< Torati 30 >
1 Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa,
“I have now told you about the ways that Yahweh our God will bless you [if you obey him] and the ways that he will curse you [if you disobey him]. I am saying that you must choose which you want. But when [you choose not to obey his laws], some day you will be living in the countries to which he will scatter you, and you will remember [what I told you].
2 hapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo,
Then, if you return to Yahweh our God and faithfully [IDM] obey all that I have today commanded you to do,
3 ndipo Bwana Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya.
he will be merciful to you. He will bring you back from the nations to which he scattered you, and he will cause you to be prosperous again.
4 Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mungu wako atakukusanya na kukurudisha.
Even if you have been scattered to the most distant places on the earth, Yahweh our God will gather you from there and bring you back [to your land].
5 Yeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako.
He will enable you to possess again the land where your ancestors lived. And he will cause you to be more prosperous and more numerous than you are now.
6 Bwana Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi.
Yahweh our God will change [MET] your inner beings, with the result that you will love him more than you love anything else and want to do only what he wants you to do. And then you will continue to live in that land.
7 Bwana Mungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa.
Yahweh our God will cause your enemies and those who oppressed/persecuted you to experience all the disasters that I have told you about.
8 Utamtii tena Bwana na kuzishika amri zake zote ninazokupa leo.
You will do what Yahweh wants you to do, as you did before, and you will obey all the commands that I have given to you today.
9 Ndipo Bwana Mungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako. Bwana atakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako,
Yahweh our God will cause you to be very successful in all that you do. You will have many children [IDM], and a lot of cattle, and you will have abundant crops. He will again be happy to enable you to prosper, just like he was happy to enable your ancestors to prosper.
10 kama ukimtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
[But he will do those things only] if you do what he has told you to do, and if you obey all his rules and regulations that I have written about [in this scroll], and if you will love him more than you love anything else and want to do only what he wants you to do.
11 Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza.
The commands that I am giving to you today are not very difficult for you [to obey], and they are not [difficult to know].
12 Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?”
They are not in heaven, with the result that you need to say, ‘(Who will need to go up to heaven for us to bring them [down here to us] in order that we can hear them and obey them?/Someone will need to go up to heaven for us to bring them [down here to us] in order that we can hear them and obey them.)’ [RHQ]
13 Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?”
And they are not on the other side of the sea, with the result that you need to say, ‘(Who will need to cross the sea for us and bring them back to us, in order that we can hear them and obey them?/Someone will need to cross the sea for us and bring them back to us, in order that we can hear them and obey them.)’ [RHQ]
14 La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.
[You do not need to do that because] his commands are here with you. You know them [MTY] and you have (memorized them/put them in your minds). So you can [easily] obey them.
15 Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo.
So listen! Today I am allowing you to choose between [doing what is] evil and [doing what is] good, between what will enable you to live [for a long time] and [what will cause you] to die [while you are still young].
16 Ninakuamuru leo kwamba umpende Bwana Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.
[I say again], if you obey the commands of Yahweh our God that I am giving to you today, and if you love him and conduct your lives as he wants you to do, and if you obey all his rules and regulations, you will prosper and become very numerous, and Yahweh our God will bless you in the land that you are about to enter and possess.
17 Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu,
But if you turn away [from Yahweh] and refuse to heed what he says, and if you allow yourselves to be led away to worship other gods,
18 nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.
I am warning you today that you will [soon] die. You will not live for a long time in the land that you are about to cross the Jordan [River] to enter and possess.
19 Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi,
I am requesting that [everyone in] heaven and the earth testify to you, that today I am allowing you to choose whether you [want to] live for a long time or to soon die, whether [you want Yahweh to] bless you or to curse you. So choose to live.
20 na ili upate kumpenda Bwana Mungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwa Bwana ndiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.
[Choose to] love Yahweh our God, and to obey him [MTY], and to (be faithful to/have a close relationship with) him. If you do that, you and your descendants will live for a long time in the land that Yahweh solemnly promised to your ancestors Abraham, Isaac, and Jacob, that he would give to them.”