< Torati 31 >
1 Kisha Mose akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote:
Then Moses went and spake these wordes vnto all Israel,
2 “Sasa nina miaka mia moja na ishirini nami siwezi tena kuwaongoza. Bwana ameniambia, ‘Hutavuka Yordani.’
And said vnto them, I am an hundreth and twentie yeere olde this day: I can no more goe out and in: also the Lord hath saide vnto me, Thou shalt not goe ouer this Iorden.
3 Bwana Mungu wenu, yeye mwenyewe atavuka mbele yenu. Ataangamiza mataifa haya mbele yenu, nanyi mtaimiliki nchi yao. Pia Yoshua atavuka mbele yenu, kama Bwana alivyosema.
The Lord thy God he will go ouer before thee: he will destroy these nations before thee, and thou shalt possesse them. Ioshua, he shall goe before thee, as the Lord hath said.
4 Naye Bwana atawafanyia watu hao kile alichowafanyia Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, ambao aliwaangamiza pamoja na nchi yao.
And the Lord shall doe vnto them, as he did to Sihon and to Og Kings of the Amorites: and vnto their lande whome he destroyed.
5 Bwana atawakabidhi kwenu, nanyi lazima mwatendee yale yote niliyowaamuru.
And the Lord shall giue them before you that ye may do vnto them according vnto euery commandement, which I haue comanded you.
6 Kuweni imara na moyo wa ushujaa. Msiogope wala msifadhaike kwa sababu yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu anakwenda pamoja nanyi; kamwe hatawaacha wala hatawatupa ninyi.”
Plucke vp your hearts therefore, and be strong: dread not, nor be afraid of them: for the Lord thy God him selfe doeth goe with thee: he will not faile thee, nor forsake thee.
7 Kisha Mose akamwita Yoshua na akamwambia mbele ya Israeli wote, “Uwe imara na moyo wa ushujaa, kwa kuwa ni lazima uende na watu hawa katika nchi ile Bwana aliyowaapia baba zao kuwapa, nawe ni lazima uwagawie kama urithi wao.
And Moses called Ioshua, and said vnto him in the sight of all Israel, Be of a good courage and strong: for thou shalt go with this people vnto the lande which the Lord hath sworne vnto their fathers, to giue them, and thou shalt giue it them to inherite.
8 Bwana mwenyewe atakutangulia naye atakuwa pamoja nawe; kamwe hatakuacha wala hatakutupa. Usiogope, wala usifadhaike.”
And the Lord him selfe doeth go before thee: he will be with thee: he will not faile thee, neither forsake thee: feare not therefore, nor be discomforted.
9 Kwa hiyo Mose akaandika sheria hii na kuwapa makuhani, wana wa Lawi, waliochukua Sanduku la Agano la Bwana na wazee wote wa Israeli.
And Moses wrote this Lawe, and deliuered it vnto the Priestes the sonnes of Leui (which bare the Arke of the couenant of the Lord) and vnto all the Elders of Israel,
10 Kisha Mose akawaamuru, akasema: “Mwishoni mwa kila miaka saba, katika mwaka wa kufuta madeni, wakati wa Sikukuu ya Vibanda,
And Moses commanded them, saying, Euery seuenth yeere when the yeere of freedome shalbe in the feast of the Tabernacles:
11 Waisraeli wote wanapokuja mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua, utasoma sheria hii mbele yao masikioni mwao.
When all Israel shall come to appeare before the Lord thy God, in the place which he shall chuse, thou shalt reade this Lawe before all Israel that they may heare it.
12 Kusanya watu wote, wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, ili waweze kusikia na kujifunza kumcha Bwana Mungu wenu na kufuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii.
Gather the people together: men, and women, and children, and thy stranger that is within thy gates, that they may heare, and that they may learne, and feare the Lord your God, and keepe and obserue all the wordes of this Lawe,
13 Watoto wao, ambao hawaijui sheria hii, lazima waisikie na kujifunza kumcha Bwana Mungu wenu kwa muda mtakaoishi katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”
And that their children which haue not knowen it, may heare it, and learne to feare the Lord your God, as long as ye liue in the lande, whither ye goe ouer Iorden to possesse it.
14 Bwana akamwambia Mose, “Sasa siku ya kifo chako imekaribia. Mwite Yoshua, mkajihudhurishe katika Hema la Kukutania, mahali nitakapompa maagizo ya kazi.” Kwa hiyo Mose na Yoshua wakaja na kujihudhurisha kwenye Hema la Kukutania.
Then the Lord saide vnto Moses, Beholde, thy dayes are come, that thou must die: Call Ioshua, and stande ye in the Tabernacle of the Congregation that I may giue him a charge. So Moses and Ioshua went, and stoode in the Tabernacle of the Congregation.
15 Kisha Bwana akatokea katika Hema katika nguzo ya wingu, nalo wingu likasimama juu ya ingilio la Hema.
And the Lord appeared in the Tabernacle, in the pillar of a cloude: and the pillar of the cloude stoode ouer the doore of the Tabernacle.
16 Kisha Bwana akamwambia Mose: “Unakwenda kupumzika na baba zako, nao watu hawa hivi karibuni watazini na miungu migeni ya nchi wanayoingia. Wataniacha na kuvunja Agano nililofanya nao.
And the Lord said vnto Moses, Behold, thou shalt sleepe with thy fathers, and this people will rise vp, and goe a whoring after the gods of a strange land (whither they goe to dwell therein) and will forsake me, and breake my couenant which I haue made with them.
17 Siku hiyo nitawakasirikia na kuwaacha; nitawaficha uso wangu, nao wataangamizwa. Maafa mengi na shida nyingi zitakuja juu yao, nao siku hiyo watauliza, ‘Je, maafa haya hayakuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko pamoja nasi?’
Wherefore my wrath will waxe hote against them at that day, and I will forsake them, and will hide my face from them: then they shalbe consumed, and many aduersities and tribulations shall come vpon them: so then they will say, Are not these troubles come vpon me, because God is not with me?
18 Nami hakika nitauficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yao yote kwa kugeukia miungu mingine.
But I will surely hide my face in that day, because of all the euill, which they shall commit, in that they are turned vnto other gods.
19 “Sasa ujiandikie wimbo huu, uwafundishe Waisraeli na uwaamuru wauimbe, ili upate kuwa ushahidi wangu dhidi yao.
Now therefore write ye this song for you, and teach it the children of Israel: put it in their mouthes, that this song may be my witnesse against the children of Israel.
20 Nitakapokwisha kuwaingiza katika nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo, nao watakapokula wakashiba na kufanikiwa, watageukia miungu mingine na kuiabudu, wakinikataa mimi na kuvunja Agano langu.
For I will bring them into the land (which I sware vnto their fathers) that floweth with milke and honie, and they shall eate, and fil them selues, and waxe fat: then shall they turne vnto other gods, and serue them, and contemne me, and breake my couenant.
21 Maafa na shida zitakapokuja juu yao, wimbo huu utashuhudia dhidi yao, kwa sababu hautasahauliwa na wazao wao. Ninajua lile wanaloandaa kufanya, hata kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo.”
And then when many aduersities and tribulations shall come vpon them, this song shall answere them to their face as a witnesse: for it shall not be forgotte out of the mouthes of their posteritie: for I knowe their imagination, which they goe about euen now, before I haue brought them into the lande which I sware.
22 Hivyo Mose akaandika wimbo huu siku ile na akawafundisha Waisraeli.
Moses therefore wrote this song the same day and taught it the children of Israel.
23 Bwana akampa Yoshua mwana wa Nuni agizo hili: “Uwe hodari na shujaa, kwa kuwa utawaleta Waisraeli katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo, nami mwenyewe nitakuwa pamoja nawe.”
And God gaue Ioshua the sonne of Nun a charge, and said, Be strong, and of a good courage: for thou shalt bring the children of Israel into the lande, which I sware vnto them, and I will be with thee.
24 Baada ya Mose kumaliza kuandika kwenye kitabu maneno ya sheria hii kutoka mwanzo hadi mwisho,
And when Moses had made an ende of writing the wordes of this Lawe in a booke vntill he had finished them,
25 akawapa Walawi wale waliolibeba Sanduku la Agano la Bwana agizo hili, akawaambia:
Then Moses commanded the Leuites, which bare the Arke of the couenant of the Lord, saying,
26 “Chukueni Kitabu hiki cha Sheria mkakiweke kando ya Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu. Hapo ndipo kitakapokaa kama shahidi dhidi yenu.
Take the booke of this Lawe, and put ye it in the side of the Arke of the couenant of the Lord your God, that it may be there for a witnes against thee.
27 Kwa kuwa ninajua jinsi mlivyo waasi na mlivyo na shingo ngumu. Kama mmekuwa mkiasi dhidi ya Bwana nikiwa bado niko hai na nikiwa pamoja nanyi, mtaasi mara ngapi baada ya kufa kwangu!
For I knowe thy rebellion and thy stiffe necke: beholde, I being yet aliue with you this day, ye are rebellious against the Lord: howe much more then after my death?
28 Kusanyeni mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na maafisa wenu wote, ili nipate kusema maneno haya masikioni mwao na kuziita mbingu na nchi ili kushuhudia dhidi yao.
Gather vnto me all the Elders of your tribes, and your officers, that I may speake these wordes in their audience, and call heauen and earth to recorde against them.
29 Kwa kuwa ninajua baada ya kifo changu hakika mtakuwa waovu kabisa na kugeuka kutoka njia niliyowaamuru ninyi. Katika siku zijazo, maafa yatawapata kwa sababu mtafanya maovu mbele ya macho ya Bwana, na kuchochea hasira yake kwa yale mikono yenu itakayokuwa imefanya.”
For I am sure that after my death ye will vtterly be corrupt and turne from the way, which I haue commanded you: therefore euill will come vpon you at the length, because ye will comit euill in the sight of the Lord, by prouoking him to anger through the worke of your hands.
30 Mose akayasoma maneno ya wimbo huu kutoka mwanzo hadi mwisho katika masikio ya kusanyiko lote la Israeli:
Thus Moses spake in the audience of all the congregation of Israel the wordes of this song, vntill he had ended them.