< Torati 33 >
1 Hii ndiyo baraka Mose mtu wa Mungu aliyotamka kwa Waisraeli kabla ya kifo chake.
Or voici la bénédiction dont Moïse, homme de Dieu, bénit les enfants d'Israël avant sa mort.
2 Alisema: “Bwana alikuja kutoka Mlima Sinai, akachomoza kama jua juu yao kutoka Mlima Seiri, akaangaza kutoka Mlima Parani. Alikuja pamoja na watakatifu makumi elfu kutoka kusini, kutoka materemko ya mlima wake.
Il dit donc: L'Éternel est venu de Sinaï, et s'est levé sur eux de Séir; il a resplendi de la montagne de Paran; il est sorti des myriades de saints; de sa droite sortait pour eux le feu de la loi.
3 Hakika ni wewe ambaye huwapenda watu, watakatifu wako wote wamo mkononi mwako. Miguuni pako wote wanasujudu na kutoka kwako wanapokea mafundisho,
Oui, il aime les peuples. Tous ses saints sont en ta main. Ils se sont tenus à tes pieds pour recevoir tes paroles.
4 sheria ile Mose aliyotupa sisi, tulio milki ya kusanyiko la Yakobo.
Moïse nous a donné la loi, héritage de l'assemblée de Jacob;
5 Alikuwa mfalme juu ya Yeshuruni wakati viongozi wa watu walipokusanyika, pamoja na makabila ya Israeli.
Et il a été roi en Jeshurun (Israël), quand les chefs du peuple s'assemblaient avec les tribus d'Israël.
6 “Reubeni na aishi, asife, wala watu wake wasiwe wachache.”
Que Ruben vive, et qu'il ne meure point, et que ses hommes soient nombreux!
7 Akasema hili kuhusu Yuda: “Ee Bwana, sikia kilio cha Yuda, mlete kwa watu wake. Kwa mikono yake mwenyewe hujitetea. Naam, uwe msaada wake dhidi ya adui zake!”
Et sur Juda, voici ce que Moïse dit: Écoute, Éternel, la voix de Juda, et ramène-le vers son peuple; que ses mains soient puissantes, et sois-lui en aide contre ses ennemis!
8 Kuhusu Lawi alisema: “Thumimu yako na Urimu yako ulimpa, mtu yule uliyemfadhili. Ulimjaribu huko Masa na kushindana naye kwenye maji ya Meriba.
Il dit aussi, touchant Lévi: Tes Thummim et tes Urim sont à ton pieux serviteur, que tu éprouvas à Massa, avec lequel tu contestas aux eaux de Mériba;
9 Alinena hivi kuhusu baba yake na mama yake, ‘Mimi siwahitaji kamwe.’ Akawasahau jamaa zake, asiwatambue hata watoto wake, lakini akaliangalia neno lako na kulilinda Agano lako.
Qui dit de son père et de sa mère: Je ne l'ai point vu; et qui n'a point reconnu ses frères, ni connu ses enfants. Car ils ont observé tes paroles, et ils garderont ton alliance.
10 Humfundisha Yakobo mausia yako na Israeli sheria yako. Hufukiza uvumba mbele zako na sadaka nzima za kuteketezwa juu ya madhabahu yako.
Ils enseigneront tes ordonnances à Jacob, et ta loi à Israël; ils mettront le parfum sous tes narines, et l'holocauste sur ton autel.
11 Ee Bwana, bariki ustadi wake wote, nawe upendezwe na kazi ya mikono yake. Vipige viuno vya wale wainukao dhidi yake; wapige adui zake hata wasiinuke tena.”
O Éternel, bénis sa force, et agrée l'œuvre de ses mains. Frappe aux reins ceux qui s'élèvent contre lui, et ceux qui le haïssent, dès qu'ils s'élèveront.
12 Kuhusu Benyamini akasema: “Mwache mpenzi wa Bwana apumzike salama kwake, kwa maana humkinga mchana kutwa, na yule Bwana ampendaye hupumzika kati ya mabega yake.”
Sur Benjamin il dit: Celui que l'Éternel aime habitera en sécurité près de lui; il le couvrira tout le jour, et il se tiendra entre ses épaules.
13 Kuhusu Yosefu akasema: “Bwana na aibariki nchi yake kwa umande wa thamani kutoka mbinguni juu, na vilindi vya maji vilivyotulia chini;
Et sur Joseph il dit: Son pays est béni par l'Éternel, du précieux don des cieux, de la rosée, et de l'abîme qui repose en bas;
14 pamoja na vitu vilivyo bora sana viletwavyo na jua, na vitu vizuri sana vinavyoweza kutolewa na mwezi;
Des plus précieux produits du soleil, et des plus précieux fruits des lunes;
15 pamoja na zawadi bora sana za milima ya zamani na kwa wingi wa baraka za vilima vya milele;
Des meilleures productions des montagnes antiques et des précieuses productions des coteaux éternels;
16 pamoja na baraka nzuri mno za ardhi na ukamilifu wake, na upendeleo wake yeye aliyeishi kwenye kichaka kilichokuwa kinawaka moto. Hivi vyote na vikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la uso la aliye mkuu miongoni mwa ndugu zake.
De ce qu'il y a de plus précieux sur la terre, et de son abondance. Et que la bienveillance de celui qui apparut dans le buisson vienne sur la tête de Joseph, et sur le front du prince de ses frères.
17 Katika fahari yeye ni kama fahali mzaliwa wa kwanza; pembe zake ni pembe za nyati, na kwa pembe hizo atapiga mataifa, hata yaliyo miisho ya dunia. Hivyo ndivyo yalivyo makumi elfu ya Efraimu; hivyo ndivyo yalivyo maelfu ya Manase.”
Il a la beauté du premier-né de ses taureaux, et ses cornes sont les cornes d'un buffle; avec elles il heurtera tous les peuples ensemble jusqu'aux bouts de la terre; ce sont les myriades d'Éphraïm, ce sont les milliers de Manassé.
18 Kuhusu Zabuloni akasema: “Shangilia, Zabuloni, wakati wa kutoka nje, nawe Isakari, katika mahema yako.
Et de Zabulon il dit: Réjouis-toi, Zabulon, dans ta sortie; et toi, Issacar, dans tes tentes!
19 Watawaita mataifa kwenye mlima, na huko mtatoa dhabihu za haki; watajifurahisha kwa wingi uliojaza bahari, kwa hazina zilizofichwa mchangani.”
Ils appelleront les peuples à la montagne; là ils offriront des sacrifices de justice; car ils suceront l'abondance des mers et les trésors cachés dans le sable.
20 Kuhusu Gadi akasema: “Atabarikiwa yeye aongezaye milki ya Gadi! Gadi huishi huko kama simba, akirarua kwenye mkono au kichwa.
Et de Gad il dit: Béni soit celui qui met Gad au large! Il repose comme un lion, et il déchire bras et tête;
21 Alijichagulia nchi nzuri kuliko zote kwa ajili yake mwenyewe; fungu la kiongozi lilikuwa limehifadhiwa kwa ajili yake. Viongozi wa watu walipokusanyika, alitimiza haki ya mapenzi ya Bwana, na hukumu zake kuhusu Israeli.”
Il s'est choisi les prémices du pays, parce que là était cachée la portion du législateur; et il est venu avec les chefs du peuple; il a exécuté la justice de l'Éternel, et ses jugements envers Israël.
22 Kuhusu Dani akasema: “Dani ni mwana simba, akiruka kutoka Bashani.”
Et sur Dan il dit: Dan est un jeune lion, qui s'élance de Bassan.
23 Kuhusu Naftali akasema: “Naftali amejaa tele upendeleo wa Bwana, naye amejaa baraka yake; atarithi magharibi na kusini.”
Et de Nephthali il dit: Nephthali, rassasié de faveurs et rempli de la bénédiction de l'Éternel, possède l'Occident et le Midi!
24 Kuhusu Asheri akasema: “Aliyebarikiwa zaidi sana katika wana ni Asheri; yeye na apate upendeleo kwa ndugu zake, yeye na anawe miguu yake kwenye mafuta.
Et d'Asser il dit: Qu'Asser soit béni entre les fils; qu'il soit agréable à ses frères, et qu'il baigne son pied dans l'huile!
25 Makomeo ya malango yako yawe chuma na shaba, nazo nguvu zako zitakuwa sawa na siku zako.
Tes verrous seront de fer et d'airain, et ton repos durera autant que tes jours.
26 “Hakuna mwingine kama Mungu wa Yeshuruni, ambaye hupanda juu ya mbingu ili akusaidie, na juu ya mawingu katika utukufu wake.
Nul n'est, ô Jeshurun (Israël), semblable au Dieu qui vient à ton aide, porté sur les cieux et sur les nues, dans sa majesté.
27 Mungu wa milele ni kimbilio lako, na chini kuna mikono ya milele. Atamfukuza adui yako mbele yako, akisema, ‘Mwangamize yeye!’
C'est une retraite que le Dieu qui est de tout temps, et que d'être sous ses bras éternels. Il a chassé de devant toi l'ennemi, et il a dit: Extermine!
28 Hivyo Israeli ataishi salama peke yake. Mzao wa Yakobo ni salama katika nchi ya nafaka na divai mpya, mahali ambapo mbingu hudondosha umande.
Et Israël habitera en sécurité; la source issue de Jacob jaillit à part dans un pays de froment et de moût, et dont les cieux distillent la rosée.
29 Ee Israeli, wewe umebarikiwa! Ni nani kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana? Yeye ni ngao yako na msaada wako, na upanga wako uliotukuka. Adui zako watatetemeka mbele yako, nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.”
Oh! que tu es heureux, Israël! Qui est semblable à toi, peuple sauvé par l'Éternel, le bouclier de ton secours et l'épée par laquelle tu es exalté? Tes ennemis dissimuleront devant toi; et toi, tu fouleras de tes pieds leurs hauts lieux