< Torati 3 >

1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
and to turn and to ascend: rise way: road [the] Bashan and to come out: come Og king [the] Bashan to/for to encounter: toward us he/she/it and all people his to/for battle Edrei
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
and to say LORD to(wards) me not to fear [obj] him for in/on/with hand: power your to give: give [obj] him and [obj] all people his and [obj] land: country/planet his and to make: do to/for him like/as as which to make: do to/for Sihon king [the] Amorite which to dwell in/on/with Heshbon
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
and to give: give LORD God our in/on/with hand: power our also [obj] Og king [the] Bashan and [obj] all people his and to smite him till lest to remain to/for him survivor
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
and to capture [obj] all city his in/on/with time [the] he/she/it not to be town which not to take: take from with them sixty city all cord Argob kingdom Og in/on/with Bashan
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
all these city to gather/restrain/fortify wall high door and bar to/for alone: besides from city [the] villager to multiply much
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
and to devote/destroy [obj] them like/as as which to make: do to/for Sihon king Heshbon to devote/destroy all city man [the] woman and [the] child
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
and all [the] animal and spoil [the] city to plunder to/for us
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
and to take: take in/on/with time [the] he/she/it [obj] [the] land: country/planet from hand: power two king [the] Amorite which in/on/with side: beyond [the] Jordan from torrent: valley Arnon till mountain: mount (Mount) Hermon
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
Sidonian to call: call by to/for (Mount) Hermon Sirion and [the] Amorite to call: call by to/for him Senir
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
all city [the] plain and all [the] Gilead and all [the] Bashan till Salecah and Edrei city kingdom Og in/on/with Bashan
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
for except Og king [the] Bashan to remain from remainder [the] Rephaim behold bed his bed iron not he/she/it in/on/with Rabbah son: descendant/people Ammon nine cubit length her and four cubit width her in/on/with cubit man
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
and [obj] [the] land: country/planet [the] this to possess: take in/on/with time [the] he/she/it from Aroer which upon torrent: valley Arnon and half mountain: hill country [the] Gilead and city his to give: give to/for Reubenite and to/for Gad
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
and remainder [the] Gilead and all [the] Bashan kingdom Og to give: give to/for half tribe [the] Manasseh all cord [the] Argob to/for all [the] Bashan [the] he/she/it to call: call by land: country/planet Rephaim
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Jair son: descendant/people Manasseh to take: take [obj] all cord Argob till border: boundary [the] Geshurite and [the] Maacathite and to call: call by [obj] them upon name his [obj] [the] Bashan Havvoth-jair Havvoth-jair till [the] day: today [the] this
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
and to/for Machir to give: give [obj] [the] Gilead
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
and to/for Reubenite and to/for Gad to give: give from [the] Gilead and till torrent: valley Arnon midst [the] torrent: valley and border: boundary and till Jabbok [the] torrent: river border: boundary son: descendant/people Ammon
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
and [the] Arabah and [the] Jordan and border: boundary from (Sea of) Chinnereth and till sea [the] Arabah sea [the] Salt (Sea) underneath: under Slopes (of Pisgah) [the] Pisgah east [to]
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
and to command [obj] you in/on/with time [the] he/she/it to/for to say LORD God your to give: give to/for you [obj] [the] land: country/planet [the] this to/for to possess: take her to arm to pass to/for face: before brother: compatriot your son: descendant/people Israel all son: descendant/people strength
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
except woman: wife your and child your and livestock your to know for livestock many to/for you to dwell in/on/with city your which to give: give to/for you
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
till which to rest LORD to/for brother: compatriot your like/as you and to possess: take also they(masc.) [obj] [the] land: country/planet which LORD God your to give: give to/for them in/on/with side: beyond [the] Jordan and to return: return man: anyone to/for possession his which to give: give to/for you
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
and [obj] Joshua to command in/on/with time [the] he/she/it to/for to say eye your [the] to see: see [obj] all which to make: do LORD God your to/for two [the] king [the] these so to make: do LORD to/for all [the] kingdom which you(m. s.) to pass there [to]
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
not to fear them for LORD God your he/she/it [the] to fight to/for you
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
and be gracious to(wards) LORD in/on/with time [the] he/she/it to/for to say
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
Lord YHWH/God you(m. s.) to profane/begin: begin to/for to see: see [obj] servant/slave your [obj] greatness your and [obj] hand: power your [the] strong which who? God in/on/with heaven and in/on/with land: country/planet which to make: do like/as deed: work your and like/as might your
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
to pass please and to see: see [obj] [the] land: country/planet [the] pleasant which in/on/with side: beyond [the] Jordan [the] mountain: hill country [the] pleasant [the] this and [the] Lebanon
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
and be angry LORD in/on/with me because you and not to hear: hear to(wards) me and to say LORD to(wards) me many to/for you not to add: again to speak: speak to(wards) me still in/on/with word: thing [the] this
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
to ascend: rise head: top [the] Pisgah and to lift: look eye your sea: west [to] and north [to] and south [to] and east [to] and to see: see in/on/with eye your for not to pass [obj] [the] Jordan [the] this
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
and to command [obj] Joshua and to strengthen: strengthen him and to strengthen him for he/she/it to pass to/for face: before [the] people [the] this and he/she/it to inherit [obj] them [obj] [the] land: country/planet which to see: see
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
and to dwell in/on/with valley opposite Beth-peor Beth-peor

< Torati 3 >