
Son habitacle est en haut; et au-dessous sont ses bras éternels; il chassera de ta face l’ennemi, et il dira: Sois brisé.
28 Hivyo Israeli ataishi salama peke yake. Mzao wa Yakobo ni salama katika nchi ya nafaka na divai mpya, mahali ambapo mbingu hudondosha umande.
Israël habitera avec assurance et seul. L’œil de Jacob sera fixé sur une terre de vin et de blé, et les cieux seront obscurcis par la rosée.
29 Ee Israeli, wewe umebarikiwa! Ni nani kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana? Yeye ni ngao yako na msaada wako, na upanga wako uliotukuka. Adui zako watatetemeka mbele yako, nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.”
Tu es heureux, Israël: qui est semblable à toi, peuple, qui es sauvé dans le Seigneur? il est le bouclier de ta défense, et le glaive de ta gloire; tes ennemis te renieront, et tu fouleras aux pieds leurs cous.