< Torati 30 >
1 Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa,
It shall happen, when all these things have come on you, the blessing and the curse, which I have set before you, and you shall call them to mind among all the nations, where Adonai your God has driven you,
2 hapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo,
and teshuvah ·completely return· to Adonai your God, and sh'ma ·hear obey· his voice according to all that I enjoin you today, you and your children, with all your heart, and with all your soul;
3 ndipo Bwana Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya.
that then Adonai your God will release you from captivity, have racham ·compassionate love· on you, and will make teshuvah ·complete return· and gather you from all the peoples where Adonai your God has scattered you.
4 Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mungu wako atakukusanya na kukurudisha.
If your outcasts are in the uttermost parts of the heavens, from there Adonai your God will gather you, and from there he will bring you back.
5 Yeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako.
Adonai your God will bring you into the land which your fathers possessed, and you will possess it. He will do you good, and increase your numbers more than your fathers.
6 Bwana Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi.
Adonai your God will circumcise your heart, and the heart of your offspring, to 'ahav ·affectionately love· Adonai your God with all your heart, and with all your soul, that you may live.
7 Bwana Mungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa.
Adonai your God will put all these curses on your enemies, and on those who hate you, who persecuted you.
8 Utamtii tena Bwana na kuzishika amri zake zote ninazokupa leo.
You shall make teshuvah ·complete return· and sh'ma ·hear obey· Adonai’s voice, and do all his mitzvot ·instructions· which I enjoin you today.
9 Ndipo Bwana Mungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako. Bwana atakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako,
Adonai your God will make you plenteous in all the work of your hand, in the fruit of your body, in the fruit of your livestock, and in the fruit of your ground, for good; for Adonai will again rejoice over you for good, as he rejoiced over your fathers;
10 kama ukimtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.
if you will sh'ma ·hear obey· Adonai your God’s voice, to keep his mitzvot ·instructions· and his statutes which are written in this book of the Torah ·Teaching·; if you turn to Adonai your God with all your heart, and with all your soul.
11 Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza.
For this mitzvah ·instruction· which I enjoin you today is not too hard for you or too distant.
12 Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?”
It is not in heaven, so that you should say, “Who will go up for us to heaven, and bring it to us, that we may sh'ma ·hear obey· it, so we may do it?”
13 Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?”
Neither is it beyond the sea, that you should say, “Who will go over the sea for us, and bring it to us, that we may that we may sh'ma ·hear obey· it, so it, so we may do it?”
14 La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.
But the word is very near to you, in your mouth and in your heart, that you may do it.
15 Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo.
Behold, I have set before you today life and prosperity, and death and evil.
16 Ninakuamuru leo kwamba umpende Bwana Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.
For I enjoin you today to 'ahav ·affectionately love· Adonai your God, to walk in his ways, and to keep his mitzvot ·instructions·, his statutes, and his judgments, that you may live and multiply, and that Adonai your God may bless you in the land where you go in to possess it.
17 Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu,
But if your heart turns away, and you will not sh'ma ·hear obey·, but are drawn away, and hawa ·bow low, prostrate· to worship other deities, and abad ·serve· them;
18 nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.
I denounce to you today, that you will surely perish. You will not prolong your days in the land where you pass over the Jordan [Descender] to go in to possess it.
19 Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi,
I call heaven and earth to witness against you today, that I have set before you life and death, the blessing and the curse. Therefore choose life, that you may live, you and your descendants;
20 na ili upate kumpenda Bwana Mungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwa Bwana ndiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.
to 'ahav ·affectionately love· Adonai your God, to sh'ma ·hear obey· his voice, and to dabak ·cling to, worship· him; for he is your life, and the length of your days; that you may dwell in the land which Adonai swore to your fathers, to Abraham [Father of a multitude], to Isaac [Laughter], and to Jacob [Supplanter], to give them.