< Torati 3 >

1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
Then we turned, and went up the way to Bashan: and Og the king of Bashan came out against us, he and all his people, to battle at Edrei.
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
And the LORD said to me, Fear him not: for I will deliver him, and all his people, and his land, into thy hand; and thou shalt do to him as thou didst to Sihon king of the Amorites, who dwelt at Heshbon.
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
So the LORD our God delivered into our hands Og also the king of Bashan, and all his people: and we smote him until none was left to him remaining.
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
And we took all his cities at that time, there was not a city which we took not from them, sixty cities, all the region of Argob, the kingdom of Og in Bashan.
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
All these cities [were] fortified with high walls, gates, and bars; besides unwalled towns a great number.
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
And we utterly destroyed them, as we did to Sihon king of Heshbon, utterly destroying the men, women, and children of every city.
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
But all the cattle, and the spoil of the cities, we took for a prey to ourselves.
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
And we took at that time out of the hand of the two kings of the Amorites the land that [was] on this side of Jordan, from the river of Arnon to mount Hermon;
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
([Which] Hermon the Sidonians call Sirion; and the Amorites call it Shenir; )
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
All the cities of the plain, and all Gilead, and all Bashan, to Salchah and Edrei, cities of the kingdom of Og in Bashan.
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
For only Og king of Bashan remained of the remnant of giants; behold, his bedstead [was] a bedstead of iron; [is] it not in Rabbath of the children of Ammon? nine cubits [was] the length of it, and four cubits the breadth of it, after the cubit of a man.
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
And this land, [which] we possessed at that time, from Aroer, which [is] by the river Arnon, and half mount Gilead, and its cities, I gave to the Reubenites and to the Gadites.
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
And the rest of Gilead, and all Bashan, [being] the kingdom of Og, I gave to the half-tribe of Manasseh; all the region of Argob, with all Bashan, which was called the land of giants.
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Jair the son of Manasseh took all the country of Argob, to the borders of Geshuri, and Maachathi; and called them after his own name, Bashan-havoth-jair, to this day.
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
And I gave Gilead to Machir.
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
And to the Reubenites and to the Gadites I gave from Gilead even to the river Arnon half the valley, and the border even to the river Jabbok, [which is] the border of the children of Ammon:
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
The plain also, and Jordan, and the coast [of it], from Chinnereth even to the sea of the plain, [even] the salt-sea, under Ashdoth-pisgah eastward.
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
And I commanded you at that time, saying, The LORD your God hath given you this land to possess it; ye shall pass over armed before your brethren the children of Israel, all [that are] meet for the war.
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
But your wives, and your little ones, and your cattle, ([for] I know that ye have many cattle, ) shall abide in your cities which I have given you;
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
Until the LORD shall have given rest to your brethren, as well as to you, and [until] they also possess the land which the LORD your God hath given them beyond Jordan: and [then] shall ye return every man to his possession which I have given you.
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
And I commanded Joshua at that time, saying, Thy eyes have seen all that the LORD your God hath done to these two kings: so shall the LORD do to all the kingdoms whither thou passest.
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
Ye shall not fear them: for the LORD your God he shall fight for you.
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
And I besought the LORD at that time, saying,
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
O LORD God, thou hast begun to show thy servant thy greatness, and thy mighty hand: for what God [is there] in heaven or in earth, that can do according to thy works, and according to thy might?
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
I pray thee, let me go over, and see the good land that [is] beyond Jordan, that goodly mountain, and Lebanon.
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
But the LORD was wroth with me for your sakes, and would not hear me: and the LORD said to me, Let it suffice thee; speak no more to me of this matter.
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
Ascend to the top of Pisgah, and lift up thy eyes westward, and northward, and southward, and eastward, and behold with thy eyes: for thou shalt not go over this Jordan.
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
But charge Joshua, and encourage him, and strengthen him: for he shall go over before this people, and he shall cause them to inherit the land which thou shalt see.
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
So we abode in the valley over against Beth-peor.

< Torati 3 >