< Torati 31 >

1 Kisha Mose akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote:
Et Moïse alla et adressa ces paroles à tous les Israélites
2 “Sasa nina miaka mia moja na ishirini nami siwezi tena kuwaongoza. Bwana ameniambia, ‘Hutavuka Yordani.’
et leur dit: Je suis maintenant âgé de cent vingt ans, et je ne puis plus entrer et sortir, et l'Éternel m'a dit: Tu ne passeras pas ce Jourdain;
3 Bwana Mungu wenu, yeye mwenyewe atavuka mbele yenu. Ataangamiza mataifa haya mbele yenu, nanyi mtaimiliki nchi yao. Pia Yoshua atavuka mbele yenu, kama Bwana alivyosema.
l'Éternel, ton Dieu, c'est Lui qui te précédera, Lui qui exterminera devant toi ces nations pour que vous en soyez maîtres. C'est Josué qui passera à votre tête, comme l'Éternel l'a annoncé.
4 Naye Bwana atawafanyia watu hao kile alichowafanyia Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, ambao aliwaangamiza pamoja na nchi yao.
Et l'Éternel les traitera, comme Il a traité Sihon et Og, rois des Amoréens, et leur pays qu'il a détruit.
5 Bwana atawakabidhi kwenu, nanyi lazima mwatendee yale yote niliyowaamuru.
Mais quand l'Éternel vous les livrera, traitez-les en tout point selon l'ordre que je vous ai prescrit.
6 Kuweni imara na moyo wa ushujaa. Msiogope wala msifadhaike kwa sababu yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu anakwenda pamoja nanyi; kamwe hatawaacha wala hatawatupa ninyi.”
Soyez courageux et fermes, n'ayez ni crainte ni peur d'eux, car c'est l'Éternel, ton Dieu, qui marchera avec toi. Il ne vous fera pas défaut, ne vous abandonnera pas.
7 Kisha Mose akamwita Yoshua na akamwambia mbele ya Israeli wote, “Uwe imara na moyo wa ushujaa, kwa kuwa ni lazima uende na watu hawa katika nchi ile Bwana aliyowaapia baba zao kuwapa, nawe ni lazima uwagawie kama urithi wao.
Et Moïse appela Josué et lui dit en présence de tout Israël: Sois courageux et ferme, car c'est toi qui entreras avec ce peuple dans le pays que l'Éternel a juré à leurs pères de leur donner, et toi qui le leur partageras.
8 Bwana mwenyewe atakutangulia naye atakuwa pamoja nawe; kamwe hatakuacha wala hatakutupa. Usiogope, wala usifadhaike.”
Et c'est l'Éternel qui te précédera; Il sera avec toi, et ne te fera pas défaut, ne t'abandonnera pas; sois sans crainte et sans alarmes.
9 Kwa hiyo Mose akaandika sheria hii na kuwapa makuhani, wana wa Lawi, waliochukua Sanduku la Agano la Bwana na wazee wote wa Israeli.
Et Moïse mit par écrit cette Loi et la remit aux Prêtres, fils de Lévi, porteurs de l'Arche de l'alliance de l'Éternel, et à tous les Anciens d'Israël.
10 Kisha Mose akawaamuru, akasema: “Mwishoni mwa kila miaka saba, katika mwaka wa kufuta madeni, wakati wa Sikukuu ya Vibanda,
Et Moïse leur donna cette instruction: Au terme de sept ans, à l'époque de l'année du relâche, à la Fête des Loges,
11 Waisraeli wote wanapokuja mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua, utasoma sheria hii mbele yao masikioni mwao.
lorsque tout Israël viendra se présenter devant l'Éternel, ton Dieu, dans le lieu choisi par Lui, tu donneras lecture de cette Loi devant tout Israël, à leurs oreilles.
12 Kusanya watu wote, wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, ili waweze kusikia na kujifunza kumcha Bwana Mungu wenu na kufuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii.
Rassemble le peuple, les hommes et les femmes et les enfants et tes étrangers qui seront dans tes Portes, afin qu'ils entendent, et qu'ils apprennent à craindre l'Éternel, votre Dieu, et à s'appliquer à la pratique de tous les préceptes de cette Loi.
13 Watoto wao, ambao hawaijui sheria hii, lazima waisikie na kujifunza kumcha Bwana Mungu wenu kwa muda mtakaoishi katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”
Et vos fils qui ignorent, écouteront et apprendront à craindre l'Éternel, votre Dieu, aussi longtemps que vous vivrez dans le pays dont après le passage du Jourdain vous allez faire la conquête.
14 Bwana akamwambia Mose, “Sasa siku ya kifo chako imekaribia. Mwite Yoshua, mkajihudhurishe katika Hema la Kukutania, mahali nitakapompa maagizo ya kazi.” Kwa hiyo Mose na Yoshua wakaja na kujihudhurisha kwenye Hema la Kukutania.
Et l'Éternel dit à Moïse: Voici, le moment de ta mort approche; appelle Josué, et placez-vous dans la Tente du Rendez-vous, et je lui donnerai mes ordres. Et Moïse et Josué allèrent se placer dans la Tente du Rendez-vous.
15 Kisha Bwana akatokea katika Hema katika nguzo ya wingu, nalo wingu likasimama juu ya ingilio la Hema.
Alors l'Éternel apparut dans la Tente, dans une colonne de nuée; et la colonne de nuée s'arrêta à la porte de la Tente.
16 Kisha Bwana akamwambia Mose: “Unakwenda kupumzika na baba zako, nao watu hawa hivi karibuni watazini na miungu migeni ya nchi wanayoingia. Wataniacha na kuvunja Agano nililofanya nao.
Et l'Éternel dit à Moïse: Voici, tu vas être couché à côté de tes pères, et ce peuple se lèvera, et se prostituera à la suite des dieux étrangers du pays dans lequel il va entrer, et il m'abandonnera, et rompra l'alliance que j'ai conclue avec lui;
17 Siku hiyo nitawakasirikia na kuwaacha; nitawaficha uso wangu, nao wataangamizwa. Maafa mengi na shida nyingi zitakuja juu yao, nao siku hiyo watauliza, ‘Je, maafa haya hayakuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko pamoja nasi?’
et ma colère s'allumera contre lui dans ce moment-là, et je l'abandonnerai et lui cacherai ma face, et il sera livré comme proie, et atteint par beaucoup de maux et de détresses, et il dira alors: N'est-ce pas parce que notre Dieu n'est pas au milieu de moi, que ces maux m'ont atteint?
18 Nami hakika nitauficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yao yote kwa kugeukia miungu mingine.
Et je cacherai ma face dans ce temps-là, à cause de tout le mal qu'il aura fait en se tournant vers des dieux étrangers.
19 “Sasa ujiandikie wimbo huu, uwafundishe Waisraeli na uwaamuru wauimbe, ili upate kuwa ushahidi wangu dhidi yao.
Et maintenant écrivez ce cantique, et apprends-le aux enfants d'Israël, mets-le dans leur bouche, afin que ce cantique me serve de témoin contre les enfants d'Israël.
20 Nitakapokwisha kuwaingiza katika nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo, nao watakapokula wakashiba na kufanikiwa, watageukia miungu mingine na kuiabudu, wakinikataa mimi na kuvunja Agano langu.
Car je les introduirai dans le pays que j'ai promis par serment à leurs pères, pays découlant de lait et de miel; puis ils mangeront et se rassasieront et s'engraisseront et se tourneront vers d'autres dieux et les serviront et me mépriseront et rompront mon alliance,
21 Maafa na shida zitakapokuja juu yao, wimbo huu utashuhudia dhidi yao, kwa sababu hautasahauliwa na wazao wao. Ninajua lile wanaloandaa kufanya, hata kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo.”
et quand alors ils seront atteints par beaucoup de maux et de détresses, que ce cantique dépose contre eux comme un témoin, car il ne doit ni être oublié, ni cesser d'être dans la bouche de leurs descendants. En effet, je connais leurs pensées qu'ils forment dès à présent, avant que je les aie introduits dans le pays que je leur ai promis par serment.
22 Hivyo Mose akaandika wimbo huu siku ile na akawafundisha Waisraeli.
Moïse écrivit donc ce cantique ce jour-là, et il l'apprit aux enfants d'Israël.
23 Bwana akampa Yoshua mwana wa Nuni agizo hili: “Uwe hodari na shujaa, kwa kuwa utawaleta Waisraeli katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo, nami mwenyewe nitakuwa pamoja nawe.”
Et il donna ses instructions à Josué, fils de Nun, en ces termes: Aie courage et fermeté, car c'est toi qui introduiras les enfants d'Israël dans le pays que je leur ai promis par serment, et Moi-même Je serai avec toi.
24 Baada ya Mose kumaliza kuandika kwenye kitabu maneno ya sheria hii kutoka mwanzo hadi mwisho,
Et lorsque Moïse eut achevé de transcrire sur un volume les paroles de cette Loi, au complet,
25 akawapa Walawi wale waliolibeba Sanduku la Agano la Bwana agizo hili, akawaambia:
Moïse fit cette injonction aux Lévites, porteurs de l'Arche de l'alliance de l'Éternel:
26 “Chukueni Kitabu hiki cha Sheria mkakiweke kando ya Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu. Hapo ndipo kitakapokaa kama shahidi dhidi yenu.
Prenez ce Volume de la Loi et le placez à côté de l'Arche de l'alliance de l'Éternel, votre Dieu, et qu'il y serve de témoin contre vous.
27 Kwa kuwa ninajua jinsi mlivyo waasi na mlivyo na shingo ngumu. Kama mmekuwa mkiasi dhidi ya Bwana nikiwa bado niko hai na nikiwa pamoja nanyi, mtaasi mara ngapi baada ya kufa kwangu!
Car je connais ton caractère rebelle, et la roideur de ton col; voici, pendant que je suis encore vivant à vos côtés, déjà vous vous montrez rebelles à l'Éternel: combien plus le serez-vous après ma mort!
28 Kusanyeni mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na maafisa wenu wote, ili nipate kusema maneno haya masikioni mwao na kuziita mbingu na nchi ili kushuhudia dhidi yao.
Assemblez auprès de moi tous les Anciens de vos Tribus, et vos Officiers, afin que je redise à leurs oreilles ces choses-là, et que je prenne à témoin contre eux les Cieux et la terre.
29 Kwa kuwa ninajua baada ya kifo changu hakika mtakuwa waovu kabisa na kugeuka kutoka njia niliyowaamuru ninyi. Katika siku zijazo, maafa yatawapata kwa sababu mtafanya maovu mbele ya macho ya Bwana, na kuchochea hasira yake kwa yale mikono yenu itakayokuwa imefanya.”
Car je sais qu'après ma mort vous vous perdrez et quitterez la voie que je vous ai tracée, et que les maux fondront sur vous dans les temps à venir, parce que vous ferez ce qui est mal aux yeux de l'Éternel pour le provoquer par l'œuvre de vos mains.
30 Mose akayasoma maneno ya wimbo huu kutoka mwanzo hadi mwisho katika masikio ya kusanyiko lote la Israeli:
Moïse prononça donc aux oreilles de toute l'Assemblée d'Israël les paroles de ce cantique dans leur entier:

< Torati 31 >