< Torati 33 >

1 Hii ndiyo baraka Mose mtu wa Mungu aliyotamka kwa Waisraeli kabla ya kifo chake.
This is the blessing, wherewith the man of God Moses blessed the children of Israel, before his death.
2 Alisema: “Bwana alikuja kutoka Mlima Sinai, akachomoza kama jua juu yao kutoka Mlima Seiri, akaangaza kutoka Mlima Parani. Alikuja pamoja na watakatifu makumi elfu kutoka kusini, kutoka materemko ya mlima wake.
And he said: The Lord came from Sinai, and from Seir he rose up to us: he hath appeared from mount Pharan, and with him thousands of saints. In his right hand a fiery law.
3 Hakika ni wewe ambaye huwapenda watu, watakatifu wako wote wamo mkononi mwako. Miguuni pako wote wanasujudu na kutoka kwako wanapokea mafundisho,
He hath loved the people, all the saints are in his hand: and they that approach to his feet, shall receive of his doctrine.
4 sheria ile Mose aliyotupa sisi, tulio milki ya kusanyiko la Yakobo.
Moses commanded us a law, the inheritance of the multitude of Jacob.
5 Alikuwa mfalme juu ya Yeshuruni wakati viongozi wa watu walipokusanyika, pamoja na makabila ya Israeli.
He shall be king with the most right, the princes of the people being assembled with the tribes of Israel.
6 “Reubeni na aishi, asife, wala watu wake wasiwe wachache.”
Let Ruben live, and not die, and be he small in number.
7 Akasema hili kuhusu Yuda: “Ee Bwana, sikia kilio cha Yuda, mlete kwa watu wake. Kwa mikono yake mwenyewe hujitetea. Naam, uwe msaada wake dhidi ya adui zake!”
This is the blessing of Juda. Hear, O Lord, the voice of Juda, and bring him in unto his people: his hands shall fight for him, and he shall be his helper against his enemies.
8 Kuhusu Lawi alisema: “Thumimu yako na Urimu yako ulimpa, mtu yule uliyemfadhili. Ulimjaribu huko Masa na kushindana naye kwenye maji ya Meriba.
To Levi also he said: Thy perfection, and thy doctrine be to thy holy man, whom thou hast proved in the temptation, and judged at the waters of contradiction:
9 Alinena hivi kuhusu baba yake na mama yake, ‘Mimi siwahitaji kamwe.’ Akawasahau jamaa zake, asiwatambue hata watoto wake, lakini akaliangalia neno lako na kulilinda Agano lako.
Who hath said to his father, and to his mother: I do not know you; and to his brethren: I know you not: and their own children they have not known. These have kept thy word, and observed thy covenant,
10 Humfundisha Yakobo mausia yako na Israeli sheria yako. Hufukiza uvumba mbele zako na sadaka nzima za kuteketezwa juu ya madhabahu yako.
Thy judgments, O Jacob, and thy law, O Israel: they shall put incense in thy wrath and holocaust upon thy altar.
11 Ee Bwana, bariki ustadi wake wote, nawe upendezwe na kazi ya mikono yake. Vipige viuno vya wale wainukao dhidi yake; wapige adui zake hata wasiinuke tena.”
Bless, O Lord, his strength, and receive the works of his hands. Strike the backs of his enemies, and let not them that hate him rise.
12 Kuhusu Benyamini akasema: “Mwache mpenzi wa Bwana apumzike salama kwake, kwa maana humkinga mchana kutwa, na yule Bwana ampendaye hupumzika kati ya mabega yake.”
And to Benjamin he said: The best beloved of the Lord shall dwell confidently in him: as in a bride chamber shall he abide all the day long, and between his shoulders shall be rest.
13 Kuhusu Yosefu akasema: “Bwana na aibariki nchi yake kwa umande wa thamani kutoka mbinguni juu, na vilindi vya maji vilivyotulia chini;
To Joseph also he said: Of the blessing of the Lord be his land, of the fruits of heaven, and of the dew, and of the deep that lieth beneath.
14 pamoja na vitu vilivyo bora sana viletwavyo na jua, na vitu vizuri sana vinavyoweza kutolewa na mwezi;
Of the fruits brought forth by the sun and by the moon.
15 pamoja na zawadi bora sana za milima ya zamani na kwa wingi wa baraka za vilima vya milele;
Of the tops of the ancient mountains, of the fruits of the everlasting hills:
16 pamoja na baraka nzuri mno za ardhi na ukamilifu wake, na upendeleo wake yeye aliyeishi kwenye kichaka kilichokuwa kinawaka moto. Hivi vyote na vikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la uso la aliye mkuu miongoni mwa ndugu zake.
And of the fruits of the earth, and of the fulness thereof. The blessing of him that appeared in the bush, come upon the head of Joseph, and upon the crown of the Nazarite among his brethren.
17 Katika fahari yeye ni kama fahali mzaliwa wa kwanza; pembe zake ni pembe za nyati, na kwa pembe hizo atapiga mataifa, hata yaliyo miisho ya dunia. Hivyo ndivyo yalivyo makumi elfu ya Efraimu; hivyo ndivyo yalivyo maelfu ya Manase.”
His beauty as of the firstling of a bullock, his horns as the horns of a rhinoceros: with them shall he push the nations even to the ends of the earth These are the multitudes of Ephraim and these the thousands of Manasses.
18 Kuhusu Zabuloni akasema: “Shangilia, Zabuloni, wakati wa kutoka nje, nawe Isakari, katika mahema yako.
And to Zabulon he said: Rejoice, O Zabulon, in thy going out; and Issachar in thy tabernacles.
19 Watawaita mataifa kwenye mlima, na huko mtatoa dhabihu za haki; watajifurahisha kwa wingi uliojaza bahari, kwa hazina zilizofichwa mchangani.”
They shall call the people to the mountain: there shall they sacrifice the victims of justice. Who shall suck as milk the abundance of the sea, and the hidden treasures of the sands.
20 Kuhusu Gadi akasema: “Atabarikiwa yeye aongezaye milki ya Gadi! Gadi huishi huko kama simba, akirarua kwenye mkono au kichwa.
And to Gad he said: Blessed be Gad in his breadth: he hath rested as a lion, and hath seized upon the arm and the top of the head.
21 Alijichagulia nchi nzuri kuliko zote kwa ajili yake mwenyewe; fungu la kiongozi lilikuwa limehifadhiwa kwa ajili yake. Viongozi wa watu walipokusanyika, alitimiza haki ya mapenzi ya Bwana, na hukumu zake kuhusu Israeli.”
And he saw his pre-eminence, that in his portion the teacher was laid up: who was with the princes of the people, and did the justices of the Lord, and his judgment with Israel.
22 Kuhusu Dani akasema: “Dani ni mwana simba, akiruka kutoka Bashani.”
To Dan also he said: Dan is a young lion, he shall flow plentifully from Basan.
23 Kuhusu Naftali akasema: “Naftali amejaa tele upendeleo wa Bwana, naye amejaa baraka yake; atarithi magharibi na kusini.”
And to Nephtali he said: Nephtali shall enjoy abundance, and shall be full of the blessings of the Lord: he shall possess the sea and the south.
24 Kuhusu Asheri akasema: “Aliyebarikiwa zaidi sana katika wana ni Asheri; yeye na apate upendeleo kwa ndugu zake, yeye na anawe miguu yake kwenye mafuta.
To Aser also he said: Let Aser be blessed with children, let him be acceptable to his brethren, and let him dip his foot in oil.
25 Makomeo ya malango yako yawe chuma na shaba, nazo nguvu zako zitakuwa sawa na siku zako.
His shoe shall be iron and brass. As the days of thy youth, so also shall thy old age be.
26 “Hakuna mwingine kama Mungu wa Yeshuruni, ambaye hupanda juu ya mbingu ili akusaidie, na juu ya mawingu katika utukufu wake.
There is no other God like the God of the rightest: he that is mounted upon the heaven is thy helper. By his magnificence the clouds run hither and thither.
27 Mungu wa milele ni kimbilio lako, na chini kuna mikono ya milele. Atamfukuza adui yako mbele yako, akisema, ‘Mwangamize yeye!’
His dwelling is above, and underneath are the everlasting arms: he shall cast out the enemy from before thee, and shall say: Be thou brought to nought.
28 Hivyo Israeli ataishi salama peke yake. Mzao wa Yakobo ni salama katika nchi ya nafaka na divai mpya, mahali ambapo mbingu hudondosha umande.
Israel shall dwell in safety, and alone. The eye of Jacob in a land of corn and wine, and the heavens shall be misty with dew.
29 Ee Israeli, wewe umebarikiwa! Ni nani kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana? Yeye ni ngao yako na msaada wako, na upanga wako uliotukuka. Adui zako watatetemeka mbele yako, nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.”
Blessed are thou, Israel: who is like to thee, O people, that art saved by the Lord? the shield of thy help, and the sword of thy glory: thy enemies shall deny thee, and thou shalt tread upon their necks.

< Torati 33 >