< Torati 3 >
1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
Então nos viramos, e subimos o caminho para Bashan. Og o rei de Bashan saiu contra nós, ele e todo o seu povo, para lutar em Edrei.
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
Yahweh me disse: “Não o temam, pois eu o entreguei, com todo o seu povo e sua terra, em suas mãos”. Far-lhe-eis como fizestes a Sihon, rei dos amorreus, que viveu em Heshbon”.
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
Então Yahweh nosso Deus também entregou em nossas mãos Og, o rei de Basã, e todo o seu povo. Nós o golpeamos até que ninguém mais ficou para ele.
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
Levamos todas as suas cidades naquela época. Não havia uma cidade que não tivéssemos tomado deles: sessenta cidades, toda a região de Argob, o reino de Og em Bashan.
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
Todas estas eram cidades fortificadas com muros altos, portões e bares, além de um grande número de vilarejos sem muros.
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
Nós as destruímos completamente, como fizemos com Sihon, rei de Heshbon, destruindo completamente todas as cidades habitadas, com as mulheres e os pequenos.
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
Mas todo o gado, e o saque das cidades, nós tomamos por saque para nós mesmos.
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
Tiramos a terra naquela época da mão dos dois reis dos Amoritas que estavam além do Jordão, desde o vale do Arnon até o Monte Hermon.
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
(Os Sidônios chamam de Hermon Sirion, e os Amoritas de Senir.)
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
Tomamos todas as cidades da planície, e toda Gilead, e todo Bashan, para Salecah e Edrei, cidades do reino de Og em Bashan.
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
(Pois somente Og rei de Bashan permaneceu do remanescente do Rephaim. Eis que seu leito era um leito de ferro. Não é em Rabbah das crianças de Ammon? Nove côvados era seu comprimento, e quatro côvados sua largura, depois do côvado de um homem).
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
Esta terra que tomamos em posse naquela época: de Aroer, que fica junto ao vale do Arnon, e metade da região montanhosa de Gilead com suas cidades, eu dei aos rubenitas e aos gaditas;
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
e o resto de Gilead, e todo Bashan, o reino de Og, eu dei à meia tribo de Manasse - toda a região de Argob, mesmo todo Bashan. (O mesmo é chamado de terra de Rephaim.
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Jair, filho de Manassés, levou toda a região de Argob, até a fronteira dos geshuritas e dos maacathitas, e os chamou, até hoje, até mesmo Bashan, segundo seu próprio nome, Havvoth Jair).
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
Eu dei Gilead a Machir.
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
Aos Reubenitas e aos Gaditas dei desde Gilead até o vale do Arnon, o meio do vale, e sua fronteira, até o rio Jabbok, que é a fronteira das crianças de Ammon;
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
o Arabah também, e o Jordão e sua fronteira, desde Chinnereth até o mar do Arabah, o Mar Salgado, sob as encostas de Pisgah a leste.
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
Eu lhe ordenei naquela época, dizendo: “Yahweh seu Deus lhe deu esta terra para possuí-la”. Todos vocês, homens de valor, passarão armados diante de seus irmãos, os filhos de Israel”.
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
Mas suas esposas, e seus pequenos, e seu gado (eu sei que vocês têm muito gado), viverão em suas cidades que eu lhes dei,
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
até que Javé dê descanso a seus irmãos, como a vocês, e eles também possuam a terra que Javé seu Deus lhes dá além do Jordão. Então cada um de vós voltará à sua própria posse, que eu vos dei”.
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
Comandei Josué naquela época, dizendo: “Seus olhos viram tudo o que Yahweh seu Deus fez a estes dois reis. Assim fará Javé com todos os reinos por onde passas.
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
Não os temerás; pois Yavé, teu próprio Deus, luta por ti”.
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
Eu implorei a Javé naquela época, dizendo:
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
“Senhor Javé, começou a mostrar a seu servo sua grandeza, e sua mão forte. Pois que deus existe no céu ou na terra que pode fazer obras como a sua, e que age poderosamente como a sua?
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
Por favor, deixe-me ir e ver a boa terra que está além do Jordão, aquela bela montanha e o Líbano”.
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
Mas Javé ficou bravo comigo por causa de você, e não me ouviu. Yahweh me disse: “Já chega! Não fale mais comigo sobre este assunto.
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
Suba até o topo de Pisgah, e levante seus olhos para o oeste, e para o norte, e para o sul, e para o leste, e veja com seus olhos; pois você não deve passar por este Jordão.
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
Mas encomenda Josué, e anima-o, e fortalece-o; porque ele passará diante deste povo, e ele o fará herdar a terra que vereis”.
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
Assim ficamos no vale perto de Beth Peor.