< Torati 3 >

1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
Alors nous nous tournâmes, et nous montâmes par le chemin de Basan, et Hog le Roi de Basan sortit contre nous, avec tout son peuple pour combattre à Edréhi.
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
Et l'Eternel me dit: Ne le crains point, car je l'ai livré entre tes mains, lui et tout son peuple, et son pays, et tu lui feras comme tu as fait a Sihon, Roi des Amorrhéens qui demeurait à Hesbon.
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
Ainsi l'Eternel notre Dieu livra aussi entre nos mains Hog le Roi de Basan, et tout son peuple, et nous le battîmes tellement que nous ne lui laissâmes personne de reste.
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
En ce même temps nous prîmes aussi toutes ses villes; [et] il n'y eut point de villes que nous ne lui prissions, [savoir] soixante villes, tout le pays d'Argob du royaume de Hog en Basan.
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
Toutes ces villes-là étaient closes de hautes murailles, de portes et de barres, et outre cela il y avait des villes non murées en fort grand nombre.
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
Et nous les détruisîmes à la façon de l'interdit, comme nous avions fait à Sihon, Roi de Hesbon, détruisant à la façon de l'interdit, toutes les villes, les hommes, les femmes, et les petits enfants.
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
Mais nous pillâmes pour nous toutes les bêtes, et le butin des villes.
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
Nous prîmes donc en ce temps-là le pays des deux Rois des Amorrhéens, qui étaient au deçà du Jourdain, depuis le torrent d'Arnon jusqu'à la montagne de Hermon.
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
[Or] les Sidoniens appellent Hermon, Sirjon; mais les Amorrhéens le nomment Sénir.
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
Toutes les villes du plat pays et tout Galaad, et tout Basan jusqu'à Salca et Edréhi, les villes du Royaume de Hog en Basan.
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
Car Hog Roi de Basan était demeuré seul de reste des Réphaïms. Voici, son lit, qui est un lit de fer, n'est-il pas dans Rabba des enfants de Hammon? sa longueur est de neuf coudées, et sa largeur de quatre coudées, de coudée d'homme.
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
En ce temps-là donc nous possédâmes ce pays-là; [et] je donnai aux Rubénites et aux Gadites ce qui est depuis Haroher, qui est sur le torrent d'Arnon, et la moitié de la montagne de Galaad, avec ses villes.
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
Et je donnai à la demi-Tribu de Manassé le reste de Galaad, et tout Basan, qui était le Royaume de Hog; toute la contrée d'Argob par tout Basan, était appelée le pays des Réphaïms.
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Jaïr fils de Manassé prit toute la contrée d'Argob, jusqu'à la frontière des Guésuriens et des Mahacathiens, et il appela de son Nom ce pays de Basan, bourgs de Jaïr, lequel ils ont eu jusqu'à aujourd'hui.
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
Je donnai aussi Galaad à Makir.
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
Mais je donnai aux Rubénites et aux Gadites, depuis Galaad jusqu'au torrent d'Arnon, ce qui est enfermé par le torrent, et ses limites jusqu'au torrent de Jabbok, qui est la frontière des enfants de Hammon;
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
Et la campagne, et le Jourdain, et [ses] confins depuis Kinnéreth jusqu'à la mer de la campagne, qui est la mer salée, au dessous d'Asdoth de Pisgar vers l'Orient.
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
Or en ce temps-là je vous commandai, en disant: L'Eternel votre Dieu vous a donné ce pays pour le posséder, vous tous qui êtes vaillants, passez tous armés devant vos frères les enfants d'Israël.
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
Que seulement vos femmes, vos petits enfants, et votre bétail, [car] je sais que vous avez beaucoup de bétail, demeurent dans les villes que je vous ai données.
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
Jusqu'à ce que l'Eternel ait donné du repos à vos frères comme à vous, et qu'eux aussi possèdent le pays que l'Eternel votre Dieu leur va donner au delà du Jourdain; puis vous retournerez chacun en sa possession, laquelle je vous ai donnée.
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
En ce temps-là aussi je commandai à Josué, en disant: Tes yeux ont vu tout ce que l'Eternel votre Dieu a fait à ces deux Rois; l'Eternel en fera de même à tous les Royaumes vers lesquels tu vas passer.
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
Ne les craignez point; car l'Eternel votre Dieu combat lui-même pour vous.
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
En ce même temps aussi je demandai grâce à l'Eternel, en disant:
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
Seigneur Eternel, tu as commencé de montrer à ton serviteur ta grandeur et ta main forte; car qui est le [Dieu] Fort au ciel et sur la terre qui puisse faire des œuvres comme les tiennes, et [dont la force soit] comme tes forces?
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
Que je passe, je te prie, et que je voie le bon pays qui est au delà du Jourdain, cette bonne montagne, c'est à savoir, le Liban.
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
Mais l'Eternel était fort irrité contre moi à cause de vous, et ne m'exauça point; mais il me dit: C'est assez, ne me parle plus de cette affaire.
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
Monte au sommet de cette colline, et élève tes yeux vers l'Occident, et le Septentrion, vers le Midi, et l'Orient, et regarde de tes yeux; car tu ne passeras point ce Jourdain.
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
Mais donnes-en la charge à Josué, et le fortifie, et le renforce; car c'est lui qui passera devant ce peuple, et qui les mettra en possession du pays que tu auras vu.
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
Ainsi nous sommes demeurés en cette vallée vis à viss de Beth-Péhor.

< Torati 3 >